Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie nafasi hii kukushukuru wewe kwa kunipa nafasi, pili nitumie nafasi hii kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge na maoni waliyoyatoa kwenye hotuba wakati wanachangia hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu na niwape tu commitment kwamba maoni yao na ushauri wao Wizara tunachukua na kwenda kuufanyia kazi na mengi tutayajibu kwenye hotuba yetu ya bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninataka tu niongelee eneo la kwanza kuhusu suala la upandaji wa bei ya mafuta ya kula. Pamoja na kuwa kwamba kuna vitu viwili ambavyo vinasababisha moja ni production yetu ya ndani kuwa ndogo hasa kwenye maeneo ya mafuta kama ya alizeti, lakini kama Serikali tumechukua hatua ya kwanza mwaka huu tumesambaza mbegu zaidi ya tani 2,000 na tunaraji kwamba kwenye eneo la uzalishaji katika Mikoa mitatu ya pilot tunaweza kuongeza katika uzalishaji wetu wa ndani kwa sababu uzalishaji wetu wa ndani ni wastani wa tani 240,000 za mafuta ya kula, wakati mahitaji yetu ni wastani wa tani 600,000.

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wa Singida peke yake mbegu za alizeti zitakazozalishwa kutokana na mbegu tani 1,000 tulizopeleka katika Mkoa wa Singida tunataraji uzalishaji wa wastani wa mbegu mpya tani 300,000 ambazo zitatuingizia kwenye uzalishaji wa mafuta lita 100,000 ya mafuta.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge kwamba mwakani kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu mwaka huu tulisambaza standard seeds mwakani tutasambaza certified seeds tani 5,000 za alizeti ambayo itakuwa subsidized. Kwa hiyo, ninaamini kwamba kufika mwaka 2024/2025 tutakuwa tuna uhakika wa kujitosheleza mafuta ya kula ndani ya nchi na hasa kwa kutumia zao la alizeti.

Mheshimiwa Spika, zao la mchikichi tumeamua kwamba tu-encourage uzalishaji wa mashamba makubwa. Tayari tumeshapata wawekezaji wakubwa wawili. Mmoja atawekeza katika eneo la Rufiji na mwingine atawekeza katika Mkoa wa Kigoma na wameshaanza kufanya soil analysis na Wizara tunaendelea kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hatua ya pili kama Serikali tunatafakari na kuangaia tax framework ambayo inaweza kupunguza gharama ya mafuta. Mojawapo viwanda vya ndani ili tuweze kuvipunguzia VAT na kuzifanya kuwa zero- rated ili gharama ya mafuta ya viwanda viwe competitive na viweze kupunguza bei ya mafuta siku ya mwisho na kuvifanya kuwa competitive. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali itakapo-table bajeti mwezi wa Saba mtaona measures mbili za upande wa uzalishaji, vilevile mtaona measure za kidodi ambazo zitaweza kusaidia uzaishaji wa ndani lakini vile vile hata mafuta tunayo-import kutoka nje kuweza kuyapunguzia bei.

Mheshimiwa Spika, eneo lingine ambalo nilitaka nichangie, niwape uhakika Waheshimiwa Wabunge hatuna upungufu wa chakula ndani ya nchi. Hatuna upungufu wa chakula ndani ya nchi na kama Serikali tuna-reserve ya kutosha ambayo kwa zaidi ya miaka saba hatujawahi kuwa na reserve ya namna hii ya zaidi ya metric tons Laki Mbili ya chakula ndani ya nchi. Tukipitisha bajeti NFRA ataingia sokoni kwenda kununua mazao kwa ajili ya kuhifadhi ili tusiweze kuingia kwenye matatizo ya upungufu wa chakula ndani ya nchi, bila ku-disturb biashara ya mazao.

Mheshimiwa Spika, nishauri Waheshimiwa Wabunge tusi-restrict biashara ya mazao kwa hofu yoyote ile, kwa sababu kama Serikali tutatumia measure tulizonazo kuweza kupunguza mfumuko wa bei pale ambapo mahindi yamepanda, tutapeleka mahindi kwa bei ya Serikali ili kupunguza bei. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme jambo lingine kuhusu zao la korosho. Serikali mwaka jana tulifanya intervention ya kutoa pembejeo bila kulipia kwa wakulima, imetusaidia uzalishaji wa korosho msimu huu umeongezeka kwa zaidi ya asilimia 10 kutoka wastani wa tani 206,000 kukaribia tani 240,000. Mwaka huu tena tutapeleka pembejeo zenye thamani ya Shilingi Bilioni 90 bure kwa wakulima wa korosho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile tutapeleka pembejeo zenye thamani ya shilingi bilioni 56 kwa wakulima wa pamba. Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo kuhusu kutafuta njia kuanzia tarehe 01 Julai ya kupunguza bei ya mboleo kwa mazao na Serikali tunachukua hatua ili kuweza kuwapunguzia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu korosho jambo moja nataka nitumie Bunge lako. Vyama vya Ushirika vilikusanya fedha za wakulima ili waweze kuchangia kununua pembejeo, kupitia Bunge lako kuviagiza Vyama vya Ushirika vyote virudishe fedha za wakulima wote. Wakulima watapata pembejeo bila kulipia, kwa sababu Serikali inaitumia export levy kwa ajili ya ku-support zao hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilitaka niongelee hoja ya Mama Kilango.

SPIKA: Sekunde 30.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ok. Nataka tu nimuombe Mheshimiwa Mama Kilango na Wabunge wote wa Mkoa wa Tanga na maeneo yanayozalisha mazao ya viungo. Serikali imeiagiza TARI kupitia TARI Mlingano kuanzia sasa uzalishaji wa mbegu na research zote za mazao ya viungo itafanyika kwenye Taasisi yetu ya TARI - Mlingano na tunaanza uzalishaji wa mbegu kwa ajili ya tangawizi na mazao mengine ya viungo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwaombe kwamba haikuwepo kwenye plan ya Serikali kwa muda mrefu zao la viungo kama zao la kimkakati, sasa limeingia kama component ya mazao ya horticulture na tutatoa utaratibu unaostahili. Nashukuru. (Makofi)