Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Mheshimiwa Bulaya anapitia shirika letu la ATCL nimejaribu kupitia taarifa ya CAG ambayo imedondoshwa asubuhi hii, unajua tunajaribu kuwa current kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, CAG anasema mapitio yangu ya utendaji wa kifedha wa Mashirika ya Umma yalibaini kuwa masharika 10 niliyoyakagua mwaka huu, yakiwemo mashirika mawili ya kibiashara katika sekta ya umma, kampuni ya ndege na kampuni ya … yalikuwa na mtaji hasi kama inavyooneshwa kwenye Jedwali Namba 6.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaenda kwenye jedwali Na. 6 anasema, ni maoni yangu kuwa kuwa na madeni mengi kuliko mali kuna tia shaka iwapo mashirika hayo yanaweza kuendeleza huduma zao na kutimiza wajibu wao katika siku zijazo. Ukienda Jedwali la Sita mashirika ya umma yenye mtaji hasi katika mashirika yote kampuni yetu pendwa ya ndege iko Namba Moja, jumla ya mali Milioni 295, jumla ya madeni Milioni 535, mali hasi Bilioni 239.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni shirika ambalo kati ya maeneo ambayo naweza nikasema manne wakati wa Awamu ya Tano na ya Sita yaliyotengewa fedha nyingi sana kuliko maeneo mengine. Kwa tuliokuwepo kipindi hicho tulisema tumeanzisha shirika hili, tumenunua ndege wakati shirika halina mpango wa biashara!

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulisema tukapuuzwa lakini leo taarifa za Serikali zinaonyesha bayana kwamba wakati tunatoa Shilingi Trilioni 1.5 mwaka 2016 ndiyo wakati ule huo huo mpango wa muda mfupi wa biashara unatengenezwa. Matokeo yake ni nini? Mtaji hasi aliouzungumzia. Tunanunua ndege Serikali kama Mwanahisa Mkuu haweki capital halafu unategemea eti ndege ndiyo zijiendeshe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huo huo, unajiuliza kuna maneno nikiyatumia hapa sipendi kukera watu. Unamtumia wakala wa ndege eti mapacha wawili mnapangia dili ya biashara! Yaani wewe na mtoto wako, Serikali ATLC ni mali ya Serikali, wakala wa ndege ni mali ya Serikali, eti wakala wa ndege ana mkodisha ATLC ndege ambayo iko dhoofu bin hoi! Sasa matokeo yake ni nini? Matokeo yake ni kwamba huyu mtu ambaye hamjampa mtaji, huyu mtu ambaye ana madeni nimesema hapa zaidi ya Shilingi Bilioni 500 sasa hivi, anaongezewa madeni mengine eti na mtoto mwingine wa Serikali anaitwa wakala wa ndege, jamani hizi ni akili jamani! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaongea kwa sababu Mheshimiwa Rais alihutubia Bunge hapa na wengine tulisema tulipinga from the beginning siyo ufufuzi wa shirika ila namna lilivyofufuliwa. Mheshimiwa Rais akasema, tutafanya utaratibu Mheshimiwa Samia tufanye maboresho ya shirika letu tulipunguzie mzigo, sasa leo deni nimezungumza hapa Shilingi Bilioni zaidi ya 500.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia mpango wa biashara wa ATLC, ngoja niwatajie safari zake walikuwa na mpango wa kwenda Johannesburg, safari za kimkakati za biashara Nigeria, walikuwa wanataka kwenda London na maeneo mengine ya Bara la Ulaya, lakini sasa ukija huku ndugu zangu kwa mujibu wa hotuba ya Waziri Mkuu sasa Arusha, Geita, Mtwara, Songea, Bunjumbura, Entebe, Harare, Lusaka, halafu wameanzisha vituo vitatu vya kimagumashi hivi Lumbumbashi, Guangzhou, Mumbai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, why tuna-divert kwenye mpango wa biashara? tunaogopa kwenda mbele watakamata ndege zetu, with due respect ni kweli ni faida kuwa na ndege 16 hadi zinapaki pale airport good! Yaani we are so proud, very proud lakini unakuwaje na ndege ambazo hazikuletei tija? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanasema hapa hivi unafikiria kwa sababu eti mmempa wakala wa ndege ambaye anamuongezea mzigo ATLC ndiyo mkienda ‘mtoni’ hamkamatwi? Hizi ni mali za Tanzania. Tutibu tatizo tulipe madeni, Serikali ndiyo mwanahisa Mkuu wa Shirika, weka mtaji maisha yaendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna viwanja 15 vya ndege nchi hii, katika viwanja 15 viwanja Vinne ndiyo vinaweza kufanya kazi masaa 24 my friend!

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo tunapozungumza haya …

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Waziri wa Fedha.

T A A R I F A

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa mchangiaji kwamba utaratibu unaotumika wa Wakala, Serikali pamoja na Shirika hauhusiani na masuala ya madeni. Serikali ilishalipa madeni, ndege zetu hazina risk ya kukamatwa popote duniani, haya mambo yanayohusiana na madeni madeni yote yalishalipwa. Hakuna sehemu ndege ya Tanzania itaenda ikamatwe kwa ajili ya madeni na zitakuja na ndege za mizigo zitafanya safari zote za mizigo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kama kuna eneo lolote, ndege ya Tanzania haijaenda zitakuwa ni logistics tu za mambo ya kufungua anga kutokana na mambo ya COVID-19 yaliyokuwa yanatokea, lakini siyo kwa masuala ya madeni, madeni yote yalishalipwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna deni lolote ambalo linaiweka nchi yetu kwenye risk ya kukamatiwa mali yeyote ya Tanzania, na taarifa zingine hizo zitakuwa taarifa ambazo zinaendelea kukamilisha taratibu tu ambazo ni za masuala ya kianga na maeneo tofauti baada ya pandemic ya covid.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mdee unapokea taarifa.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina taarifa hapa ya shirika lenyewe kwa Kamati ya PAC inasema hivi ukurasa wa 10, naweza nikakupatia Mheshimiwa Waziri, inawezekana ulitoa hela zikaishia katikati. Inasema madeni ya ATCL na Serikali yanaathiri biashara na utendaji wa ATCL kwa kushindwa kutekeleza mipango ya kibiashara na kuhofia kukamatwa kwa ndege. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano safari zilizoanzishwa za Johannesburg zilisitishwa wakati mipango ya kuanzisha safari za kimkakati za kibiashara za Nigeria, London na maeneo mengine. Hii ni nyaraka inaonesha ukurasa wa Kumi nitakupatia hii nyaraka.

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

T A A R I F A

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtaarifu mchangiaji ya kwamba taarifa anayoisema ni ya hesabu za fedha za mwaka 2019/2020, na tayari Kamati ya PAC mimi nikiwa mjumbe wa Kamati ya PAC deni la awali lilishalipwa Shilingi Bilioni 120 ambazo ziliripotiwa katika mwaka wa fedha husika.

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Halima Mdee unaipokea hiyo taarifa?

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa niliyonayo mimi ni ya tarehe 31 Januari, 2022 juzi na imesainiwa na Afisa Mtendaji Mkuu Mhandisi Ladislaus Matindi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema haya unajua mimi nashindwa kuelewa tunapozungumza haya mambo hakuna anayemvizia mwenzie hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa natamani huo uchungu ambao wote tunao huo wa kupanda kwa mafuta na natarajia kipindi cha bajeti ya Nishati hapa ama kipindi cha Bajeti Kuu hapa, kama mzizi wa fitina wa mafuta, kama mzizi wa fitina wa vyakula kupanda bei, haujatafutiwa ufumbuzi pachimbike na ndiyo nitajua kweli sisi ni Wawakilishi wa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiroho safi Tanzania ni yetu, siyo kwa ubaya! kwa hiyo ninaposema wakati wa taarifa ya Waziri Mkuu inaonesha tuna miruko ya ndani, katika viwanja 15 vya ndani, vinavyoweza kuruka masaa 24 basi hata tutendee haki ndege zetu ni viwanja Vinne my friend! Nilidhani Waziri wa Fedha ataniambia, Halima wakati tunaanza kupata kwenda huko mbele tutahakikisha viwanja vyote 15 vya ndani vinafanya kazi masaa 24. (Makofi)