Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kupongeza Kamati hizi tatu kwa kazi kubwa sana na nzuri ambayo wamefanya. Kusema ukweli wamefanya Bunge hili leo lichangamke kwa sababu ya kazi kubwa ambayo imefanywa na Kamati hizi tatu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, LAAC wamekuja na Maazimio sita, PIC imekuja na maazimio 11, na PAC imekuja na maazimio saba. Serikali tumeyachukua maazimio yote positively na kusema kweli ni kazi ya Serikali kwenda kuyafanyia kazi. Napenda nikuhakikishie kwamba tumeyasikia, na pia tumesikia michango ya Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi hii iliyofanyika leo inatokana na ripoti ya CAG ya mwaka 2019/2020. Huu udhaifu mliousema hapa, ni ya 2019/2020. Sasa taarifa ambayo sisi tunaamini imeandaliwa na CAG na ikapokelewa na Mheshimiwa Rais, na ikaletwa humu Bungeni, na mmeifanyia Kazi mkaitendea haki, tunawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais wakati anapokea taarifa hii, alisema maneno yafuatayo: “Kumekuwepo na mifumo mingi Serikalini, mifumo ambayo haisomani, na kila mmoja ukitengeneza mfumo unauruhusu uchotaji wa fedha.” Pia akaendelea kusema, “kuna usimamizi usiokuwa na weledi Serikalini unaosababisha wizi.” Mwisho wa kunukuu. Akaagiza CAG, PCCB na DPP wachukue hatua bila kuogopa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba, kwa taarifa hii na michango hii na mapendekezo ya Maazimio haya ya Kamati, Mheshimiwa Rais naamini atayapokea kwa mikono miwili na atahakikisha kwamba haya yote yanaenda kusimamiwa na kutekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama hapa kwa niaba ya Serikali kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge, na hasa Bunge hili ambalo kimsingi ni Bunge la CCM. Kama Bunge la CCM linaikosoa Serikali yake katika chombo muhimu, maana yake Bunge hili linaaminika na wananchi. Kwa hiyo, michango yenu Waheshimiwa Wabunge na maazimio haya, ni kazi ya Serikali kufanyia kazi. Tumeyapokea na naomba kuwahakikishia kwamba tunakwenda kuyafanyia kazi na tutarudisha hapa taarifa wakati kama huu mwaka unaokuja na mtaona mabadiliko makubwa sana Serikalini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yako mambo hapa yamezungumzwa ni aibu. Accounting Officer huyo huyo anachelewa kulipa, mradi unakuwa penalized, halafu yeye mwenyewe anasaini malipo ya kumlipa tena Mkandarasi huyo huyo. Haiwezi kuwa sawa sawa. Ni lazima tuseme, na tuje tueleze ndani ya Bunge hili, nani alichelewesha? Nani amechukuliwa hatua? Hatua zionekane kweli zikichukuliwa, siyo zisemwe tu zimechukuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima tuweke mfumo wa sasa ambao utaruhusu kwamba yule anayekosea Serikalini anaadhibiwa; na yule anayefanya vizuri, anapongezwa na kusifiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika na Waheshimiwa Wabunge, nataka niwahakikishie tumewasikia, nami na wenzangu tunaunga mkono hoja hizi za Kamati na Serikali iko tayari kuzifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)