Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri. Pia na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa anayoifanya pamoja na hotuba nzuri.

Mheshimiwa Spika, naomba nichangie katika maeneo matatu; kwanza Finance Bill ijayo ilete na mabadiliko ya matumizi ya fedha za export levy kwenye zao la korosho ili zitumike pia kuendeleza sekta ya korosho.

Pili, miradi ya gesi asilia na LNG ianze kutekelezwa ili kuinua uchumi wa watu wa Lindi na Mtwara na Watanzania kwa ujumla. Mazungumzo yanayoendelea yaharakishwe na utekelezaji uanze.

Mheshimiwa Spika, Kitengo cha Maafa kishughulikie maombi ya Wabunge wa Nanyamba na Tandahimba na barua ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara yanayohusu wananchi wa vijiji vilivyovamiwa na kikundi cha maharamia kutoka Msumbiji wapewe msaada wa kibinadamu. Vijiji hivyo ni Kitaya, Kilimahewa (Nanyamba) na Kilimahewa (Tandahimba).