Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja ya Dharura (Changamoto ya Kupanda kwa bei za Mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa)

Hon. Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja ya Dharura (Changamoto ya Kupanda kwa bei za Mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa)

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kuongea kwa ufupi; la kwanza tupo kwenye kitu tunaita crisis management. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Mbunge, tatizo letu tunataka wananchi wa-feel kwamba Bunge linafanya kazi yake na Serikali inatusikiliza kwenda kulifanyia hili. Naomba tufanye yafuatayo, kwa sababu tunajua chanzo cha tatizo na tunajua tutokee wapi; kuna tozo, kuna kila kitu; watu wanasubiri majibu, ningeomba Serikali kwa haraka iwezekanavyo; tutazungumza mpaka asubuhi hapa hatutafikia mahali isipokuwa Serikali waje na jawabu tunatokaje hapa ili kupunguza maumivu ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wamezungumza huko vita, kitu gani, hatuna tatizo, lakini vita ni opportunity, kwa hiyo huko mbele ya safari tutajua nini cha kufanya, lakini leo tunawaomba sana Serikali njooni na majibu, sasa hivi nini kinafanyika, tupunguze tension ya wananchi ili maisha yarudi kama kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)