Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kupata nafasi hii. Awali ya yote niipongeze kwa namna ya pekee hotuba ya Kambi ya Upinzani Bungeni ambayo imefafanua mambo muhimu na imeitendea haki sekta hii ya habari. Nianze kwa kupongeza kazi nzuri ambazo zinafanywa na waandishi wa habari hapa nchini, kazi zinazofanywa na wasanii, kazi zinazofanywa na wanamichezo mbalimbali hasa wale wanaojitolea kwa nguvu zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nami niungane na Mheshimiwa Zitto kwamba hata katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri, pamoja na kuisahau timu ya Taifa Stars hata Twiga Stars wamefanya kazi nzuri sana na walifuzu South Africa baada ya kuichapa Eritrea kwa bao nne kwa mbili, tulipaswa tuwaenzi kinadada hawa ambao wanafanya vizuri na wapo katika list ya timu nane bora za Afrika zinazofanya vizuri.
Baada ya kusema hayo vilevile Mheshimiwa Waziri ameshindwa hata kutueleza ni jinsi gani hii Wizara inaendelea kuwaenzi wanamichezo ambao wametumia nguvu na jasho lao kwa mfano Ndugu Francis Cheka, ambaye baada ya kumchapa Mserbia, hivi sasa Ndugu Francis Cheka, anaokota chupa, ndiyo ajira yake aliyonayo hivi sasa mkoani Morogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninatoka Morogoro ninamfahamu, nimekuwa mwandishi na nimekuwa nikiandika habari zake, kungekuwa na mpango wa kuendelea kuwaenzi watu hawa siyo tu pale baada ya kumaliza pambano, angalau awe role model aendelee kufanya kazi zake vizuri na vijana wengine wavutiwe na kazi nzuri ambayo anaifanya kwa maana tuone ni yapi manufaa ya yeye kupigana na kupata ushindi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo niende kwenye suala ambalo mwaka huu Aprili 15, Idara ya Habari, Mawasiliano ya Bunge ilitoa taarifa zake kwa vyombo mbalimbali vya habari, kwamba inaanza mpango wa kuwa na feed maalum ambayo tv itakuwa inarushwa na Bunge. Hali kadhalika Waziri naye alifika Bungeni na akatudhihirishia hilo, kwamba hivi sasa taarifa za Bunge zitakuwa zinawafikia wananchi kwa uhalisia, kwa high quality na tukawa tunaamini hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu huu ambao wanasema wameutoa katika Mabunge ya Jumuiya za Madola, utaratibu huu hapa kwetu kidogo ni tofauti, feed maalum zinatumika kwa nchi ambazo hasa waliangalia wingi wa vyombo vya habari, kuondoa congestion ya waandishi wa habari wote kuingia kwenye Bunge kupiga picha, ikizingatiwa kwamba waandishi wa television lazima awe mwandishi na mpiga picha, achana na redio achana na magezeti, sasa wakawa na mpango maalum ambao utasaidia Bunge liwe na television yake isaidie vyombo binafsi kila mmoja kwa wakati wake aweze ku-rely hizo information na kuzisambaza katika vyombo vyake. Wakati huo huo wananchi wawe na uwezo wa ku-access hiyo television na kuangalia ni kitu gani kinachojiri Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kwetu ni tofauti na kinachofuata hivi sasa, tangu kuanza kwa mpango huu tumefanya monitoring ya day to day, kuna vitu ambavyo tumevibaini, mojawapo ni kufanya editing ya kupitiliza, taarifa tunazozizungumza, taarifa ambazo zinakosoa Serikali hazipewi nafasi, uchujaji huu wa namna hii ambao mwishoni mnatoa vitu vile ambavyo tu vinapendeza Serikali hatuwatendei haki wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeangalia hata uwiano wachangiaji wa upande wa Serikali na kambi pinzani, hakuna uwiano sahihi, tuna ushahidi, tunarekodi, na tumefanya monitoring za kutosha. Waziri Kivuli wa Ulinzi Mheshimiwa Juma Hamad Omar akiwasilisha taarifa yake hapa, amepewa dakika tatu tu, tena za mwishoni za kushukuru, waandishi wa habari wameshindwa kuiandika ile habari, na kama mli-monitor saa mbili habari hiyo haikuweza kutokea, sasa uchujaji wa namna hii tunakwenda wapi, kama tuna mambo ya feed maalum? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini sasa waandishi wapiga picha wasiruhusiwe wakaingia wakachukua kile ambacho wanafikiri kitafaa, kuendelea kuwaruhusu waandishi wa magazeti na wapiga picha kuingia, huku waandishi wa television wakisubiri nje na baada ya kurekodi wanapelekewa clip kwenye external ambazo tayari zimeshachujwa, waandishi hawa wataandika nini, ushahidi upo na tunafuatilia na tunajua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, licha ya hilo mpango huu wa feed maalum bado quality yake ya picha siyo nzuri, mfumo unaotumika waandishi wa habari wakichukua ni lazima waende waka-condense lazima waende waka-convert kwenye adobe kwa maana hiyo wakatanue picha quality inapungua, hiyo ndiyo hali halisi. Kwa maana hiyo, kuna haja sasa ya kufikiria ili kuondoa utata kwa waandishi hawa wa television pamoja na kuwepo huu mfumo wa Bunge lakini wawe na uwezo wa kupiga picha kwa quality ambazo wanafikiri zinakidhi vigezo kwenye vyombo vyao vya habari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Serikali isiruhusu mpango huu pamoja na hoja za awali kwamba ni gharama, Mheshimiwa Nape alituambia ni shilingi bilioni nne tulifanya assessment za kutosha, tukagundua wala haifiki bilioni Nne ilikuwa ni shilingi bilioni 2.1, wadau wamejitokeza wako tayari kusaidia wamezuiwa, mpango huu bado unaendelea kuwakwamisha waandishi wa habari kufanya kazi zao kwa uhuru, hili ni jambo ambalo Serikali inapaswa kuliangalia upya. Televisheni ya Taifa (TBC) inafanya nini kama inaendeshwa kwa kodi za Watanzania, kwa nini haipewi jukumu hili la kupeleka hizi taarifa kwa wananchi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo mengi, katika taarifa ya Waziri amezungumza mambo mbalimbali, lakini sijaona mahali ambapo amekuja na mpango wa kuwasaidia waandishi wa habari ambao wanafanya kazi katika mazingira magumu. Waandishi wa habari wanafanya kazi kutwa nzima, hawana mikataba, hawana maslahi mapana, lakini amekuja na mkakati kwamba lazima walipie Press Card kwa shilingi 30,000 ili kuingiza mapato katika Wizara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachosema siyo hilo tu, Wizara kama inataka kumsaidia mwandishi wa habari ingekuja na mpango ambao ungewabana wamiliki wa vyombo vya habari walau kutenga asilimia fulani ya kuwasaidia waandishi hawa wawe na bima za afya, wawe na security za kazi, waweze kufanya kazi yao kama kweli tunatambua mchango wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kweli mnatambua mchango wake wewe mwenyewe binafsi Waziri kila unapopita, kila unachofanya, hufanyi bila waandishi wa habari, lakini inapokuja kuhusu masuala yao hapa hatujaona sehemu ambayo umejikita kupambania maslahi ya watu hawa! Zaidi ya hayo umenukuliwa ukisema sasa unataka kuja na mkakati wa waandishi wa habari kuwa na degree, ni jambo la ajabu sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi zilizoendelea nyingi watu wenye taaluma ya diploma ndiyo wazalishaji wakubwa na hata hapa nchini tunatambua mchango wa walimu wenye diploma, wauguzi, madaktari wenye level ya Assistant Medical Officer (AMO) wanafanya kazi nzuri sana, lakini ni kwa nini inapokuja kwa waandishi wa habari kije kigezo cha degree? Tulitegemea kuona mikakati kwamba nini kifanyike walau wapate muda wa kujiendeleza…
MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Siungi mkono hoja.