Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipatia nafasi ili niweze kuungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu kuchangia hizi hoja mbili zilizoko mbele yetu, hoja ya Kamati ya Miundombinu pamoja na hoja ya Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji.

Mheshimiwa Spika, naomba nianze na suala zima la mtiririko wa bajeti kwenye Wizara ya Kilimo na nitaomba nijikite sana kwenye kilimo kwa sababu kilimo zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania wanategemea kilimo, kiuchumi na kwenye mambo mengine yote.

Mheshimiwa Spika, mwaka jana mwezi wa Sita tunaahirisha Bunge hapa, bajeti ambayo ilikuwa ni kipaumbele na tuliyoipigia makofi na kuishangilia ilikuwa ni bajeti ya Kilimo ambayo ilitoka bilioni 200 mpaka tukafika bilioni 900. Tulisema hapa kwamba suala la kutenga hii bajeti liendane na suala zima la kupeleka fedha kwenye Wizara husika ili tuweze kufikia malengo tunayoyakusudia.

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa tuna nusu mwaka, Serikali kwa maana ya Wizara ya Fedha wametoa asilimia 19 tu ya bajeti ya maendeleo. Tunavyozungumza hapa, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa dhamira yake njema ya kuwasaidia wakulima na kuinua kipato cha Taifa letu, akaamua kwa kuwa suala la mbolea limekuwa ni changamoto gharama ni kubwa, akaomba Wizara itoe shilingi bilioni 150 ili ziende kwenye mbolea watu wetu waweze kupata mbolea kwa bei ya chini.

Mheshimiwa Spika, leo tunavyozungumza Wizara ya Fedha imetoa bilioni 50, lakini bilioni 50 zenyewe zimetolewa kwa kunatanata hizi, kuanzia mwezi wa Novemba, Disemba na hii Januari ndiyo wanaendelea wamefikisha bilioni 50. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wenzangu wamesema…

SPIKA: Mheshimiwa Kunti, Mheshimiwa Waziri wa Fedha amesimama. Mheshimiwa Mwigulu ni taarifa, utaratibu ama?

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika ni taarifa.

SPIKA: Inabidi ukisimama uniambie ili nijue ni Kanuni gani inaniongoza, karibu.

T A A R I F A

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ninampa taarifa mchangiaji Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi tunavyoongea hatuna shida ya fedha kwa ajili ya Wizara ya Kilimo, fedha kwa ajili ya Wizara ya Kilimo, kwa ajili ya irrigation, kwa ajili ya mbolea zote zipo hivi tunavyoongea, isipokuwa tunazitoa kufuatana na jinsi certificate zinavyoiva. Mikataba yote ya program imeshasainiwa, kwa hiyo, kadri certificate inavyokuja tunawasilisha na Waziri wa kisekta atasimama hapa akuambie kwamba wanasubiri certificate halafu tulipe, na mikataba yote ilishasainiwa.

Mheshimiwa Spika, inabidi tukubaliane ili tuelewane, fedha hatufanyi kazi ya kugawana tunatekeleza project ndiyo utaratibu wa malipo unavyofanyika. Kwa hiyo, fedha kwa ajili ya irrigation zipo na zinasubiri certificate ili tuweze kulipa, zote zipo hata hela za mbolea zipo.

SPIKA: Haya ahsante sana, Mheshimiwa Kunti unaipokea taarifa hiyo?

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, naomba nisiipokee na ninaomba niendelee na mchango wangu.

Mheshimiwa Spika, nimesema hivi, Mheshimiwa Mwigulu unao muda wako pia wa kuja kujieleza haya yote unayotamani kuyaeleza. Fedha bilioni 150 zipo, tunatakiwa tutoe fedha ziende kwa waagizaji wa mbolea ili watu wale waweze kutoa mbolea. Hapa sasa hivi ninavyozungumza magari yapo bandarini yanapakia mbolea, Wahindi wamegoma kutoa magari ya mbolea, vijijini huko hakuna mbolea, msimu wa kupanda Watanzania wamepanda bila mbolea, wamepanda zimeota na mbolea ya kukuzia ni tafrani! Tunakwenda kwenye uzalishaji mbolea ya kuzalisha haipo nchini, sasa yeye ananiambia mbolea ipo unaona raha kuweka hela benki zipo pale zimetulia halafu Watanzania tunapata shida? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hizo fedha kama zipo za mbolea bilioni 100 iliyobaki tunaomba kesho ilipwe ili Watanzania waweze kupata mbolea na tuachane na hizi story zenu mnazotuletea.

Mheshimiwa Spika, naomba niendelee na suala la kilimo lakini suala la mbolea zilipwe. Wizara ya Kilimo imesaini mikataba 64 kwenye umwagiliaji, sijui ujenzi wa mabwawa na kadhalika kwenye miradi yao yote. Umesaini mikataba halafu wamekuambia tupe fedha hutoi fedha unatuambia fedha zipo unaziweka hizo fedha zikusaidie nini au zikufanyie nini wewe? Watu wapo tayari kwa ajili ya Kwenda site, mikataba imesainiwa, toeni fedha ili mikataba Wakandarasi waende site wakaanze kufanyakazi za ujenzi.

Mheshimiwa Spika, tunakuwa tunatarajia kwenye suala la umwagiliaji Taasisi yetu ya ASA inayokwenda kuzalisha mbegu, Wakandarasi hawa walipwe fedha zao ili ASA mwakani tuweze kupata mbegu ya kutosheleza yenye gharama nafuu. Leo tunavyoongea mbegu ya mahindi kilo mbili inauzwa shilingi 14,000 mpaka shilingi 20,000, ukija kwenye mbegu bora ya alizeti inauzwa shilingi 70,000 mpaka shilingi 90,000! Sasa huyu mkulima ni wa namna gani anaenda kupata hizo mbegu kwa namna hiyo?

Mheshimiwa Spika, tulitarajia fedha za umwagiliaji zingetolewa ASA wakapata hizo fedha, mashamba yao yakawekewa mfumo wa umwagiliaji, wakalima mbegu na Watanzania wakapata mbegu kwa gharama nafuu na zinazopatikana kwa wakati, kwa hiyo biashara ya kuambiwa fedha zipo, shida sijui hatugawani hela kama njugu, hiyo miradi mingine mnayogawana kama njugu mbona hatusemi na mnazitoa tu kama njugu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala pia la usimamizi, Mheshimiwa Rais aligawa pikipiki baada ya kufanya uzinduzi, baada ya kugawa zile pikipiki zimeenda site, pikipiki zile zinasimamiwa na watu wa TAMISEMI, hivi tunavyoongea haziendi site kwa sababu hawana mafuta, sijui kwako Spika Jimbo la Mbeya kama wanakwenda, tukija kwenye suala la bajeti tukisema jamani tunaomba hawa watu wasimamiwe na Wizara husika mnasema ooh! Sijui nini, sijui vitu gani! Mnatuvuruga na mnatuchanganya. Leo, sera ya kilimo inasimamiwa na Waziri wa Kilimo, tukienda kwenye utekelezaji anaekwenda kusimamia utekelezaji ni TAMISEMI! Huyu mtu ameharibu huku Waziri wa Kilimo hana uwezo wa kumwajibisha huyu Afisa anaesimamiwa na TAMISEMI huku chini, ni mpaka procedure tena Waziri wa TAMISEMI aingilie hapo ndiyo aende awajibike.

Mheshimiwa Spika, leo mafuta ya pikipiki, pikipiki zipo kule chini, Mkurugenzi anafanya shughuli zake kwa pikipiki zile zile ambazo zilitakiwa kwenda kufanyakazi ya kilimo, kwa hiyo kilimo kimebaki pale, Afisa Kilimo yupo pale, pikipiki haina mafuta, anatumwa na Mkurugenzi ambaye anapelekewa mafuta nenda kanifanyie kazi yangu fulani, tunaenda wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninaomba Serikali ipitie upya mfumo wake wa kiutawala kuhusiana na suala zima kwenye Wizara hususani Wizara za kisekta za uzalishaji, kwamba wate hawa wa chini ni lazima watoke TAMISEMI nak ama hawatoki TAMISEMI basi tuone ni namna gani tuweke Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI atakaeshughulika na Wizara za uzalishaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nizungumzie pia suala la mifugo. Tumekuwa tukisafiri, tunatoka Mwanza mpaka Dar es salam, tumekuwa tukiona malori yameongozana yakiwa yamepakia ng’ombe hai anatolewa Mwanza ama Shinyanga anapelekwa Dar es salam kwenda kuchinjwa.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na ajali nyingi zinazotokana na malori haya; madereva wamechoka ng’ombe wale wanapata ajali kule wanakufa na wengine wanakatika. Hatima yake hata hizo nyama tunazokula hazina afya kwa matumizi ya binadamu. Ng’ombe umemkeshesha siku tatu, wiki yuko barabarani, akifika apumzishwi anapitilizwa anaenda kuchinjwa; nyama ile inakuwa haina ubora kwa lishe ya binadamu.

Mheshimiwa Spika, na umeeleza hapa kwamba Kamati ya Kilimo tumewaambia kwamba kuna udumavu wa samaki, je, sisi tunaokula inakuwaje? Je, tujiandae nasi kuwa wadumavu wa afya, kwasababu tunachokula tunajaza tumbo na hatuli chakula bora. Kwahiyo tuna lishe duni na naamini ndiyo maana hata tunaona hapa watu sijui ni kwasababu ya samaki wadumavu ndiyo maana tunaambiwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)