Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Spika, kwanza ninamshukuru Mwenyezi Mungu Muumba mbingu na ardhi kwa kuzidi kunitetea, kunipa pumzi, kunipa uhai na kusimama katika Bunge hili Tukufu na kutoa hoja yangu katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Ninaipongeza hotuba ya Waziri Kivuli, kaka yangu Mheshimiwa Mwinyi yale mazuri yachukue yafanyie kazi ili tuboreshe Wizara yetu ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa isonge mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, Mheshimiwa Waziri ulitamka juzi ukasema Jeshi liko stand by, nataka niwaambie Jeshi liko stand by na Serikali iwe stand by kwa kupeleka bajeti ya Wizara kwa wakati ili wapate kutatua matatizo yanayowazunguka wanajeshi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Serikali iwe stand by kwa kuhakikisha vyombo vya ulinzi na usalama vinapatiwa makazi bora na vinapatiwa stahiki zote zinazotakiwa ndani ya Serikali. Tumehakikisha vyombo vya ulinzi na usalama vinakaa katika mazingira magumu, asilimia kubwa ya vyombo vya ulinzi na usalama havina makazi. Tangu Bunge lililopita, Bunge la mwaka 2010, nimekuwa mdau mkubwa sana wa Jeshi nikilalamika kuhusu vyombo vya ulinzi na usalama, hasa hivi vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo vipo mipakani, vimekuwa vikikutana na changamoto kubwa sana. Tuhakikishe sasa hawa mnawapa stahiki zinazostahili, wapate kwa wakati muafaka.
Mheshimiwa Spika, pia hapa pamezungumzwa sana kuhusu mambo ya wastaafu wa Jeshi, na mimi nitachangia kidogo kwa sababu baadhi ya wenzangu wamechangia.
Mheshimiwa Spika, leo hii tumeona kuna wastaafu ambao wamepigania nchi hii, wamekwenda Uganda. Tukaangalia, kwa mfano, tuliona wale wastaafu ambao walikwenda kupigana Uganda, wale wazee wengine wakarudi hawana viungo, wengine hawana mikono, leo hii wengine walishakufa, wengine wana ulemavu, wako Mgulani. Hawa wazee hebu kawaangalieni wamewakosa nini? Muwapelekee angalau sabuni, msiwatumie wakati wana viungo vyao wakishakuwa hawana viungo vyao mnakwenda kuwatafutia mahali mnawaweka kama scrapper. Niombe kwa kweli kazi ya Jeshi ni ngumu sana na Jeshi wanafanya kazi katika mazingira magumu na mwanajeshi hawezi kulalamika.
Mheshimiwa Spika, wewe mwenyewe ni shahidi. Tumefanya ziara katika Kambi za Jeshi Zanzibar, umeona mazingira ya Zanzibar yalivyo. Ukiangalia miundombinu ya Zanzibar, leo nenda kwenye zile mess za Jeshi zile utofautishe na hizi za polisi, zina tofauti kubwa sana. Sasa hivi mwanajeshi anauziwa kitu kwa bei kubwa sana katika mess zao zile za Jeshi. Mlisema kwa kipindi cha zamani walikuwa wakipata angalau vifaa kama vya ujenzi vinashuka bei, chakula kinashuka bei, leo nenda Jeshini pale uende kama mess ya Jeshi pale, nenda mwenyewe tumefanya ziara pale na nikakuambia, uangalie vitu vinavyouzwa ghali pale, hakina tofauti na kitu ambacho unanunua dukani. Sasa huyu mwanajeshi ataponea wapi! Ukiangalia yeye ndiyo mnamwambia akae stand by, hii stand by nawaambia siyo nzuri sana. Stand by mhakikishe nao mnawapa stand by zao. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Spika, uzalendo saa nyingine unaweza ukawa tena uzalendo mtu anashindwa uzalendo. Mhakikishe wanapata nao hizo stand by lakini siyo wawe stand by kwa Chama cha Mapinduzi kwa kule Zanzibar na huku Tanzania Bara. Kwa kweli hii stand by baadaye itakuja kuwageuka nawaambia kabisa! (Makofi)
Mheshimiwa Spika, suala lingine ukiangalia hawa wasaafu kwa kweli wengi wanapiga ramli wamekuwa waganga wa kienyeji sasa hivi. Mnawapa shilingi 20,000, unayempa shilingi 20,000 au shilingi 50,000 ukiangalia ni mtu ambaye ametumikia Jeshi na unajua ukishakaa katika kazi hii ya ulinzi na usalama, ukirudi uraiani huna rafiki kila mtu anakuona adui na ndiyo maana nasema mhakikishe wakiwa katika kazi hizi muwape hata angalau mikopo wajenge nyumba za kisasa waishi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, leo kuna rafiki yangu mmoja ni mwendawazimu, alipigana vita Marekani pale DC, lakini Serikali yake inamlipa mshahara, anakula vizuri, vile vitu ambavyo hawezi kutumia jamaa zake wanachukua wanakula. Ukienda kwake anaishi kama mfalme lakini ni mwendawazimu. Ninyi kwa nini watu ambao wana akili zao wengine hawana viungo, hawana nini mnashindwa kuwapa pesa lakini mnaweka pesa zikifika karibia na uchaguzi mnawaambia kaeni stand by. Niwaambie wanajeshi wote msikubali kukaa stand by, mtakaa stand by pale mtakapopata stahiki zenu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tukirudi nyumba za wakufunzi hawa ambazo ziko kambi za JKT, nyumba nyingi siku za mvua nendeni mzunguke, zinavuja, wanavujiwa. Mnakuta nyumba ipo lakini yale majengo ni ya zamani, sasa kitu gani hamtaki kuwajengea hawa wakufunzi wa JKT nyumba nzuri ili watoto wale wanaokwenda kwa mujibu wa sheria wapate kufundishwa vizuri na mwalimu. Lakini mwalimu anafundisha wanafunzi saa ya kulala mvua ikinyesha anasimama, baadaye uchaguzi ukifika kaeni stand by, hiyo ni sawa? Hakuna kukaa stand by hapo. Wote msikae stand by.
Mheshimiwa Spika, kuhusu vijana hawa ambao JKT tunawapeleka kwa mujibu wa sheria na katika hotuba yako nimeona umegusia pia Wabunge waende. Kwa kweli Wabunge waende kwa sababu hili Bunge wameingia vijana wengine ni mateja wa unga wamo humu, wengine wanavuta bangi, wengine wanavua mama zao nguo, mama zao wengine walishakufa, wanakuja humu Bungeni wanawatukana mpaka wazazi wao. (Makofi/Kicheko)
Kwa hiyo, niombe kabisa na Mheshimiwa Rais Magufuli vijana wote Wabunge ambao hawana nidhamu, hawana standard ya kuzungumza katika Bunge hili waende JKT. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Spika, Wabunge wote vijana ambao hawana nidhamu ya kuzungumza katika Bunge hili na waende na wale ambao hawajapitia, kwa nini watu wanakwenda kwa mujibu wa sheria, form six wanakwenda, na Wabunge wote JKT wakirudi wawe na discipline ya kuzungumza ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hawa vijana wengine wanaokwenda kwa mujibu wa sheria mkishawachuja wale vijana, ninaomba kwanza muangalie namna gani ya kuboresha vile viwanda vya VETA mle ndani ili wale vijana wengine watakaopata ajira na wengine wabaki pale.
TAARIFA
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU...
Mheshimiwa Maryam endelea, dakika zako nimezitunza.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana najua utanilindia tu muda wangu.
Neno teja pia liko kwenye kamusi ya Kiswahili, kaangalie, mengine kama nini pia na wewe utoe semina elekezi kwenye Wizara ambayo upo na Mheshimiwa Jenista Mhagama. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nilikuwa nakwenda kwenye suala la vijana ambao wamechukuliwa kwa mujibu wa sheria na wengine kwa kujitolea ambao wanapelekwa JKT, kuna wengine wanachukuliwa wanapata ajira, wengine hawapati ajira. Ninaomba Serikali ihakikishe viwanda vyote ndani ya kambi kuwe na VETA vijengwe viwanda ambavyo vijana wale watajiajiri, najua kuna mashamba ya kulima hata zile nguo wawe wanashona wenyewe ili tupunguze hizi changamoto kwa sababu wale vijana wakingia uraiani wanakuwa nao hawana kazi halafu wanaingia tena kwenye mambo ya uhalifu. Hilo naomba mlifanyie kazi ili vijana wale wapate kujiajiri.
Mheshimiwa Spika, pia zinapotokea nafasi kama nafsi zile za ulinzi, nafasi za ndani ya Serikali, wale vijana wapewe kipaumbele kwa sababu ni vijana ambao mmeshawafundisha namna ya kutumia silaha, kila kitu walishasomea sasa mkiwaacha kama hivi watashawishika baadaye wanaweza kwenda hata kujiunga na Boko Haram. Kwa hiyo, huo ndiyo ushauri wangu natoa kwa Serikali.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri suala lingine ninazungumzia ni kuhusu hii migogoro ya ardhi. Hii migogoro ya ardhi pia imezungumzwa sana na Mheshimiwa Halima Mdee pia pale kazungumza, utaona sana kwa upande wa Zanzibar kulivyokuwa na migogoro, kambi zote kwa sababu Mheshimiwa pia umekuwa msikivu na umzezunguka. Hizi beacon kuna ambazo zimewekwa tangu mwaka 1962, sasa zile beacons zimeshapotea.
Kwa hiyo pia uangalie namna gani kutatua hi migogoro kwa wakati na pesa zipelekwe. Hakuna kuwa standby mpaka pesa zipelekwe.