Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nichangie kidogo kwenye hoja ambayo ipo mezani.

Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya PIC, Kamati ambayo ni mtambuka, kwa hiyo moja kwa moja niseme kwamba naunga mkono hoja zote tatu za PIC, PAC na LAAC. Pia, nichukue nafasi hii kupongeza sana Wenyeviti wetu kwa jinsi ambavyo wamewasilisha taarifa hizi; na kwa sababu ya ufinyu wa muda na mimi nitazungumza kwa kifupi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu TANAPA; kuna mwenzetu ameshalizungumzia lakini nongezee. Mwaka 2020 tulipitisha sheria hapa, Sheria ya Fedha Namba Nane ambayo ilipelekea makusanyo yote yanayokusanywa na mashirika haya ya uhifadhi kukusanywa na mamlaka ya mapato. Pamoja na nia njema ya Serikali kuhakikisha kwamba haya mashirika hayaathiriki na athari za UVIKO – 19 ambayo ilisababisha kukawa na upungufu wa watalii nchini lakini hatua ile imefanya mashirika haya ambayo yanafanya kazi kwenye mazingira magumu ya porini kushindwa kutekeleza majukumu yake sawa sawa, hasa kwenye miundombinu ambayo kwa sababu ya hali ya mazingira huwa inaharibika haribika hasa kwenye barabara na sehemu nyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunashauri kwamba ili kutatua tatizo hilo Serikali iangalie namna ya kuwaruhusu wa-retain, kuwe na retention yale makusanyo wabaki nayo moja kwa moja bila ya kungojea kwenda kuomba fedha Serikalini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Bandari ya Dar es Salaam iliyopo chini ya Mamlaka ya Bandari ndilo lango kuu la uchumi wa landlock countries za DRC, Rwanda, Burundi, Uganda, Malawi, Zambia, Zimbabwe na Sudan ya Kusuni. Wingi wa shehena ambazo zinapitia pale bandarani zinafanya bandari hii inaelemewa. Sasa hivi Bandari ya Dar es Salaam inafanya upanuzi lakini bado upanuzi ule hautakidhi uzito wa kuelemewa na shehena ambazo zinapitia pale. Kuna mradi wa ujenzi wa Bandari Kavu Kwala ambao sahivi umefikia percent 98 kumalizika.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashauri Serikali iharakishe na ihakikishe kwamba mradi ule unamalizika haraka kwa sababu bandari ile itakapoanza kufanya kazi itapunguza mzigo wa shehena pale bandarini kwa percent 30; lakini pia kuna mpango wa kujenga Bandari mpya ya Mbegani Bagamoyo ambayo sana sana itatumika kwa ajili ya kushushia makontena. Bandari ile nayo ni muhimu sana, hivyo mradi ule utekelezwe haraka ili kunusuru Bandari ya Dar es Salaam na kuifanya itekeleze majukumu yake kwa tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ya ufinyu wa muda, hayo ndiyo niliyokuwa nataka kusema. Niseme naunga mkono hoja na nakushukuru sana. (Makofi)