Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri na mpango aliouleta. Pia naipongeza Serikali kwa ujumla kwa kuendelea kusimamia bajeti yetu vizuri ambayo tuliipitisha mwaka wa fedha unaoendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali, nimeona kwenye taarifa ya utekelezaji tayari mmelipia ndege tano, na katika hizo ndege tano, ndege moja ni kwa ajili ya mizigo. Ninaipongeza sana, na hii inatukumbusha kwamba uchumi tunaokwenda kuupigania ni uchumi ambao hakuna namna, lazima kama tunataka kukuza utalii tuwe na ndege za kutosha. Juzi tukio la kuanguka kwa ndege kule Bukoba, linatupa picha kwamba kama nchi tunapaswa kuwa na a very strong airline ambayo inaaminika na yenye ndege ambazo watu wanapokuja Tanzania wana uhakika nazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipindi tunachangia hoja za Kamati juzi, mchangiaji mmoja alisema anashangaa kuona Shirika limewekeza Bima fedha nyingi compared na Precision Air. Sasa factor namba moja ndiyo hiyo kwamba Shirika letu lina ndege mpya nyingi na pengine ndiyo sababu na tahadhari ambazo zimechukuliwa zinaweza kutufundisha kuwa na Bima nzuri zaidi yanapotokea majanga. Mheshimiwa naipongeza sana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo nataka kulizungumza haraka haraka, huko nyuma tulipiga kelele sana kuhusu blueprint na ikazungumzwa sana kwenye level ya juu, lakini hii blueprint nadhani imekomea kwenye level za juu na haijatafsiriwa kwenye halmashauri zetu. Mwenyekiti wa Kikao cha wafanyabiashara kwenye Wilaya ni Mkuu wa Wilaya, halafu DED ni Mjumbe (mtu wa kawaida), lakini DED ndiye anaye-deal na wafanyabiashara. Kwa hiyo, naomba Serikali iiteremshe hii blueprint kule chini ili ikasaidie kutafsiri tulichokiwaza wakati tunaianzisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nataka kuzungumza hapa kwa haraka ni utalii. Kwenye eneo hili nazungumza eneo moja tu. Miaka yote ya nyuma nimeangalia bajeti ya Mheshimiwa Waziri, tumetoka kwenye makadirio ya Shilingi trilioni 41, tumekwenda kwenye Shilingi trilioni 43. Tunahitaji kubuni maeneo ambayo tutapata fedha nyingi. Kuna eneo moja ambalo tunaweza tukalifanya vizuri vikiungana mkono na ndege zinazokuja na huu ni utalii wa mikutano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema kwenye michango yangu muda fulani kwamba utalii wa mikutano siyo kama wa watu wanaokuja kwenye holiday tourism, hapana. Ila ni lazima tuwe na kitengo cha kufanya lobbying kuvuta mikutano mikubwa ije Tanzania. Bila kufanya hivyo, tutaisikia tu mikutano mikubwa inafanyika nchi jirani, halafu sisi hatuwapati hao watalii tunaowazungumzia. Kwa hiyo, sasa lazima Serikali ifanye jambo hilo na ianzishe sasa kwa bidi kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo nataka kuzungumza sasa kwa kina kidogo ni uvuvi. Nimeona Serikali imetenga eneo la uvuvi, nami nataka kusema kwamba mpaka leo bado hatujatumia vizuri uwepo wa Ziwa Victoria na bahari. Nilikuwa naangalia takwimu za Wizara, nikaangalia trend ya export ya Nile page, ukiangalia kwenye latest report pamoja na ukubwa wa ziwa tulilonalo, tulipata dola 132,000 ambazo ni takribani kama shilingi bilioni 300 za Kitanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jirani yetu ambaye anamiliki asilimia saba mpaka tisa alipata karibu shilingi bilioni 400 hadi shilingi bilioni 500, maana yake hatujatumia vizuri. Baharini, huku hali ni mbaya zaidi. Pamoja na ukubwa wa territorial na maji tuliyonayo yote yale, tuliuza nje thamani ya fedha zisizozidi dola 40,000 na Serikali ikapata kodi ya dola milioni 62; na hizi ni taarifa latest kutoka Wizara yenyewe. Naangalia hapa shida iko wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, hatujafanya uwekezaji wa kutosha. Ni kweli Waziri amesema tunatenga fedha kwa ajili ya kujenga meli baharini, lakini it is very scientific kwamba meli ile yenyewe tu peke yake haiwezi kutuongezea mapato. Kwa sababu Meli ambazo zinaweza kutuongezea mapato ni lazima ndani ya muundo wenyewe wa meli mle ndani iwe na miundo ya kufanya processing, kufanya parking, freezing na unapovua samaki unapata bycatch nyingi. Kuwe na mfumo wa kutoa zile bycatches lakini na link ya masoko. Naangalia Serikali inataka kufanya hiyo biashara, itaweza? Tutaweza kweli ku-breach hiyo gap tunayoifikiria? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huko nyuma tulikuwa na TAFICO, nami wakati nasoma fisheries nilifanya field TAFICO. Kwa nini ilikufa? Ni kwa sababu Serikali ilifikiri ikiwa na meli yake inaweza ikafanikisha kupata mapato ya uvuvi baharini, lakini ni jambo lingine kabisa. Sisi tunge- invest kwenye kuhakikisha kwamba tunapata teknolojia latest ikawawezesha Watanzania ambao wanavua samaki Ziwa Viktoria na baharini, kuwa na teknolojia ambayo ni latest wakaweza kuvua kuhifadhi, ku-process na kutafuta masoko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, alizungumza mtu mmoja hapa juzi kwamba kuanzia Tanga mpaka Mtwara hakuna kiwanda cha samaki. Ukitengeneza meli za Shilingi bilioni 40, ukanasa samaki kule tani 60, utauza raw, utapeleka Soko la Kariakoo, na kadhalika, ili uweze ku-transform fikra za kufikiri tukapata fedha za kigeni. Kwa sababu lazima uwe na viwanda na viwanda havijengwi na Serikali. Tuwe na Kiwanda kikubwa kinachoweza kuprocess Samaki, kinachoweza kutafuta masoko nje; na masoko ya samaki ni very competitive. Sisi kwenye Nile page tunapambana na Kenya, Uganda na Tanzania, lakini always Tanzania bei yetu ni ndogo kuliko hizi nchi nyingine. Kwa hiyo, lazima tufikirie ku-invest peke yake na hizi meli kubwa hakutatusababisha tuongeze mauzo ya nje, jambo ambalo nadhani ni la msingi sana kwenye fedha hizi tunazowekeza, kwamba lengo letu ni kuongeza mapato na kuongeza wigo wa bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)