Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kunipatia fursa ya kuchangia kidogo kwenye hoja ambayo iko mbele yetu. Napenda kuwapongeza Wizara ya Fedha kwa kazi hii nzuri waliyotuletea hapa na ambayo tunaijadili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Mheshimiwa Hasunga anasema hapa nilikuwa nasoma kitabu kimoja, kimeandikwa na Professor Keith Penny, Professor of psychology and neuroscience. Kwenye hicho kitabu kuna sentensi moja inasema “it takes money to make money”.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunachangia Kamati zetu zile tatu, kulikuwepo tatizo kubwa ambalo tulibainisha. Mashirika yetu mengi yanaendeshwa chini ya mtaji wake, yanahitaji mtaji. Kulingana na hiyo quote ambayo nimeisema, bila kuwekeza kwenye mashirika yetu ya umma tusitegemee miujiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita kidogo kwenye kilimo, kwa sababu watu wengi miongoni mwa watu wangu wa Muleba ni wakulima na kama tunavyofahamu zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wamejikita kwenye kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani tatizo tulilonalo kama nchi, wasemaji wengi wamesema, tunalo tatizo na lazima tutafute tumejikwaa wapi ili tuweze kutoka pale. Nikiangalia mfumo wetu wa Taifa tumejifunga kwenye kanuni na sheria zetu ambazo nyingi zinatukwaza. Kule kwetu Mheshimiwa Bashe anafahamu nimemwona pale, kila ikifika mwezi Julai lazima nimwone Mheshimiwa Bashe. Sisi ni wakulima wa kahawa, lakini ikifika mwezi Julai, Agosti tuna task force nyingi kuliko think tanks za kutuletea suluhu ya matatizo yetu. Tutaunda task forces tunaanza kukimbizana na wakulima wadogo wadogo wenye gunia moja, debe mbili eti magendo, tunawakwaza wakulima na wengi wanakata tamaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huko kwetu watu wengi walingoa mibuni na tunayo Sheria ya Kahawa, inasema eti kahawa ni mali ya Serikali. Kati ya sheria mbovu na hiyo ni moja ya sheria mbovu. Mheshimiwa Bashe wakati tunaongea pale alisema anataka free market, sasa inapokuja free market, let make it a free market for every crop for every business, tufungue soko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazo taasisi za udhibiti, tunayo taasisi ya Fair Competition katika nchi hii, tuiachie ifanye kazi yake. Wakati mwingine tunakimbizana na hawa watu wadogo wadogo hawa, ukiangalia wakulima wa kahawa kwa mfano Kagera, zaidi ya asilimia 90 ni wakulima wadogo wadogo ambao baada ya kuvuna mazao yao tunaanza kukimbizana nao. Hayo mazao wanayapeleka wapi? kama kule wanakoyapeleka kuna soko zuri, bei nzuri, kwa nini tusije na utaratibu mzuri tukawawekea utaratibu mzuri wakauze kule tukakusanye kodi sisi kama Watanzania? Kuna tatizo gani kwenye hilo? Tuachane na mfumo wa ku-paralyze soko kwa kuwafungia wakulima kana kwamba ni wezi, kana kwamba ni smugglers, kana kwamba yaani hawana; mazao wamezalisha wenyewe lakini tunapambana nao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye uvuvi, tatizo ni lilelile. Ukiangalia tozo za sekta ya uvuvi na ukizilinganisha na nchi nyingine, ndio maana ukiangalia nchi jirani Uganda, Kenya wanafanya vizuri kwenye uvuvi. Sisi wenye sehemu kubwa ya ziwa tunapata mapato kidogo kwa sababu ya tozo tulizonazo. Huu siyo muujiza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye tozo tulizonazo kwa mfano fillet, Tanzania ile viwango vya tozo kwa kilo tunatoza shilingi 552, wenzetu Uganda wanatoza shilingi 115, Kenya shilingi 34.51 hizi ni hela za Kitanzania. mabondo sisi tunachaji shilingi 7,500, wenzetu Uganda shilingi 460, Kenya shilingi 34. Vichwa vya samaki sisi tuna- charge shilingi 46, wenzetu Uganda shilingi 115, Kenya shilingi 34, ndio maana tunakula vichwa hapa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni mtu gani ambaye ataingia kwenye ziwa akuletee wewe mazao ya uvuvi badala ya kuyapeleka kule ambako tozo na tozo nyingine ziko much more user friendly. Sisi kwetu tozo ziko juu sana, tuangalie haya mambo Mheshimiwa Waziri wa Fedha tunapokuja kutengeneza hizi. Tunavutiaje haya mazao kwetu? Ndio maana Uganda tunavyoongea wana viwanda 20, sisi tuna viwanda nane, Kenya wana viwanda vitano, lakini ukiangalia ziwa tunalolimiliki sisi ni zaidi ya asilimia 50, liko kwa upande wetu. Hata ukiangalia mauzo ya nje, tunavyongea leo, Uganda wanafanya vizuri zaidi kuliko sisi na nchi ya pili baada ya Nigeria, lakini sisi tuko wapi kwa sababu ya mifumo tuliyojiwekea ya sheria, kanuni, tumejifungia kiasi kwamba tunajitengenezea umaskini sisi wenyewe kwa kujua au kutokujua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana Mheshimiwa Hasunga alikuwa anasema we are living in the cycle poverty na hii tumeitengeneza sisi wenyewe kwa kanuni zetu, sheria zetu. Tukae chini tuangalie ni wapi kanuni zetu zinatufunga, ni wapi sheria zetu sio nzuri, ni wapi competitive advantage tunaweza tukaitumia tukijilinganisha na mataifa jirani, tusijifungie ndani, tukadhani sisi ni kisiwa, sisi tunafanya biashara peke yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na naunga hoja mkono. (Makofi)