Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia jioni hii Wizara yetu ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Wizara ambayo mimi ni mdau mkubwa kwenye sekta hii. Nianze kwanza kwa kumpongeza Waziri Mheshimiwa Nape pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Anastazia Wambura kwa kuteuliwa kushika nafasi hii, sisi wanamichezo tuna imani nao, najua bado muda ni mapema tuwape muda ili waoneshe njia na nina uhakika tutafanya vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na jambo ambalo wenzangu wamelipitia pitia ni hili la Sheria ya Bahati Nasibu. Kwanza, lazima tuelewe Shirika hili la Bahati Nasibu limekuwepo kwa muda mrefu, na sidhani kama ile bahati nasibu tuliyokuwa tunaifahamu mpaka sasa ipo. Ni vema sasa Serikali ikabadilisha sheria, Sheria ya Bahati Nasibu ya Taifa ihamishiwe Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Nasema hivi kwa sababu sheria haisemi mapato ya bahati nasibu yanaenda wapi lakini tunaelewa kabisa kwamba bahati nasibu ni michezo ya kubahatisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye michezo ya kubahatisha kuna michezo mingi tu ya kubahatisha, kuna casino, kuna betting, kuna mapato pia yatokanayo na michezo mbalimbali yanayofanywa na makampuni ya simu. Tuna imani sana pesa nyingi zinapatikana kule na zinatosha kabisa kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Michezo (Sports Development Fund). Mfuko huu ndiyo unaweza ukafanyakazi ya kuendeleza michezo badala ya kuhangaika, ni fedha nyingi sana na hata nchi zingine zina mfuko kama huu. Hakuna haja ya kuhangaika kupitisha kikombe kwa ajili ya kuchangia, lakini muda mwingi hii bahati nasibu ya Taifa na kwa vijana wa sasa hata hawaelewi kazi gani hasa inafanya.
Kwa hiyo ushauri wangu Mheshimiwa Nape ukae na viongozi wengine, mlete sheria hapa Bungeni tubadilishe, Sheria ya Bahati Nasibu ibadilishwe. Bahati nasibu kwa sasa iko chini ya Wizara ya Fedha, bahati nasibu inapaswa kuwa chini ya Wizara ya Michezo, maana yake hii ni michezo ya kubahatisha, hii ni kekundu na keusi umeliwa ndiyo maana yake hii. Kwa hiyo ni vizuri ikaletwa kwenye Wizara yako ili mapato haya na uanzishwe mfuko huu nimesema Sports Development Fund, mfuko huu ndiyo unaweza kuwa mkombozi wa kazi mbalimbali za michezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uwanja wa Taifa, kama ilivyo jina ni Uwanja wa Taifa. Tumekuwa na uwanja wa Taifa sasa na Uwanja wa Uhuru, huu uwanja wa uhuru ndiyo tulizoea kuuita Uwanja wa Taifa au shamba la bibi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ku-declare mimi ni kati ya wale tunaoleta timu za nje kucheza Tanzania, kwa hiyo ninayoyaeleza ni ya ukweli na hakika. Viwango au tozo kwenye uwanja wa Taifa ni vingi mno, tunanyonya jasho la wachezaji na viongozi wanaotengeneza timu hizi, ukicheza Uwanja wa Taifa iko VAT asilimia 18, iko gharama ya mchezo asilimia 15, lakini iko asilimia tano kama ni CRDB asilimia tano lakini kama hii Max Malipo ambayo inazungumzwa kuletwa sasa ni asailimia tisa. Kwa hiyo, utaona kabisa kuna karibu asilimia 42 ya mapato yote yanapotea kwenda kwenye vyanzo hivi. Uwanja wa Taifa umejengwa na Serikali kama ambavyo tunapita kwenye madaraja na kutumia barabara hizi ni huduma, Serikali haifanyi biashara na hata kama ikifanya biashara haiwezi kufanyia biashara jasho la wachezaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima sasa wakati umefika tozo hizi zipungue, ukiwa Uwanja wa Taifa mbali na hizi nilizosema yako makato mengine ya umeme, usafi sasa vyote hivi kama mmekata asilimia 15 ya mchezo kwa nini mkate tena umeme, kwa ni mkate usafi, wapo Wachina pale na wenyewe wanalipwa kiajabu ajabu, ukienda pale yaani kama na wewe ni mshiriki wa kuagiza timu, unaweza ukatoka pale hata senti tano hujapata kwa sababu ya tozo hizi, yaani zile asilimia 58 zinazobaki, baadaye zinapotea hapo bado timu hazijagawana, hazijafanya nini. Kwa hiyo, niiombe sana Serikali iangalie tozo za Uwanja wa Taifa.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, liko suala la TFF na TRA. Mheshimiwa Waziri nimwombe sana sakata hili limekuwa linazungumzwa tu, hebu wakati wa majumuisho njoo na taarifa tujue nani mwenye tatizo kati ya TRA, TFF na Hazina kwa sababu deni hili siyo deni halisi la TFF, deni hili ni la Serikali ukishasema nitamlipa mshahara huyu maana yeke ni pamoja na kodi yake kwa maana ya PAYE. Sasa utasemaje unalipa mshahara unalipa net pay kwa nini usilipe na kodi na Serikali iliji-commit kulipa mshahara ya hawa makocha kutoka nje, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri njoo na majibu hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la mechi ya Brazil limezungumzwa hapa, mechi ya Brazil na Taifa Stars, mechi hiyo jamani haikuwa chini ya TFF ilikuwa chini ya Kamati iliyoundwa na Serikali na fedha zote walichukua, wao ndiyo wenye wajibu sasa makato ya VAT tena yanaongeza deni ambalo TRA inakuja kuchukua.
Mimi nadhani mnawaonea TFF, akaunti tunaambiwa zimefunguliwa lakini fedha imechukuliwa, kwa nini fedha zichukuliwe na kama akaunti imefunguliwa iko vizuri, lakini je, TRA ina maana wameona hela tu za TFF zinaweza kumaliza matatizo tuliyonayo ya maji, umeme na nini? Nadhani Waziri njoo hapa utuambie nini kimetokea kwenye fedha za mechi ya Brazil pamoja na Taifa Stars mpaka kufikia TFF inafungiwa tunapata taabu, mpira sasa tunaendesha kwa madeni, haifai. Mimi ni Mjumbe wa TFF kwa hiyo ninayoyasema ni mambo ambayo nayajua vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, liko tatizo la nyasi bandia uwanja wa Nyamagana, nyasi bandia za uwanja wa Nyamagana Halmashauri ya Jiji la Mwanza ililipa kiasi chake ambacho kilitakiwa kabla ya FIFA kuleta msaada ule tukalipa, nyasi bandia hizi sasa imekuwa kama story, lini zitafika Mwanza na lini kazi ile itakwisha maana yake sasa uwanja ule umegeuka kuwa gofu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine mwaka 2014 mimi niliongozana na timu ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu kwenda Brazili kwenye Kombe la Dunia, timu ile ikashinda ikaja hapa Bungeni mkaishangilia sana, zikatoka ahadi za Serikali nyingi sana. Mojawapo ni uwanja, Serikali iliahidi kutupatia uwanja kwa ajili ya watoto hawa ambao ni mabingwa wa dunia, hapa hakuna bingwa wa dunia mwingine, ni wale watoto wa Mwanza ambao mwaka kesho kutwa tunaenda Urusi kutetea kombe la dunia.
Mheshimiwa Nape najua utakuwa bado upo tusaidieni nauli za kwenda kwenye kombe la dunia, mashindano yale hufanyika kila kabla ya world cup mtusaidie kama Serikali kwenda kule, pia tunataka ahadi ya Serikali ya kutupatia uwanja.
MHE. JOHN P. KADUTU: Nakushukuru naunga mkono hoja.