Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nawapongeza sana kwa kukamilisha mpango kabambe wa hifadhi ya mazingira kama ilivyojionesha katika ukurasa wa 36 wa hotuba ya bajeti. Pamoja na pongezi hizi ninaomba kutoa ushauri kama ifuatavyo: -

Kwanza ni kuhusu kukijanisha Dodoma; ninashauri kushirikisha vyuo vya elimu ya juu na kati katika kukijanisha Dodoma. Kwa mfano, tunaweza kusema kila wanafunzi wawili wapande mti na kuulea katika muda wote wa masomo. Tuna vyuo kama vile UDOM, St. John, Mipango-IRDP, CBE, Hombolo na baadhi ya vyuo binafsi kama vile DECA. Ikiwa wanafunzi wanakaa almost miezi tisa katika mwaka, ninaamini wakipewa mche na kukawa ni sehemu kwa mfano ya kigezo cha kupata mkopo, tunaweza kusaidia kukijanisha maeneo ya vyuo na maeneo yanayozunguka.

Pili, COP26 na namna ya kunufaika na fedha za mifuko ya GCF, GEF, Adaptation Fund n a kadhalika, nilifuatilia mkutano wa Glasgow, niliona ambavyo Mheshimiwa Rais alivyoyasihi mataifa makubwa kuheshimu pledge zao katika kuzisaidia nchi zinazoendelea kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi. Tumeona CRDB wamepata fedha kwa mfumo huu.

Mheshimiwa Spika, nashauri tuzisaidie taasisi nyingi zaidi kama vile vyuo vikuu, NGOs na kadhalika ziweze kupata fedha hizi ambazo nyingi ni grants. Ukifuatilia kwa ukaribu utafahamu kwamba ili ku-access hizi funds kuna vigezo kama vile kupata accreditation. Nchi kama Kenya, Rwanda na Morocco wamekuwa wanufaika wa hizi funds na zimesaidia katika miradi ambayo inasaidia kuinua maisha ya wananchi wa kawaida. Kwa mfano kama ilivyo katika mikoa ya Iringa na Njombe ninaamini funds hizi zingeweza kuhamasisha zaidi suala la kupanda miti katika mikoa mingine kadri ya species ambazo zitafaa.

Mheshimiwa Spika, tatu ni kuhusu hewa ukaa/carbon credit; wananchi wengi wa Mafinga/Mufindi wamekuwa wakiomba kupata elimu kuhusu suala hili. Tunawashukuru sana Wakala wa Misitu Tanzania-TFS ambao waliwezesha ziara ya mafunzo kwa Madiwani wa Mafinga na Mufindi kutembelea Wilaya ya Tanganyika kuhusu manufaa ya hewa ukaa.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Mufindi ama kwa kutojua au kwa shida zao waliuza maeneo yao kwa makampuni makubwa kama vile green resources ambapo kuna maelezo yasiyo rasmi kwamba waliahidiwa kwamba waachie maeneo yao na kwamba watanufaika na malipo ya hewa ukaa. Kwa sababu suala hili naweza kusema ni complicated, nashauri itolewe elimu kwa kuanza na semina kwa Wabunge na baadae kwa Wenyeviti wa Halmashauri na wadau wengine kadri mtakavyoona inafaa ili tuweze kufahamu ni vigezo gani vinapaswa kuzingatiwa ili taasisi au mwananchi apate kunufaika na masuala ya hewa ukaa. Kwa mfano ilivyo sasa, wananchi wa Mufindi na maeneo ya Morogoro kama vile Uchindile wanadai kuwa fedha za hewa ukaa zinatolewa, lakini wanufaika ni makampuni makubwa yaliyopanda miti katika ardhi ya vijiji.

Mheshimiwa Spika, nne ni kuhusu kupanda miti milioni 1.5 kwa kila Halmashauri; kama nilivyoshauri katika kukijakinisha Dodoma, nashauri ushiriki wa shule za msingi, sekondari na vyuo, sio katika kupanda tu bali katika kuitunza miti. Kwa sababu hakika tumekuwa tunapanda miti kila mwaka lakini inayo-survive ni michache mno.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.