Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Mawaziri wote kwa ytendaji mzuri katika Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajikita katika maeneo yafuatayo; miundombinu, afya, maji na elimu.

Mheshimiwa Spika, nianze na miundombinu; naomba Serikali iangalie upya mradi wa DMDP, uangaliwe upya kwa umuhimu wa Jiji la Dar es Salaam na hasa Wilaya ya Kigamboni na Ubungo ziwe kipaumbele. Lakini pia barabara ya Nzasa - Kilungule nayo sasa ikamilike. Mradi umechukua muda mrefu sana. Barabara hii ni muhimu sana kwa wakazi wa Buza na wale wanaoenda Mbande na Kongowe.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa afya, naipongeza Serikali kwa ujenzi wa vituo vya afya, naomba Serikali iangalie jinsi ya kupanua Hospitali ya Mbagala Zakhiem kwani imezidiwa, idadi ya wagonjwa ni kubwa sana.

Kwa upande wa elimu, naipongeza Serikali kwa ujenzi wa madarasa mapya, lakini niiombe Serikali sasa iangalie ukarabati wa shule kongwe na hasa maeneo ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Kuhusu suala la maji, niiombe Serikali waendelee na mpango wake wa ujenzi wa Bwawa la Kidunda ndio suluhisho la upatikanaji wa maji kwa muda wote katika Mkoa wa Dar es Salaam. Naomba sana Serikali itekeleze mradi huo. Mradi wa Visima vya Kimbiji na Mpera sasa ukamilike ili wananchi wa Kigamboni na Mbagala waweze kupata maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja.