Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya, pia nimpongeze Waziri na timu yake yote kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na upungufu mkubwa wa watumishi katika kada zetu mbalimbali, kwa Wilaya ya Lushoto kuna upungufu kwenye kada ya afya na elimu zaidi ya watumishi 11,000 hawa ni katika kada mbili, bado kada nyingine. Kwa hiyo, niiombe Serikali kwa kipindi hiki cha bajeti Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto iweze kupata walimu hao niliyoorodhesha hapo juu, hasa ukizingatia Wilaya ya Lushoto ina shule nyingi pamoja na vituo vya afya na zahanati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mfuko wa TASAF unasaidia sana wananchi wetu, lakini kunakuwa na changamoto hasa kwa watu wa vijijini wengi wao kutopata fedha hizi za TASAF na ukikuta baadhi ya wanaopata unakuta wengi wao sio walengwa, hii inatutupia lawama sisi Wabunge. Lakini pia pesa za TASAF ziwe na account yake tofauti na ilivyo kwa sasa na pia inaleta mkanganyiko hasa pale pesa zinapoingia, zinachukua muda mrefu kuzipeleka kwa wahusika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia niiombe Serikali ipeleke pesa hizi vijijini kwani huko vijijini ndiyo kuna wahitaji zaidi kuliko mjini, pia fedha hizo ziongezwe kiwango wanachopewa ni kidogo mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na malalamiko mengi kwa wastaafu wetu hawapewi stahiki zao kwa wakati pindi wanapostaafu, unamkuta mstaafu anafuatilia mafao yake zaidi ya miaka miwili mwisho wa siku anafariki bila kupata mafao yake na ukizingatia wengi wanaostaafu hawana kazi nyingine ya kufanya. Kwa hiyo, mstaafu huyu unamkuta maisha yake yanakuwa ni ya taabu na mwisho wa siku humpelekea kuiaga dunia. Niiombe Serikali yangu tukufu iwalipe wastaafu wetu hawa kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watumishi wengi wanahama kwenye Halmashauri kwa sababu ya kupata mshahara mdogo tofauti na idara nyingine, mfano sasa hivi watumishi hao wanakimbilia kwenye mashirika kama TANESCO, TARURA, TPDC na TASAF, kwa hiyo huku wanapata mishahara mikubwa kuliko hawa wa Halmashauri, ukizingatia elimu zao ni sawa.

Kwa hiyo, niiombe Serikali iweke uwiano sawa wa mishahara ili kuondoa ubaguzi na sintofahamu na kufanyakazi kinyoge kwa hawa watumishi wa Halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.