Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Nimesimama hapa kwanza kabisa kuwapa moyo Wanajeshi wote wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, licha ya kuwapa moyo, naomba nichukue nafasi hii kuwathibitishia Wanajeshi wetu wote wa jeshi letu, Serikali iliyopo madarakani ya Chama cha Mapinduzi itaendelea kuwajali na kuwaheshimu siku zote.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kusema, tunaendelea kuthamini kazi na michango yao mizuri katika kulinda amani ya nchi yetu ya Tanzania bila kujali chama chochote cha siasa katika nchi yetu ya Tanzania.
Sisi kama Serikali tutaendelea kufanya nao kazi, wasisikilize propaganda ya mtu yeyote. Sisi kama Serikali tunaendelea kufanya nao kazi na tunatambua mchango wao muhimu katika Serikali yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati leo tukizungumza kwenye Bunge hili na tunajua kwamba 61% ya nguvu kazi ya nchi yetu ya Tanzania ni vijana kati ya umri wa miaka 15 na 35 na Jeshi hili la Wananchi wa Tanzania kupitia JKT wamekubali kushirikiana na Serikali na kuamua kuwachukua vijana wa Tanzania kutoka Jimbo la Iringa na majimbo mengine yote katika nchi hii ya Tanzania na wamekwenda kufanya mafunzo ya JKT. Pamoja na mafunzo hayo ya JKT, Serikali imeona umuhimu wa wale vijana wanaokwenda pale kwa kujitolea na imeona wanatakiwa wafanyiwe maandalizi ya kutosha ili tutatue tatizo la ajira nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, yamezungumzwa maneno hapa, Serikali haina mpango na hao vijana. Leo nataka kuliambia Bunge hili tayari Serikali imeingia mkataba na Jeshi la Kujenga Taifa, tayari Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Tanzania limeanza kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana wote wanaochukuliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwenye JKT kwa kujitolea ili wanapomaliza mafunzo yale waweze kuunganishwa na vyombo mbalimbali vya mikopo na kujiajiri kutokana na skills wanazozipata wakiwa jeshini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo jeshi hili ambalo linaenda kutatua matatizo ya ajira kwa wapiga kura wetu, ilitupasa humu ndani leo tulipongeze na kulipa heshima kubwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania na si vinginevyo. Ndiyo maana imenipasa hapa kusema nawashukuru na kuwapongeza Makamanda wote wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania pamoja na kulinda amani ya nchi ya Tanzania bado wamejitolea kuhakikisha malengo ya Jeshi la Kujenga Taifa kama hawafahamu hapa Wabunge ambao wanadharau uwepo wa Jeshi hili, ni haya yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, jeshi hili lina kazi ya
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
180
kutoa malezi bora kwa vijana, jeshi hili lina kazi ya kutoa mafunzo ya ujasiriamali na jeshi hili lina kazi ya kufundishwa kuwa jeshi la akiba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maneno haya na umuhimu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania tutasimama imara kulilinda na kulitetea daima. Tutasimama imara kuliheshimu na kuwapa heshima Wanajeshi wote wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Serikali tunasema tunawaomba waendelee kulinda amani ya nchi ya Tanzania kila siku. Waendelee kukuza maadili ya vijana wetu wa Tanzania kwa namna zote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumaliza mchango wangu kwa kumpongeza sana Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Sisi kama Wabunge tunamtia moyo aendelee kuliongoza jeshi letu sawasawa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kumpongeza sana Waziri mwenye dhamana ya kusimamia Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Nakushukuru Mheshimiwa Dkt. Mwinyi, endelea kutusaidia kulipa moyo Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.