Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Madini

Hon. Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Madini

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipatia nafasi ya kuchangia kwenye Wizara hii ya Madini. Namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii ya leo aliyonipatia ya kuzungumzia Madini, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri na timu yake nzima wakiwepo wataalam kwa kazi kubwa wanayoifanya.

Mheshimiwa Spika, tunaona kabisa kwamba mchango wa sekta hii sasa kutoka asilimia 6.3 katika kipindi kama hiki tumekwenda kwenye asilimia saba inaonesha kwamba lengo la Serikali ambalo lilikuwa kwenye mpango mzima kwamba mwaka 2025 tuwe na asilimia 10 linaweza likafikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa kwasababu lengo ni hilo na inaonekana kasi ni kubwa ningeomba sasa tuzidishe sasa tuizidi hiyo asilimia 10 ili ionekane kabisa kwamba tumefanya kazi nzuri zaidi.

Mheshimiwa Spika, pamoja na pongezi hizi nitoe ushauri wa Serikali kama mchangiaji Profesa Muhongo alivyosema dunia sasa ipo kwenye energy transition, hapa kwenye energy transition maana yake tunakwenda kwenye yale madini mkakati, critical minerals na dunia ya sasa inakwenda huko. Kwa hiyo, niwaombe sana GST ambao ninaona hapa wamepewa fedha kama Shilingi Milioni Mia Moja Arobaini na Tatu tu, tuangalie namna gani tunaweza tukawaongezea ili waweze kuingia kwenye kutafiti hayo madini ambayo dunia ya sasa inakwenda.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa ninaangalia hapa Canada wana madini mengi ambayo sitaki niyataje, ni karibu 34 yanaonekana hapa kwenye hizo critical minerals, kwa hiyo niwaombe sana GST na Wizara kwa ujumla iwasaidie sana GST ili waweze kupita kwenye utafiti huu.

Mheshimiwa Spika, niliona imetajwa kidogo kwenye madini ya mkakati, lakini bado haitoshi kwasababu dunia inakwenda huko. Kama tulivyosikia China wanataka kutoa magari nilikuwa ninaona Research moja inaonesha kabisa kwamba gari la umeme linaweza kutumia kama kilo 200 hivi, lakini gari ambalo litakwenda kutumia hizi critical minerals zitatumia kama kilo 40, niliona mtu mmoja amefanya reseach kama hiyo. Kwa hiyo, ningeomba sana tuwaelekeze hawa GST wafanye utafiti wa kutosha ili dunia inapokwenda kubadilika na sisi tubadilike pamoja nao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nijikite sasa kumpongeza Waziri kwa leseni za wachimbaji wadogo 4,490 ambazo zinaonekana kwenye hotuba yake. Hizi hata kwenye Jimbo langu la Busanda kuna watu wamefaidika na leseni hizi lakini niishauri Serikali katika kuwasaidia wachimbaji wadogo nimeona kabisa inaonesha STAMICO wamepitia vikundi vitano, vikundi vitano ndani ya nchi hii kama ndiyo vinaenda kutathminiwa maeneo yao kuonekana kuna madini kiasi gani ni vichache sana, iwezeshwe STAMICO kuhakikisha kwamba inaweza kupitia vikundi vingi.

Mheshimiwa Spika, hapa vinaonekana kwenye Randama Ukurasa Na. 11, vikundi vitano tu vimepitiwa, navyo vinaonekana vimepita Kilindi, Morogoro na Singida, kule kwangu Busanda ina maana hawakupita kipindi chote hiki na kuna wachimbaji wadogo wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile nijielekeze kuonesha kwamba katika wachimbaji wadogo tunaowazungumzia hawa wamekuwa wanasuasua katika kutambua mchanga au mawe kwamba yana dhahabu kiasi gani, na wamekuwa wanatumia maabara hizi za watu binafsi.

Mheshimiwa Spika, ninaishauri mamlaka inayosimamia maabara hizi, watu wetu wamekuwa wanakwenda kupima PPM kiwango cha dhahabu kwenye udongo au kwenye mawe wanaambiwa hapa kunaonekana kuna 18 kumbe amedanganywa, anachukua mtaji mzima kuendelea kufanya kazi kwenye eneo hilo Milioni Mia Tatu, Milioni Mia Nne, akienda kusafisha chenjua anakuta Shilingi Themanini matokeo yake anapata hasara ambayo kwa kawaida inaweza kumpotezea maisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mamlaka inayohusika na maabara hizi ihakikishe kwamba inazipitia kuzikagua ili wananchi wetu wahakikishe kwamba wanapata faida badala ya kupata hasara kwa sababu wamedanganywa na matokeo yaliyofanyika kwenye maabara hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme wazi kwamba yapo maeneo mengi ambayo yameendelea kumilikiwa na watu, hawa watu wenyewe ukiwatafuta kwenye maeneo yetu wanaonekana siyo wakazi wa maeneo hayo kwa sababu ni haki yao kupata maeneo hayo lakini wananchi wetu wanahitaji kuchimba. Ninaomba maeneo hayo ambayo sasa yanamilikiwa na hayafanyiwi kazi Wizara iyashughulikie kuhakikisha kwamba yanaweza kutaifishwa yakarudishwa mikononi mwa wananchi ili waendelee kufanya uchimbaji mdogo mdogo kwa sababu asilimia 35 ya wachimbaji wetu ni wachimbaji wadogo, nao wanachangia pato hilo la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitoe angalizo kwamba tunaweza tukaiona Wizara hii inachangia sana kwasababu bei ya dhahabu imepanda, niwaombe sana Wizara tuhakikishe kwamba majadiliano negation teams zifanye kazi kwa haraka kuongeza watu wanaoendelea kuwekeza kwenye sekta hii. Kwa mfano, tuna special mining license mbili tu, ukiziona zimekuja mbili zimekuja kipindi hiki lakini za kwanza ambazo special mining license tumekuwa nazo zimepatikana nafikiri mwaka 2000, 2002 na 2003 kwa hiyo tuna miaka karibu 15 hadi 20 ambayo tulikuwa hatujatoa leseni za hivi karibuni.(Makofi)

SPIKA: Haya ahsante sana Mheshimiwa Kengele imeshagonga.

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)