Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi kubwa inayofanywa na Serikali, naomba kushauri yafuatayo; kwanza Hospital ya Wilaya ya Nansio haina x-ray machine. Naomba mtusaidie digital x-ray machine ili kuokoa maisha ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Kituo cha Afya cha Nakatunguru kiongezewe miundombinu ili kipunguze msongamano katika Hospital ya Wilaya natatu, kuhusu upungufu wa watumishi kwa kada za afya na elimu unaathiri sana utoaji wa huduma kwa wananchi Wilayani Ukerewe, naomba katika mgao ufuatao wa watumishi Jimbo la Ukerewe liangaliwe kwa upekee.