Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Shamsi Vuai Nahodha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. SHAMSI VUAI NAHODHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza mchango wangu kwa kunukuu maneno ya Biblia takatifu; “watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.” (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Taifa tunapoangalia matatizo yanayotukabili ama yasababishwa na kiwango cha chini, ama yanasababishwa na ukoesefu wa maarifa, hasa ya sayansi na teknolojia. Tangu tupate uhuru mpaka sasa tunapoangalia mipango yetu ya maendeleo bado dhamira ya mipango yetu haijabadilika sana, lengo letu ni kupambana na umasikini na kukuza uchumi wa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo baadhi ya watu wanajiuliza mbona tumechukua muda mrefu sana kukabiliana na matatizo ya umaskini? jibu nitalitoa baada ya kunukuu maneno ya Abraham Lincoln, mmoja wa Marais wa Marekani, alisema maneno ha yana ninaomba tuyatafakari. Alisema, nikipewa kazi ya kukata mti na nimepewa saa sita, saa nne za kwanza nitazitumia kwa kunoa shoka na saa mbili za mwisho ndiyo nitaanza kati ya kukata mti; sasa tatizo letu la msingi lipo hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Taifa tunaujua ukweli huu, lakini bado tunashindwa kuutekeleza kwa vitendo. Kwa maoni yangu, ninapoangalia mpango sioni waziwazi kama elimu ndicho kipaumbele chetu namba moja. Watu wenye maarifa ya kutosha na sahihi wana uwezo mkubwa sana wa kufanya mambo makubwa katika Taifa lao. Wanaweza kulibadilisha jangwa kuwa ardhi ya kilimo, nitatoa mfano. Hakuna jambo linalonisikitisha sana kama kiongozi na kama Mtanzania ninapoona nchi ya Misri ambayo asilimia 60 ya nchi yake ni jangwa, wamejifunza sayansi na uhandisi wa kutumia maji ya kilimo cha umwagiliaji maji zaidi ya miaka 1,000. Watanzania tuna mito, tuna maziwa, tunashindwa nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Marehemu Baba wa Taifa alitambua sana umuhimu wa elimu hasa ya ufundi, ndiyo maana alitujengea vyuo vingi sana vya kati vya elimu ya ufundi, lakini kwa bahati mbaya sana viongozi tuliokuja baadaye tulivibadilisha vyuo hivi na kuwa vyuo vikuu. Kama kuna kosa la kiufundi tumelifanya basi ni jambo hili. Ushauri wangu ni nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu, naiomba Wizara ya elimu kama kweli tuna lengo la kupambana na umasikini tuwekeze fedha za kutosha, angalau asilimia 20 ya bajeti kwa ajili ya ufundishaji vijana wetu, hasa masomo ya sayansi na teknolojia, ili kukuza uwezo wa vijana wetu wa kufikiri, wa kubuni, wa kutatua matatizo na kutafuta mbinu na vifaa vya kutatua matatizo yetu. Na kama tunatoa elimu ambayo haina uwezo wa kuwasaidia vijana kufikiri, basi tunapaswa kufikiri upya. Na kama tunadhani elimu ni ghali basi naomba tuujaribu ujinga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)