Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

MHE. NOAH L. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Taarifa ya Kamati zote mbili ya Katiba na Sheria na Sheria Ndogo.

Mheshimiwa Mwneyekiti, kama tujuavyo Bunge lako limepewa mamlaka chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 64 na Ibara ya 97 yenyewe ndiyo imepewa mamlaka katika kuhakiisha kwamba sheria inatungwa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwamba hakuna chombo kingine chochote chenye mamlaka labda Bunge ikasimu madaraka haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi hiyo imekuwa ikifanyika vyema na Bunge lako na Kamati pia tumeendelea kufanya kazi nzuri ya kuchambua miswada mbalimbali ambayo imekuwa ikiletwa na Serikali kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunakwenda kupata sheria nzuri, Sheria ambayo inakuwa ni ya matumaini, sheria ambayo inaweza kujenga uchumi na mambo ambayo yanaleta matumaini kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile pia katika jambo lolote tulipokuwa kwenye mjadala mbalimbali kuna sheria ambazo zimepitwa na wakati, ambayo sasa kama tunataka kujenga uchumi lazima tutizame sheria zetu, kama tunataka kuhakikisha wananchi wetu wanapata nafuu ya maisha kwa maeneo mbalimbali lazima tuangalie sheria zetu, kwa mfano kama tunataka kuhakikisha kwamba mali za Serikali zipo salama lazima tuendelee tena kuangalia sheria hii ya manunuzi (Public Procurement Act) sasa inatakiwa irekebishwe kwa sababu imekuwa kama ndiyo yenye kutoa mwanya wa wale wahalifu wa wizi na masuala ambayo hayafai katika ubadhirifu wa mali za umma. Sheria hii inatoa mwanya mkubwa sana, lakini sheria hii imeendelea kuchelewesha miradi mbalimbali ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; ni kwa nini hatutaki kuirekebisha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kutokutaka kurekebisha simaanishi kwamba katika utaratibu wa kutunga sheria tunajua kwamba lazima Serikali ilete muswada kwenye Kamati na baadae tuje kwenye Bunge, sasa hii ni changamoto kubwa kwa sababu Serikali lazima ione kwamba hiyo sheria imekuwa na mapungufu makubwa; kwa nini hatutaki kurekebisha au tunataka kuendelea kuwalea hawa wezi, hawa wanaoweka mwanya wa ujambazi, hawa ambao wanataka kutafuna fedha ambazo zinatafutwa na Mheshimiwa Rais usiku na mchana? Hii siyo sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sheria hizo zinatakiwa zirekebishwe, lakini pia hata Sheria ya TAKUKURU bado na yenyewe ina madhaifu makubwa, watu wenye kesi za kuku sijui na kesi ndogo ndogo za kupigana ndiyo wanaoshughulikiwa zaidi kuliko wale ma-giants wanaofanya ufisadi. (Makofi)

Kwa hiyo, lazima sheria hizi ziangaliwe kama kweli tuko seriously katika kuhakikisha kwamba nchi yetu inataka kusonga mbele kiuchumi, kijamii na kisiasa. Mheshimiwa Rais, amekuwa akijitahidi sana ku-harmonize mambo mengi sasa na sisi wasaidizi wake tujitahidi kuhakikisha kwamba tunakwenda kwa spirit hiyo hiyo ya Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria pia ambayo inatakiwa irekebishwe sheria iliyoanzisha TEMESA. Hii nayo ni kidonda ndugu kwenye halmashauri zetu, sheria ile inasema gari ikatengenezwe TEMESA, lakini halmashauri inalazimishwa wakishapeleka gari pale wao TEMESA wanapeleka kwenye garage za uchochoroni. Sasa gharama inakuwa kubwa kuliko hata halmashauri ingetengeneza, hii nayo ni changamoto kubwa ambayo lazima Serikali ifike mahali iweze kuangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna suala la utunzi wa sheria kwa lugha ya Kiswahili. Tumepitisha sheria hapa tukasema ile sheria imeeleza bayana kwamba katika mjadala lazima katika maamuzi yetu au utungaji wa sheria lazima sheria iwe kuna Kiswahili na Kiingereza ili iweze kusaidia wananchi wetu waweze kupata haki zao na waweze kuelewa hasa tukizingatia kwamba Tanzania sisi siyo kisiwa, sisi ni miongoni mwa nchi za Commonwealth ambayo tunatumia precedent za Jumuiya ya Madola na kama unavyojua kuna maneno mengine kwenye sheria ambayo hata Kiingereza haina, maneno kama mandamus, certiorari, obiter dictum na mambo kama hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni ngumu sana kwa hiyo tunataka tuombe Serikali ifike mahali ituletee na tumeshauri kama Kamati, tunapoletewa miswada uje muswada wa Kiingereza na Kiswahili kwa sababu kama jinsi ambavyo ilikuwa intention ya Bunge wakati wa kutunga ile sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimeona nisiache suala la Marekebisho ya Sheria ya Ndoa, nataka niiulize Serikali; nini chanzo cha kurekebisha sheria hiyo? Kwa nini tunataka kwenda kuangalia sheria nzima ya ndoa kama ndiyo ni mbaya zaidi? Mahakama imetoa hukumu mwaka 2016 kwamba vifungu namba 13 na 17 vya Sheria ya Ndoa inakiuka Katiba, sasa kama Mahakama imetoa Serikali ikakata rufaa mwaka 2019, Mahakama ya Rufaa Tanzania ikakataa; sasa Serikali imeenda tena zaidi inataka tena kuchukua maoni kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wadau wamefungua kesi ya kutokukubali maoni hayo yachukuliwe; sasa je, Serikali haioni katika kukataa kutekeleza uamuzi wa Mahakama yenyewe inakosa uhalali wa kuweza kuendelea kusimamia sheria? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini Serikali inataka kuangalia sheria nzima ya ndoa kama ni mbaya badala ya kuangalia vifungu viwili ambayo Mahakama imesema? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka kusababisha mgogoro pasipo na sababu, hii siyo sawa, lazima muangalie vifungu viwili tu ambayo Mahakama ndiyo imesema. (MakofI)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja. (Makofi)