Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha mchango wa maandishi kama ifuatavyo kuhusu changamoto za kimaendeleo jimbo la Singida Kaskazini; kwanza tatizo la upungufu mkubwa wa watumishi katika Idara ya Elimu Msingi ina upungufu wa walimu 1097, Idara ya Elimu Sekondari ina upungufu wa walimu 151 na sekta ya afya ina upungufu wa watumishi 542.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye utawala; Halmashauri ina upungufu watumishi 47; Watendaji wa Vijiji 24 kati ya 84 na Watendaji wa kata sita, jumla ni upungufu wa watumishi 2867.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kuwe na msawazo, Mikoa na Halmashauri zenye upungufu wa asilimia 50 na kuendelea zipewe kipaumbele katika kupatiwa watumishi. Halmashauri ya Wilaya ya Singida ni muhanga wa tatizo hili. Naomba sana ipatiwe watumishi hawa.

Pia naomba fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa Kituo cha Afya Ngimu ambapo boma lina miaka 14 sasa (boma lipo usawa wa linta). Pamoja na zahanati ya Pohama ambayo iko lenye linta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba vifaatiba katika Hospitali ya Wilaya Ilongero na Vituo vya Afya Mgori na Msange. Pia ambulance nne kwa mchanganuo ufuatao; moja kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Ilongero, moja kwa ajili ya Kituo cha Afya Mgori, moja kwa ajili ya Kituo cha Afya Msange na moja kwa ajili ya Kituo cha Afya Makuro.

Kuhusu TARURA iendelee kuongezewa fedha katka Wilaya ya Singida DC iweze kujenga daraja la Mgori ambalo ni drift huuwa watu, daraja la Mpambaa na kuboresha barabara za makao makuu ya Wilaya na za miji midogo ya Ilongero, Ngamu, Msange na Mtinko.

Pia ni ushauri kuwa zabuni za barabara zitangazwe kuanzia mwezi aprili ili ziweze kutekelezwa wakati wa kiangazi (mwezi Julai hadi Novemba).

Mheshimiwa Mwenyekiti,napendekeza maslahi ya Madiwani yaboreshwe, walipwe mshahara wa kila mwezi usiopungua shilingi milioni moja. Pia walipwe posho za vikao kwa uwiano sawa kwa kuzingatia mazingira ya sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri eneo la manunuzi liboreshwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha.