Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Kwanza nimpongeze Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria kwa hotuba yake nzuri sana, ametuwakilisha vizuri Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ni siku ya Katiba na Sheria ndogo; ni Sheria tu leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya vitu ambavyo nachangia leo, naanza na suala la ajira na kazi kwa sababu liko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, lakini ni jambo ambalo limekuwa na Changamoto nyingi sana. Vijana wetu wengi wako hapa wanahangaika wakitafuta ajira. Kila Mbunge hapa kila wakati analetewa majina, CV za vijana wengi wakitafuta kazi. Wakati interview zinafanyika, aidha nafasi ni 30 wanaletwa watu hapa 4000, 5000; si, sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi tumeona wameanza kubadilisha kidogo, sasa wameanza kugawa kwa zone, ili kuwaondolea vijana usumbufu kuhangaika k wenda sehemu moja wako 3000, 4000 halafu nafasi ni 50 tu. Kwa hiyo, ndilo jambo moja tu ambalo nilitaka nishauri Serikali mbadilishe na mje model ambayo itawasaidia kuwaondolea usumbufu vijana hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila Mbunge hapa, ukisikia ajira zimetoka 10,000 hesabu za haraka haraka ni kwamba unachukua idadi ya majimbo unagawa ili walau kila Mbunge kwake kule aone vijana wake kadhaa wamepata ajira. Hilo ndilo tegemeo la kila Mbunge hapa na tunataka hivyo. Hatutaki tusikie ajira ziko 10,000 lakini ajira zinavyoenda unashangaa humuoni mtoto wa Kiteto ama kutoka jimbo lolote la Mbunge hapa; mnatugombanisha na wananchi. Kwa hiyo, tengenezeni model nzuri sana itakayotusaidia. Kama mnavyogawa poesa za miradi, kwa mfano kama ilivyokuwa UVIKO; mbona imewezekana na miradi imekwenda kila mahala. Tunataka kwenye ajira pia Mlete Model ambayo itatusaidia wote tuone kwamba tumejumuishwa na suala la ajira na Kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala jingine muanzishe, anzisheni mijadala; mnajua hatusemi hili ni la kwenu peke yenu, tuanzishe nijadala ya mara kwa mara ya namna ya kuboresha suala la ajira nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine ni ofisi au idara inayoitwa ya Mpigachapa wa Serikali (Government printer); sijui wabunge wangapi wanafahamu hii Government printer; hata sisi Kamati yetu kwa mara ya kwanza tumefahamu jana zaidi baada ya kuja kutuonesha na tukaona; lakini kazi kubwa inayofanywa na idara hii ni kubwa zaidi. Inasimamia Nembo na Bendera ya Taifa inasimamia kuchapisha nyaraka za Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Mahakama na Bunge. Hata bendera tulizonazo; na mwaka jana hapa tulirumbanarumbana kidogo kujua ipi bendera sahihi ya Bunge; na siku hizi vipeperushi vingi sana vipo mtaani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ofisi hii haijawezeshwa ipasavyo Serikali imekuja na mkakati mzuri sana wa kuboresha ofisi hii ama idara ya Mpiga Chapa wa Serikali; ni Ofisi muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana kwa mfano walikuwa wanatuambia kwamba, kama wangeweza kupata pesa wangeweza kuchapisha nakala milioni sita ambayo ingeweza kupatia Serikali bilioni 20. Lakini kwa sababu ya ufinyu wa bajeti sasa hivi wanapata nakala laki sita peke yake. Kwa hiyo ni muhimu wabunge wafahamu kwamba ofisi hii muhimu sana ya Serikali inayohifadhi nyaraka na alama za Taifa letu ni muhimu iwezeshwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) vilevile haipati pesa za kutosha ili iweze kufanya kazi yake kwa ufanisi. Mimi nilipata nafasi ya kumtembelea DPP siku moja, nilishangaa sana, ofisi yake ni ya ajabu sana. Najua sasa hivi wanajenga ofisi yao; lakini ni vyema Serikali ikatenga pesa ili watu hawa wanaofanya kazi kubwa wapate kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni Law School of Tanzania. Law school of Tanzania; na mimi ni mwanafunzi wa Law School of Tanzania, first cohort. Ukisikia mambo yanayoendelea huko wakati mwingine unasoma vijana wale wanenda kufungua kesi; mahakamani ni dhahiri kwamba kuna jambo la kufanywa na Serikali. Kwa mfano ripoti ya Dkt. Mwakyembe muilete bungeni tuangalie, tu-interrogate ili na sisi tuweze kushauri namna bora; na Mheshimiwa wakili msomi, Mavunde tulikuwa cohort moja first cohort; lazima, hata wewe unajua unamawazo mazuri ya namna ya kuboresha hiyo zaidi ili vijana wetu wasisumbuliwe lakini tuwatengeneze Wanasheria wazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na Kamati imesema hapa labda kuna haja ya kuanzisha ile entry exam. Lakini sheria ile iliyounda law school ni kama ilimlazimisha kila mtu kwenda Law School of Tanzania, ambayo si sawa. Waende wale ambao wanataka kuwa mawakili. Kwa hiyo kama kuna haja ya kufanya hivyo basi ni vizuri tuangalie mifumo ile. Na pengine baadhi ya courses, kwa mfano Mheshimiwa Mavunde wakati tunasoma accounting for lawyers; sawa ni important lakini kwa nini, but why do you examine me on accounting for lawyers inanisaidia nini? Halafu baadaye inanishushia tu grade zangu hainisaidii chochote. Kuna course nyingine ni muhimu lakini ukini-examine accounting for lawyers kweli? Na mengine mengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu lugha ya uandishi wa sheria; Bunge hili lilipitisha sheria hapa ya kusema tutumie Kiswahili, jambo ambalo ni jema sana; Watanzania wengi lazima wafuatilie, waweze kusoma sheria tunazotunga na waweze kuelewa kwa lugha hiyo. Hta hivyo kwa sababu Tanzania si kisiwa peke yake, ni vyema kama walivyoshauri Kamati, tupate sheria hizi zote kwa lugha ya Kiingereza na Kiswahili, Kwa sababu si kwamba sheria zetu tunazotunga zina Mahakamani peke yake bali pia zinatumika kufundisha wanafunzi; na wanafunzi wanatoka kila mahali duniani kuja kwenye Mahakama zetu na kwenye vyuo vyetu. Kwa hiyo ni muhimu sana ili tuondokane na mambo kama hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho nitazungumzia habari za Mahakama. Hii program mliyoanzisha Mahakama ya-integrated justice, ile Mahakama Jumuisho, ni program nzuri sana. Siku hizi mahakama zetu unatembelea mahakama utafikiri ni hoteli kabisa. Hata ukitembelea judiciary square hapa naambiwa ni jingo sijui la sita ama la kumi Southern of Sahara, ni nzuri sana, program ile ni nzuri sana. Lakini sasa tunataka haki zitoke kwenye majengo yale. Sisi hatutaki kwa sababu ni jengo refu tu, no, challenge sasa ni kwamba we want justice kutoka kwenye Mahakama hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imezungumzwa hapa na sheria ndogo; wakati mwingine Bunge linashauri kuhusu jinsi tunavyotafsiri sheria zetu. Hakuna kitu kibaya sana kama Serikali msipofahamu bunge lilimaanisha nini kwenye sheria hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko suala la mifugo, ina-touch hii Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali; na vifungu vinavyotumika kila wakati ni Kifungu cha 116 cha Sheria ya Wanyamapori kwenye ku-compound offenses. Kama juna eneo ambalo tunafanya hovyo kuliko yote ni kwenye compounding of offenses. Sheria, na Bunge lilisema hivi, Section 116, na ninaomba kunukuu; “This section shall apply to offenses committed under the Act in relation to protected areas, the director may compound an offense by requiring a person to pay a sum of money provided that such money shall not be less than two hundred thousand shillings and not exceeding ten million shillings”

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo ndivyo Bunge lilivyosema; a person. Lakini wanakaa waswahili fulani tu kule wanaanza kuhesabu vichwa vya mifugo halafu wanasema lipa laki moja moja; that is not the intention of the law. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge hili likinyamazia vitu kama hivi; na si Bunge kabisa, ni mtu mmoja bingwa tu, alivyosema Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria Ndogo hapa. Haya makosa yaliyogundulika takriban kanuni 31 zenye kasoro za kiuandishi zinakwenda kinyume na Katiba. Haya ni makosa tu yamegundulika kwa kusoma zile sheria, lakini wangekwenda field leo wakajua ni watu wangapi wameumia kwa sababu ya sheria hizo ni mbaya zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Sheria ya TANAPA Section 20A bado inazungumzia kwamba fine kama unataka ku-compound should not exceed one hundred thousand, should not exceed; lakini a person pays. Sasa, wakati Bunge linatunga sheria definition of livestock maana yake ni mbuzi kondoo nguruwe farasi kuku ndama hata mayai. Sasa laki moja leo ng’ombe ni wa laki moja na nusu ama laki moja halafu unataka kutoza fine ya shilingi laki moja utafanya Bunge hili lisiaminike hata kidogo. Lakini kumbe wala sio sisi, ni wale wanaosimamia sheria. Kwa hiyo Waheshimiwa Mawaziri muwe wakali sana. Bunge hili likisema na likishauri kanuni hii haifai ama hii compounded haifai ni vyema mkasimamia kwa nguvu zote ili Bunge liendelee kuheshimika…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante sana kengere ilishalia muda mrefu.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na ninaunga mko hoja.