Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge ni chombo cha uwakilishi. Ndani ya Bunge hili kila Mtanzania anawakilishwa kwa Mbunge waliyemchagua wao wenyewe. Wananchi wana haki Kikatiba kuona live nini wawakilishi wao wanakifanya na nini kinaendelea ndani ya chombo hiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu zote zilizotolewa na Mheshimiwa Waziri kuhusu kuzuia matangazo ya Bunge Live hazina mashiko hata moja.
Mheshimiwa Waziri akiwa Mwanza alipohojiwa sababu hasa alisema Bunge la Kumi 2010 – 2015 lilifanya maamuzi hayo jambo ambalo ni uongo wa mchana kweupe. Sisi tuliokuwepo wakati huo hatukuwahi kujadili suala hilo wala kutoa maamuzi ya kipuuzi kama hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali leo ieleze Watanzania sababu hasa ya kuzuia matangazo ya Bunge live kwa Watanzania. Kitendo cha TBC kurudia matangazo ya Bunge usiku kuanzia saa 4.30 usiku baada ya kuchuja na kuondoa wasiyotaka yaonekane wakati ambapo watu wamechoka na kazi za kutafuta kipato mchana kutwa na wanatakiwa kupumzika ili wapate nguvu ya kufanya kazi siku inayofuata, ni manyanyaso kwa Watanzania, ni matumizi mabaya ya kodi zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vipaji vya michezo hujengwa kuanzia primary school, secondary school ndipo tunaweza kupata wanamichezo wazuri wenye weledi na wanaoweza kujiajiri kwenye michezo na kuleta heshima kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za michezo zinazotolewa kwa shule zetu kwa watoto wetu huko shuleni ni kidogo sana; hakuna vifaa vya michezo, hawapati mazoezi ya kutosha na walimu wa michezo hawawezeshwi. Serikali imejipanga vipi kuhakikisha michezo shuleni inawezeshwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wanacheza wakiwa shuleni na hata wakiwa majumbani kwao. Viwanja vya michezo kwenye mitaa mingi maeneo mbalimbali hapa nchini yamevamiwa na kujengwa nyumba na shughuli nyingine. Watoto wanacheza barabarani na kila leo wanagongwa na magari, pikipiki na vyombo vingine vya usafiri. Serikali ina mpango gani mahususi kuhalalisha inafanya uhakiki wa viwanja vya watoto wetu vilivyoporwa, kuvamiwa ilimradi kutumiwa na watoto kwa malengo ya michezo na kukuza vipaji vya watoto wetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilipiga marufuku kuwatumia watoto wadogo kwenye maigizo na kutengeneza mikanda ya sanaa za maigizo. Tumeendelea kuona watoto wadogo wakitumika kwenye maigizo na hivyo kuathiriwa kisaikolojia na kushindwa kufikia ndoto zao. Watoto wenye ndogo za kuwa madaktari wanapoingizwa kwenye maigizo wakati akili zao hazijaweza kuamka, automatically tunawahamisha mwelekeo wa ndoto zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ieleze Bunge, kwa nini watoto bado wanaendelea kushirikishwa kwenye maigizo? Umri wa mtoto unajulikana ni miaka 18 kushuka chini.