Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO: Mheshimiwa Spika, mchango wangu umejielekeza katika ukurasa wa kumi na moja ambapo hotuba hii imejielekeza katika kuboresha usafiri wa abiria na mizigo katika maziwa makuu.

Mheshimiwa Spika, niendelee kuipongeza Serikali kwa kuendelea kujenga miundombinu rafiki ya usafirishaji abiria na mzigo. Ujenzi wa meli mpya ijuilikanayo kwa jina la Hapa Kazi Tu unaoendelea Mwanza kwa sasa umefikia asilimia 65; ushauri wangu kwa Serikali wale vijana wetu wazawa ambao wameshiriki katika utengenezaji wa meli hiyo itakapomalizika kutengenezwa ni vema kupewa kipaumbele kwa kupatiwa ajira katika meli hiyo kwa sababu ninaimani kubwa pindi wakipatiwa ajira katika meli hiyo watakuwa na uzalendo mkubwa kwa kuitunza ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na pia naomba kuwasilisha.