Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nakushukuru kwa siku hii ya leo adhimu kwa kunijalia kunipa nafasi hii katika Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa leo hii ni siku yangu ya kwanza kuchangia katika Bunge hili, nishukuru viongozi wangu wote walioniwezesha kufika hapa pamoja na Mwenyezi Mungu; nimshukuru Rais wangu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, kwa ushindi alioshinda wa kishindo siku ya tarehe 20 Machi, 2016. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia niwashukuru na wadau wangu walioniwezesha wa Mkoa wa Kusini Unguja, kuniamini na kunithamini wakanipa kura zao ili niwe Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kusini Unguja. Nasema sitawaangusha.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuchangia suala la Wizara hii ya Jeshi la Ulinzi na Kujenga Taifa. Kwanza niseme, alisimama mwenzangu hapa akazungumzia kwamba Jeshi limepindua Zanzibar. Jeshi halijapindua Zanzibar! Nataka kuuhakikishia ukumbi huu kwamba Serikali ya Mapinduzi tarehe 20…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa, Mwantumu, hiyo kauli ilifutwa asubuhi. Kwa hiyo, tuendelee. (Makofi)
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuendelea kuchangia, kuna ndugu zetu wa polisi ambao ni trafiki na pamoja…
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Usinishuhulishe!
Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa jitihada zao wanazozifanya katika Serikali ya Muungano huu wa Tanzania ninawapongeza kwa dhati. Hufanya kazi zao kubwa sana, kuimarisha Muungano ndiyo maana tumekuwa na utulivu, amani na uhuru wa nchi yetu. Nawaomba wazidi kulinda Muungano, wasirudi nyuma na wala wasitetereke. Waulinde, wausimamie na wautetee kwa maslahi ya nchi yetu na Serikali ya Jamhuri ya Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuendelea katika huduma za jamii, mfano afya, ujenzi na utalii kuwa karibu na wananchi kutoa mafunzo ya ulinzi ili wananchi wazidi kufaidika na kujijengea kwenye harakati za maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wetu wa Kusini Unguja tuna ulinzi wa uhakika kwenye Jeshi la Ulinzi na wanatusaidia vikubwa kutulinda na wala hatuna tatizo tunakwenda nao vizuri, tunashirikiana nao vizuri na ndiyo tumejivunia mpaka leo hii tumefikia hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nichangie kuhusu suala la ujenzi wa Kituo cha Mkoa cha Polisi Jumbi; kuna Kituo cha Mkoa wa Kusini Unguja kilikuwa kinafanya kazi pale Fuoni lakini Kituo kile kilihamishiwa Mkoa wa Kusini, Wilaya Kati pale Jumbi. Naomba Mheshimiwa Waziri, kwa udhati wako wa moyo, kwa imani yako, utusaidie kituo kile kiwe na jengo imara, lenye mvuto na pale lilipo ni njiani basi paonekane kwamba pana jengo la Kituo cha Polisi; na watu wote wanaopita pale wajue kwamba hili ni jengo la polisi la Mkoa wa Kusini Unguja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa jitihada na busara zake jinsi anavyoliendesha Jeshi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante sana.