Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi nikachangia Mapendekezo ya Mpango huu wa Taifa wa Mwaka 2023/2024. Mpango huu ni wa tatu katika mpango wa miaka mitano wa 2022 mpaka 2025/2026 na mpango wetu huu unadhima ya kukuza uchumi shirikishi na uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunalenga kukuza uchumi wa viwanda na uchumi shirikishi tunategemea mpango wetu huu ungeangalia zaidi catalyst (vichachua uchumi). Vichachua uchumi vyetu hivi ni viwanda ni nishati ni usafiri na usafirishaji ni muhimu sana. Toka tumesema Tanzania ya viwanda bado hatujafanya vizuri kwa viwanda. Viwanda ni kichachua uchumi kwa wazalishaji wote; kwa wakulima kwa wafugaji na hata kwa wachimba madini. Wakiwa na uhakika kwamba viwanda vipo pale kwa ajili ya kusindika, uzalishaji utaongezeka kwa sababu ya uhakika wa soko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini viwanda ndivyo vingeenda ku-solve changamoto ya aijra ya vijana tunayoisema kila siku. Vile vile, viwanda hivi ndio vingesaidia kuongeza kipato kwa mkulima kwa kuongeza mnyororo wa thamani. Wenzangu wamesema, tunazalisha na tunauza malighafi kwa wenzetu. Tunazalisha korosho, pamba, mahindi vinaenda kama malighafi, tunaenda kujenga viwanda vya wenzetu wanasindika na sisi ndio walaji wanaturudishia. Sasa tubadilike na sisi tukatafute masoko ya vitu ambavyo tayari tumeshavi-process kwenye viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishati ya umeme ni muhimu sana kama kichochezi cha uchumi katika Taifa letu. Niwapongeze tu Wizara tu kwamba wameweza kufikia vijiji 9,160 kati ya vijiji 12,400 na kitu. Umeme ni kichochea uchumi muhimu sana, ni haki ya kila Mtanzania kupata nishati ya umeme. Umeme ambao tayari umekwisha kupelekwa unaishia katika center za vijiji ambapo unapaswa umeme kufika kwenye vitongoji kama ilivyo dhima yetu ili kila mtu a-enjoy kuwa na umeme katika eneo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme unatoa ajira kwa vijana walioko vijijini watatengeneza visaluni vyao watukuwa na viwanda vidogo vidogo vya welding wengine watamwagilia kwa kutumia pump. Vile vile ungepunguza hii rural-urban migration, kwa sababu vijana wanaomaliza chuo kikuu ukawapeleka kwenye vijiji ambavyo havina umeme wasingeweza kukaa huko. Umeme tunahitaji wa kuaminika, unajenga fursa ya wawekezaji nikivutio kwa wawekezaji kuja kama kuna umeme wa uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natamani mpango huu sasa utuambie, pengine uhakika wa umeme, tungeweza kuupata baada ya kukamilisha mradi mkubwa huu wa Julius Nyerere ambao tulitarijia kupata mega watts 2,115. Mradi huu umeanza tangu Disemba 2018 nawapongeza kwamba tumefikia sehemu nzuri asilimia 77 lakini tumekwisha kuwekeza 1.2 trilioni. Sasa ili weze kutoa output tunakila budi kuona kwamba mpango ukoje na mpango kazi ukoje, kwamba katika mpango unaokuja, tukamilishe ili tuweze kupata umeme wa uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, usafirishaji ni changamoto kubwa sana. Usafirishaji huu ndiyo sababu kina mama zangu kule wanalalamika bei kubwa ya vifaa wanavyovitumia, bei kubwa ya pembejeo, kwa sababu barabara na vivuko ni ngumu. Nategemea mpango huu uwekeze vya kutosha kwa TARURA na TANROADS ili barabara zetu na vivuko vipitike mwaka mzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni shida sana, wakulima wamezalisha kule, kuja kuleta mazao yao mjini ni kazi kubwa na yanaharibika mwengine ni perishable foods, zinakaa pengine kwenye usafirishaji siku nzima au siku ngapi baada ya magari kukwama, unakuta kwamba uharibifu wa mazao ni mkubwa sana. Kwa hiyo, tuangalie hizi pillars katika mpango wetu huu. Kwamba lazima tuboreshe hizi viashiria ili kwamba tuweze kukuza uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mpango huu nategemea pia utaendelea kuwekeza katika sekta za kiuchumi ambayo ni kilimo, mifugo, maliasili pamoja na madini. Mimi nawapongeza sana kwamba tumeshafanya vizuri kwa kuongeza bajeti iliyopita, tumeongeza bajeti zaidi ya mara tatu na tumeanza kuona matokeo makubwa. Sasa ninafikiri uwekezaji huu lazima tuone ni maeneo gani hasa tutawekeza kwenye kilimo. Sehemu ambayo ina - risk kidogo na sehemu ambayo tukiwekeza miradi mikubwa, tukawekeza fedha nyingi itaweza kurudisha kwa mapema, yaani pay back period iwe ndogo. Kwa mfano, naipongeza Wizara kwa mpango wake, sasa hivi tunatakiwa tuhamie kwenye uwekezaji wa mashamba makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona Wizara imekwisha kupata ekari 183,000 hapa Chamwino. Mimi nawapongeza kwa sababu kuwekeza katika mashamba makubwa ya pamoja (block farming) ina faida kubwa kwa sababu ni mashamba yapo pamoja uzalishaji utafanyika kwa gharama ndogo, itakuwa economical of scale lakini rahisi kusambaza teknolojia. Vile vile sasa kuweza kupata soko, mazao yanayotakiwa kwa ile quality. Kwa mfano shamba lilipo hapa kama tunawapata assignments watazalisha soya itaenda kuzalisha ile soya ambayo tayari tuna soko lake nje. Basi jitihada hizi zifanyike kwa zone. Kila zone agro-zone, kwa mfano hata Manyara tungeweza kupata mashamba Kiteto, basi yapatikane mashamba yaangaliwe hali ya udongo hata tuka - assign pengine ikazalisha hata mahindi ya njano ambayo tayari tunasoko Misri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mpango huu ni mzuri nawapongeza. Kwamba hatuna risks zozote za kuwekeza katika kilimo kama hicho, na kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji ambacho risks zake ni ndogo. Fursa ni nyingi kwenye kilimo, tumeona kwamba maeneo yanoyofaa kwa kilimo ni zaidi ya hekta milioni 44 na ambazo tumeweza kulima asilimia 38 mpaka 40. Kwa hiyo zaidi ya asilimia 60 ya eneo linalofaa kwa kilimo bado halijatumika. Kwa hiyo, bado tunaweza kuweka wawekezaji ambao unalima na ambao hauna risks kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nikifikiria kwamba tungeweza kuwekeza pia kwenye mifugo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namalizia ahsante sana. Tungeweza kuweka kwenye ranch zetu kule tukanenepesha mifugo au tukazalisha malisho ya mifugo kwa matumizi ya ndani na nje tungeweza pia kufanya vizuri. Nakushuru sana, naunga hoja mkono. (Makofi)