Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa mchango wa maandishi kuhusu tohara ya kitabibu na natambua juhudi za Serikali katika jambo hili.

Mheshimiwa Spika, pamoja na wanaume wengi kujitokeza kufanya tohara lakini bado baadhi wanaona aibu, nashauri campaign iendelee pia kwa kuwashirikisha wale wanaume waliofanyiwa tohara wakiwa na umri mkubwa na pia Wabunge na viongozi wanaotoka maeneo yasiyofanya tohara kwa wanaume wafanye campaign hiyo ili kupunguza maambukizi mapya ya VVU. Hali kadhalika ushauri utolewe kuwa watoto wa kiume watahiriwe wakiwa wadogo ili kuwaondolea kadhia ya kutahiriwa katika umri mkubwa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.