Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa fursa kuhitimisha hoja yangu, lakini pia nawashukuru sana waheshimiwa Wabunge kwa michango ambayo wametoa ambayo kusema kweli wameboresha hoja tumepata jumla ya wachangiaji 14; ambapo Wabunge ni tisa na Mawaziri watano ambao wameshehenesha na kuiboresha hoja yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Sheria Ndogo ni jicho la Bunge la kutazama jinsi gani ambavyo sheria ndogo zinatekelezwa, zinatungwa, zinakwenda na Sheria na Katiba na nchi yetu inafuata mfumo wa utawala bora. Sasa ili kuwe na utawala bora kuna mgawanyo wa majukumu kuna mihimili mitatu na Mhimili wa Bunge ndio wenye jukumu la kutunga sheria zote za nchi hii ziwe sheria mama, ziwe sheria ndogo na kadhalika, hiyo inaelezwa kwenye Ibara ya 64 ya Katiba yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa chini ya Ibara ya 97(5) Bunge linaweza kukasimu madaraka yake kwa vyombo mbalimbali, kwa mtu mmoja mmoja, kwa idara mbalimbali, kwa vyombo mbalimbali Serikalini ili kutunga sheria ndogo. Sasa kukasimu siyo kuachia, siyo kukabidhi, unabaki na madaraka yote, lakini unampa mtu mwingine afanye kwa niaba yako, akikosea au asipotekeleza unamrudi, unamwambia rudisha hapa unaendelea mwenyewe.

Kwa hiyo, Bunge ndio linafanya kazi hiyo ya kuhakikisha kwamba sheria ndogo zlilizotungwa na mamlaka mbalimbali zinakwenda kulingana na Katiba, sheria mama na miongozo mingine ambayo tumejiwekea na ndio maana nasema Kamati hii ni jicho la Bunge la kutazama utungaji huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge lina wajibu wa kuhakikisha kwamba hakuna sheria ndogo yoyote itakayotungwa ambayo ni kero kwa wananchi, na ikiwepo lazima Bunge liingilie na liseme.

Kwa hiyo, taarifa yetu inachosema ni kwamba kuna baadhi ya Wizara, Halmashauri na mamlaka nyingine ambazo zinatunga sheria mbovu au hazitungi sheria ambazo ni kero kwa wananchi, sasa tukinyamaza tutakuwa tunaachia wajibu wetu ambao tunatakiwa tuufanye, hatuwezi kunyamaza lazima tuseme na tusahihishe pale ambapo kuna matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ziko nyingi Waheshimiwa wamesema Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda amesema hapa saa nane za usiku unaenda kumdai mtu ushuru nyumbani kwake kwa nini? Mheshimiwa Damas Ndumbaro, Waziri WA Katiba na Sheria amejibu, lakini nafikiri hakumwelewa Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kudai ushuru ni jambo la kawaida, ni jambo jema, lakini kwa nini umfuate saa nane za usiku? Mdai mchana, kama ni jambazi, ni gaidi huyo ameondoa haki yake ya kuwa na faragha, huyo mshughulikie kwa sheria zote zilizopo. Lakini huyu ni raia mwema, unamdai kodi, mdai kwa utaratibu ambao umewekwa na sheria usikiuke sheria mama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ziko sheria nyingi ambazo ama hazitungwi vizuri au hazitungwi kabisa au hazisimamiwi, kuna mfano ambao kwenye taarifa haumo, siku hizi kwenye mitaa kwenye makazi ya watu unakuta kelele nyingi sana baa zinapiga miziki, spika kubwa hivi, anafungulia mpaka mwisho. Makanisa na misikiti yanapiga kelele kubwa sana kwenye mitaa ya watu, watu hawawezi kulala usiku wala kupumzika mchana NEMC ipo, BASATA ipo, Halmashauri zipo hazichukui hatua yoyote. Huu ni utekelezaji mbaya wa sheria ndogo na hatuwezi kunyamaza, lazima tuseme mtufuatilie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Sylvia Sigula, Mheshimiwa Christopher Ole-Sendeka, Mheshimiwa Kasalali Mageni na wengine wamezungumzia pale mwishoni kwamba ni vizuri labda baadhi ya sheria hizi kabla ya kutumika, maana yake sheria ya sura ya kwanza inaruhusu sheria zitumike kabla ya kuja Bungeni, Halmashauri, za Wizara huko zitumike kabla ya kuja Bungeni angalau basi za Halmashauri zije kwanza Bungeni kabla ya kutumika kule kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri hii iwe hoja ya Bunge na mimi naomba hii tuipitishe kama hoja ya Bunge, hoja ya Kamati kwamba sheria hizi ziletwe, zipitie kwanza kwenye Kamati yetu, zipitie Bungeni, halafu ndio zitumike kule kwenye kusimamia wananchi. (Makofi)

Kwa hiyo, naomba hiyo iongezwe hii sura ya kwanza iletwe Bungeni ifanyiwe marekebisho kusudi sheria hizi zije kwanza Bungeni kabla ya kwenda kusimamia maslahi ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. KILUMBE S. NG'ENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.