Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

Hon. Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia machache katika Kamati yetu ya Miundombinu.

Mheshimiwa Spika, mimi nitajikita katika sekta ya ujenzi; kwa kweli wenzetu wa TANROADS wanafanya kazi kubwa na ni watu ambao huwa ni wa kupigiwa mfano, sote Wabunge tunaitegemea TANROADS. Sasa hivi Barabara nyingi ziko katika hali nzuri na ambazo bado hazijatengenezwa lakini tayari ule uelekeo upo. Kwa kweli tuwapongeze sana wenzetu wa TANROADS kwa jinsi ambavyo wanafanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile niiombe Serikali kuwaongezea bajeti wenzetu hawa wa TANROADS. Bila ya kuwa na bajeti kubwa hawatoweza kumaliza kazi ambazo tumezitegemea, lakini vilevile TANROADS wana ukosefu wa wafanyakazi. Niiombe Serikali iwaongezee wafanyakazi ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi mzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende moja kwa moja katika TBA; kwa kweli ni wa kupigiwa mfano. Tumewatembelea na tumeona kazi zao ambazo wanazifanya ni kazi nzuri sana, lakini wana changamoto ya kudai fedha nyingi katika Serikali. Niiombe Serikali kusimama wima ili waweze kurejeshewa fedha hizi na waendelee kufanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nije moja kwa moja katika TEMESA, vilevile wana ukosefu wa wafanyakazi, niiombe Serikali kuwapatia wafanyakazi ili waweze kuimarisha kazi zao vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalizie mchango wangu mdogo kwa upande wa High Court. Kuna changamoto kubwa ya bajeti yao ambayo haikidhi haja, niiombe Serikali kwamba waongezewe bajeti ili na wao waweze kufanya kazi vizuri, lakini pia wana changamoto ya wafanyakazi. Wafanyakazi ni kidogo mno naomba sana waongezewe wafanyakazi.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa nimalizie kwa kukupongeza wewe kwa kuonesha juhudi zako nzuri kutuletea Bonanza la Wabunge kuona kwamba Wabunge wote miili yao iweze kuimarika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naunga mkono kwa asilimia 100. (Makofi)