Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwashukuru na kuwapongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mawaziri na viongozi wote wa wa Ofisi ya Rais – Utumishi, kwa uongozi wao na utendaji uliotukuka wa Ofisi ya Rais – Utumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kutumia fursa hii kukupongeza wewe binafsi, Spika na uongozi wote wa Bunge kwa uongozi wenu mahiri na wenye ubunifu wa hali ya juu katika kuongoza mhimili wa Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi, kwa hotuba nzuri iliyojaa ubunifu mkubwa na imedhihirisha utayari wa Taifa letu katika kuboresha maisha ya wananchi na pia utayari wetu wa ushindani wa Kimataifa (National Competitiveness). Bajeti hii inaenda sambamba na dhima ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/2022 – 2025/2026 ambayo ni kujenga uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mapitio ya kipindi cha bajeti 2021/2022, Serikali kupitia Wizara ya Utumishi na Utawala Bora imesimamia kwa uadilifu na ufanisi mkubwa masuala yote ya utumishi na hasa kurudisha uwabikaji kazini iliopelekea ufanisi mkubwa hasa kwenye utekelezaji wa miradi. Jimbo la Mbeya Vijijini limenufaika kupitia miradi ya TASAF ambapo imebadilisha maisha ya wananchi katika vijiji husika. Pia kwa kusimamia vizuri, rushwa na upendeleo umepungua kwa kiasi kikubwa kupelekea ufanisi mkubwa sehemu za kazi na hata miradi kukamilika kwa ufanisi mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mafanikio hayo makubwa, napendekeza kuendeleza mafunzo ili kuboresha weledi wa watumishi ikiwemo upanuzi wa Chuo cha Watumishi Mbeya na eneo muafaka kwa ujenzi wa chuo kipya na cha kisasa ni Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya ambapo kuna maeneo mazuri ikiwemo yaliyokuwa mashamba ya Tanganyika Packers, Mbalizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na upungufu mkubwa wa watumishi katika sekta mbalimbali, napendekeza Serikali iendelee kutoa ajira zaidi hasa kwenye maeneo ya kuchochea uchumi na pia sekta ya afya, elimu na kilimo. Kutokana na idadi kubwa ya wahitimu kukosa ajira na wametapakaa kila kona ya Tanzania hasa vijijini, napendekeza Serikali kuhakikisha ajira zinatolewa kwa usawa wa maeneo yote ya Tanzania kulingana na sifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na majukumu na unyeti wa mashirika ya kadhaa ya umma ikiwemo ushindani wa kupata watalaam wazuri, mashirika haya yaruhusiwe moja kwa moja kutoa ajira ili yaendane na mahitaji yao na Tume ya Ajira wawe na jukumu la ushauri/udhibiti. Taasisi kama CAG kisheria anatakiwa awe huru ikiwemo uhuru wa kuajiri na hata taasisi kama mabenki, TANESCO, Bandari, TRA ni muhimu wakapewa uhuru wa kuajiri kulingana sifa ila kupata watalaam wazuri kiushindani na pia kulingana na bajeti za mashirika husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na maboresho ya mfumo wa TASAF, napendekeza pia kuboresha zaidi mfumo huo ikiwemo msukumo wa miradi ilenge maeneo yatakayochochea uzalishaji wa mali ili zisaidie jamii kwa upana mkubwa. Pamoja na maeneo ya uzalishaji, msukumo ujumuishe kuimarisha masoko ya bidhaa zitakazozalishwa katika maeneo ya mradi. Miradi ilenge kuboresha elimu na hata kusomesha watoto wanaotoka kwenye kaya maskini ya maeneo husika. Serikali iboreshe taratibu za kupata maeneo ya miradi ya TASAF ili kupunguza malalamiko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.