Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa kunipa nafasi nichangie huu mpango wetu, Mpango wa Tatu wa maendeleo katika nchi yetu. Pamoja na muda nisiache kumshukuru sana Mheshimiwa Rais na kuendelea kumpa moyo mkubwa kabisa kwamba kazi anayoendelea kuifanya kwenye nchi haina mfano na tunaendelea kumuombea kwa Mungu aendelee kumpa afya njema ili Watanzania waweze kuendelea kuona matunda yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nitasema jambo moja tu ambalo Serikali imeanza kulifanyiakazi lakini naona hatuendi nalo kwa speed nalo ni eneo la usimamizi wa maafa nchini. Nikitambua tayari Kifungu cha 35 cha Sheria ya Bajeti Sura ya 439 kinaeleza wazi juu ya kuanzishwa kwa Mfuko huu, lakini ukweli Serikali hapa kupitia Kamati ya Kudumu ya Sheria na Katiba Mwezi Febuari 14, 2022, Kamati iliwasilisha hapa juu ya Mapendekezo ya Muswada wa Sheria kwenye jambo hili. Septemba mwaka huu 2022 Waziri Kaka yangu Simbachawene naye aliwasilisha Muswada wa Sheria wa Usimamizi wa Maafa Nchini, ni jambo jema sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli kwamba bado Mfuko huu aujaanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Bajeti. Lazama tukubaliane inawezekana umuhimu wenzetu hawajaujua bado. Kwa nini tunahitaji kuharakisha mfuko huu kupatikana? Niwakumbushe tu Waheshimiwa Wabunge, juu ya majanga mengi nchi ambayo tumewahi kuyapata katika kipindi cha miaka kadhaa. Mwaka 1996 Tarehe 21, Mei, tulipata maafa makubwa kupitia MV Bukoba, wananchi wanajua. Ni kweli kupitia taarifa ya Jaji Robert Kisanga tuliweza kupoteza wananchi wetu, watoto wetu, wazee wetu 391 dhidi ya waliookolewa 114 tu, unaweza ukaona hili ni janga!

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hilo tu ni juzi tu MV Spice tarehe 10 Septemba 2011, zaidi ya maiti zilipatikana 243 lakini waliokutwa hai ni 900 tulipoteza hawakupatikana kabisa zaidi ya 1,370 hata kupatikana. Niwakumbushe tena kwa haraka kupitia maji tu Bahari na Maziwa ajali kubwa ya MV Skagit mwaka 2012 wananchi zaidi ya 222 walipoteza maisha, kuna MV Julius mwaka 2017 pia MV Nyerere mwaka 2018 ambayo ilikuwa inatokea Bungarara kuelekea kwenye Kisiwa cha Ukara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya majanga ni makubwa kama nchi. Tumepoteza ndugu zetu wengi, nini maana ya Mfuko huu? Mfuko huu utatusaidia pale ambapo haya majanga ambayo yameendelea nimeyataja ikijumuishwa hata hiyo ya juzi ya ndege, tungeweza sasa hapa kuona fedha za haraka za dharura ambazo zingeweza kusaidia hata kupeleka Jeshi letu la Navy la Uokoaji, katika maeneo ya kimkakati na tukaweza kuwawezesha kupitia Mfuko huo.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile moto. Masoko yetu mengi, Soko la Kariakoo tumelikarabati kwa Billion 32, Mheshimiwa Waziri Mkuu alienda pale kukarabati tu, Soko la Mwanjelwa - Mbeya, Soko la Ilala kwa Naibu Spika lakini hata Mwenge zaidi ya bilioni 50. Madhara yake ni nini kama hatuna Mfuko huu? Madhara yake mpango wa kama huu na bajeti zetu tunazoziweka kila mwaka zinaenda kuharibiwa, maana yake yale tunayotarajia kuyafanya activities zinazotakiwa kufanywa haziwezi kufanyika. Kwa sababu dharura imekuja hatujajipanga nayo tunaenda kuchukua hela maana yake ni activities nyingine zinaweza zisifanyike. Kwa hiyo, ni maombi yangu sana Mfuko huu ninajua nia na dhamira ya Serikali ndiyo maana tumeanza na sheria basi tuelekee kwa sababu ndiyo nia yake kwenda kuanzisha Mfuko huu tukaanzishe haraka ili tuweze kufika sehemu salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mengi watu wanayajua. Mlima Kilimanjaro zaidi ya siku 15 tumeshindwa kuuzima hata ule moto ni hatari, haya madhara yake ni makubwa karibu hata manne, moja ni uchumi wa nchi yetu lakini la pili ni mapato watalii hawawezi kuja leo kwa haraka lakini vilevile ina-distort hata ile goodwill ambayo tunayo kama nchi ndani ya vivutio vyetu hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ajali hizi zinawapa umaskini watu wetu. Amezungumza role model wangu, Mheshimiwa Kaka yangu pale Mheshimiwa Hasunga, kwamba ni ukweli mpango wetu unazungumzia juu ya dhima ya kuona maendeleao ya watu wetu. Sasa kama watu wetu wanakufa na hatuna mipango ya dharura kutengeneza Mfuko wao hili dakika ikifikia pale tunachukua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka, leo tunafanya nini kwa sasabu hatuna mfuko huu? Tunaenda Fungu 21 tunachukua hela pale haiwezekani, hatujawahi kuukuta ule Mfuko lile Fungu 21 lina hela muda wote. Kwa hiyo, ni vizuri na ni muhimu sana tufike sehemu tuone umuhimu wa Mfuko huu.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Naunga mkono hoja (Makofi)