Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na mimi leo nina maeneo matatu ya kuchangia kwa ajili ya kuishauri Serikali yangu katika masuala mazima ya biashara na uchumi wa nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma research iliyofanywa na Price Waters Cooper kwa projection ya uchumi na biashara ya dunia kwa miaka 27 inayokuja. Ripoti inaonesha the imaging seven economies ambazo zinajumuisha mataifa ya Indonesia, Uturuki, China, Brazil, Mexico na mataifa mengine. Utafiti huu unaonesha kwamba baada ya miaka 27 kufika mwaka 2050 mataifa kama Indonesia yanakwenda kuwa moja ya mataifa yanayokuza chumi zao sana kutokana na biashara na uwekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nalisema hili kwa sababu sisi Tanzania we cannot be jack of all trade, kama nchi alikuwa anazungumza mdogo wangu Mheshimiwa Ezra na Mbunge mwenzangu hapo nimemsikia kwa makini sana. Sisi kama nchi lazima tuwe na vipaumbele vichache ambavyo vitaweza kulifanya Taifa letu liweze kuwa na mambo ya msingi ya kujivunia katika biashara ya dunia. (Makofi)

Leo tunapozungumza habari ya nchi iko katika shortage ya mafuta, hivi ni kweli watanzania mnataka kuniambia sisi Tanzania tumeshindwa kabisa kuwa na uwezo wa kuwa na sufficient ya mafuta katika Taifa letu, mafuta ya kula? hili jambo mimi nimelizungumza Bunge lililopita nilizungumza alikuwa anazungumza Mheshimiwa Ezra. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, uzalishaji wa mafuta kweli tumeshindwa kuwa na mikakati ya kuwa na mashamba na hili mimi nalizungumza Wizara ya Biashara najua mnafanyakazi nzuri na kuna recommendation zenu nitawapa. Wizara ya Kilimo iko na Waziri makini najua it’s doing the best ila ninachotaka kusema ni kwamba hivi ni kweli Tanzania leo sisi ni wa kulia tuna shortage ya mafuta ya kula? With all arable land ambayo Mungu ametupatia kama nchi tunalia habari ya mafuta ya kula. Can we give excuse ya habari ya war in Ukraine for habari ya mafuta ya kula kwa wananchi wetu?

Mheshimiwa Naibu Spika, shida moja tuliyonayo ni kwamba we plan a lot, hatuchukui maamuzi serious ya kufanya maamuzi ya kuleta mageuzi katika Taifa letu. Huu mfano alikuwa anauzungumza Mheshimiwa Ezra Serikali tukiamua kwa kupata wawekezaji tukawa na mashamba peke yake ya mashamba ya alizeti ya mfano maelfu ya heka, mimi ninawaambieni hili Taifa hatuhitaji kuagiza mafuta hapa haturuhusu tu kuwapa deal wafanyabiashara lakini we are killing the economy of the country na biashara kwenye nchi haiwezi kwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi natoa ushauri Serikali Wizara ya Kilimo kaka yangu Bashe you are very smart Waziri wangu. Waziri wa Biashara mwalimu wangu umenifundisha Mzumbe University fanyeni coordination tuhakikishe na tuweke mipango ndani ya kipindi cha miaka kumi hili Taifa liondokane na habari ya utegemezi wa kuagiza mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo linatu-cost pia sasa tunavyozungumza haya mambo mipango lakini hata ukiangalia Tume ya Mipango yenyewe tumeiua. Tume ya Mipango tumeiua hatuna Tume ya Mipango, all these great things tunazozizungumza hatuna Tume ya Mipango. (Makofi)

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumpa taarifa ndugu yangu Kingu kwamba Serikali imechukua hatua na kufuatia ushauri uliotolewa na Wabunge katika Bunge la bajeti lililopita, Serikali imegawa mbegu katika mikoa mikuu mitatu ya alizeti ikiwemo Mkoa wa Singida na mwaka huu peke yake mkoani Singida tumegawa jumla ya tani 1,039 na Mkoa wa Singida baada ya crop survey itatuzalishia jumla ya tani 365,000 za ziada za alizeti zitakazotupatia lita 115,000 za mafuta katika uzalishaji wetu na mwaka ujao wa fedha tutagawa tani 5,000 kwa nchi nzima. (Makofi)

Kwa hiyo, siyo kwamba Serikali haijachukua hatua Serikali inachukua hatua na hii ni budgetary na tumeshaanza kufanyia kazi. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kingu taarifa unaipokea?

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa taarifa ya Mheshimiwa Bashe, kwa kweli sina mashaka na utendaji wa Waziri Bashe, lakini tungependa kuona sasa kwenye market haya anayoyazungumza Mheshimiwa Bashe tuone uzalishaji unapatikana. Kwa sababu sasa hivi scarcity ya mafuta ninyi mnajua wote mnajua nchi iko kwenye scarcity kubwa ya mafuta, lakini kwa sababu ni hatua zinaendelea it’s well and good ndiyo tunahitaji vitu vya namna hiyo vitokee. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili ambalo nilikuwa nataka kulizungumza tulikuwa tuna mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo, mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo mimi nimesoma ripoti ya utendaji kazi wa Bandari ya Salala iliyoko huko Mashariki ya Kati. Ujenzi wa mradi wa Bagamoyo sisi si tumezubaa sasa hivi tumekuwa tunazungumza, lakini nakwambia tukiacha kutekeleza ujenzi wa mradi wa Bagamoyo in next ten years mtaona wenzetu Mombasa ama Msumbiji wame-peak na sisi Tanzania tutabaki kuwa observer. Tukiweza kutekeleza mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo sasa hivi tunazungumza habari za usafirishaji kwenye bahari zimekuwa kubwa, tukiweza kujenga mradi ule wa Bandari ya Bagamoyo, tutaweza kuleta meli kubwa za fifth generation ambazo zitaweza kuifanya Tanzania kuwa hub ya kuchukua mizigo na kuipeleka kwenye nchi za interior ambazo ziko land locked na hiyo itafungua biashara katika nchi.

Sasa shida kubwa ni kwamba tunapozungumza mambo kama haya tunayachukulia taratibu taratibu lakini lazima twende kwa speed ambayo dunia inatutaka kwenda kwa speed kwa lengo la kuwasaidia watanzania katika masuala mazima ya biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine ambalo nilikuwa nataka kulizungumza niipongeze sana Wizara, Wizara niwapongezeni sana...

(Hapa kengele ililia kushiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante, kengele ya pili hiyo. Lakini sasa upate ulifanya nini? Hebu rudia ulifanya haya sekunde mbili. (Kicheko)

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, niitumie nafasi hii kuipongeza sana Wizara na kwenye hili kwa kweli niwapongeze kwa mara ya kwanza nimeona mikataba iliyokuwa yamesainiwa Dubai, nimeona utekelezaji wa ujenzi wa viwanda 200 Kwala ukiendelea kwa macho yangu nimeenda kutembelea, nitoe pongezi sana kwa Katibu Mkuu wa Wizara na Waziri Mwalimu wangu Profesa Kahyarara ni mtu wa matokeo alipokuwa NSSF alisimamia ujenzi wa viwanda vya Bodi ya Nafaka vimetokea na sasa naona ujenzi wa viwanda 200 unaendelea hayo ndiyo mambo tunayoyataka kwa hili Serikali nawapongeza. (Makofi)