Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni mpongeze na kumshukuru Rais wetu Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya hasa kwa kutupatia fedha za miradi ya maendeleo katika majimbo yetu, Mwenyezi Mungu azidi kumbariki Rais wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimpongeze Waziri wa TAMISEMI pamoja na Katibu Mkuu bila kuwasahau wasaidizi wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizo katika Jimbo la Lushoto lina changamoto zifuatazo; nikianza na kada ya afya; katika Jimbo la Lushoto lina Tarafa mbili ambazo ni Tarafa ya Lushoto na Tarafa ya Mlola, Tarafa ya Lushoto haina kituo cha afya hata kimoja, hivyo kuna upungufu wa vituo vya afya vitatu ambavyo wananchi wameshaanza kujenga kwa kutumia nguvu zao wenyewe, vituo hivyo ni kama ifuatavyo; Kituo cha Afya Gare, Kituo cha Afya Kwai na Kituo cha Afya Makanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba katika bajeti hii Serikali itenge pesa kwa ajili ya kumalizia vituo hivi vinavyojengwa kwa nguvu za wananchi na vituo hivyo mpaka sasa vina miaka mitano bado tu mpaka sasa havijatengewa fedha, pamoja na nyumba za watumishi, vifaa tiba pamoja na watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kada ya elimu kuna changamoto kama zifuatazo; niaze na sekondari; sekondari nyingi zina upungufu wa maboma, ukarabati, mabweni, uzio pamoja na maabara. Sekondari zifuatao ndiyo zenye chagamoto za mahitaji tajwa hapo juu ni Sekondari ya Mlongwema, Sekondari ya Mdando, Sekondari ya Kweulasi, Sekondari ya Makole, Sekondari ya Balozi Mshangama, Sekondari ya Malibwi, Sekondari ya Ntambwe, Sekondari ya Kireti na Sekondari ya Kwai na Sekondari ya Kwemashai. Hizi ndiyo sekondari zenye changamoto kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za msingi zenye uhitaji ni hizi zifuatazo; Shule ya Msingi Ungo, Shule ya Msingi Hondelo, Shule ya Msingi Ngulu, Shule ya Msingi Kilangwi, Shule ya Msingi Handei Boheloi, Shule ya Msingi Kwemashai, Shule ya Msingi Gare B, Shule ya Msingi Bombo Ngulwi, Shule ya Msingi Ngulwi, Shule ya Msingi Mbula B na A na Shule ya Msingi Kwembago. Hizi ndiyo baadhi ya shule za msingi zenye changamoto kubwa,kama nilivyo ainisha hapo juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upannde wa TARURA katika Jimbo la Lushoto kuna changamoto ya barabara ambazo hazipitiki kabisa toka wakati wa mafuriko na hazijawahi kutengewa fedha, barabara hizo ni barabara ya Dochi - Ngulwi hadi Mombo kilometa 16, barabara ya Kwedaraja kupitia Kwemashai hadi Kwelushega kilometa nane, barabara ya Kwekanga, Makole hadi Ngwelo kilometa sita, barabara ya Kihitu - Ngwelo - Kaya hadi Kigulunde kilometa saba, barabara ya Kizara – Ngulu - Kilangwi hadi Kwelugogo kilometa 11, barabara ya Boheloi, Makanka hadi Masange kilometa tisa, barabara ya Kilole kupitia Ula hadi Ungo kilometa tisa, barabara ya Kilole hadi Kweboma kilometa nne na barabara ya Ntambwe hadi Kwalei kilometa saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizi ndiyo zinazotoa mazao kutoka mashambani hadi mjini, kwa hiyo hizi ni barabara muhimu hasa kwa kuchochea uchumi wa sehemu hizo, niiombe Serikali yangu tukufu itenge pesa kwenye bajeti hii ili barabara hizi ziweze kuhudumia wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali yangu tukufu iwatambue wazee wa nchi hii kwa kuhakikisha wanapata kadi za bima ya afya sambamba na kupata huduma inayostahili kuliko jinsi ilivyo sasa, kwani wanafika hospitali hawapati huduma zaidi ya kurudishwa au kuandikiwa dawa kwenda kununua kwenye maduka ya dawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja ya kwamba Serikali imetenga dirisha la wazee, pia niishauri Serikali inapotoa pesa za vituo vya afya au zahanati kwenye ramani ya jengo waongeze chumba cha kuhudumia wazee tu, sambamba na hayo kuna haja ya Serikali kujenga kliniki za wazee na ikiwezekana wazee hao waende kliniki kila mwezi kwa ajili ya kuangalia afya zao, kwani katika nchi hii wazee ni hazina na ndiyo tunu ya nchi yetu, kwa hiyo lazima tulinde afya zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niungane na Waheshimiwa Wabunge kuhusu kuongeza posho za Madiwani wetu, naunga mkono hoja iliyotolewa na Waheshimiwa Wabunge wenzengu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja mkono kwa asilimia mia moja.