Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Naomba nami nichangie kwenye mpango huu, niongeze mambo matatu ambayo siyaoni kwenye mpango. Kabla sijaongeza hiyo, niseme kwamba mpango huu ni muhimu sana kwa sababu ndiyo mpango wa kwanza tangu tutoke kwenye janga la COVID- 19, lakini ndiyo mpango ambao utatuambia ni kwa kiasi gani tunaenda kukamilisha au ku-achieve our National Development Vision 2025. Umuhimu wake ni mkubwa sana na tunafahamu kwamba moja ya mafanikio ya jumla ambayo tuliyapata mwaka 2021 ni Benki ya Dunia kuitangaza Tanzania kwamba imefika uchumi wa kati (Lower Middle-Income Country) pamoja na kwamba suala hili itakuwa ni muhimu Mheshimiwa Waziri akalitolea msimamo baadae kwa sababu tunasikia takwimu zingine zinasema tumeshuka, nyingine tuko pale pale, ni muhimu Serikali ikaliweka vizuri jambo hili ni kubwa sana siyo jambo la kupita hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nilikuwa nasoma taarifa za World Bank kwenye website yao na Waheshimiwa Wabunge, mnaweza mka-google, wana-update kila baada ya muda fulani. Kwa mujibu wa takwimu hizi za Benki ya Dunia, nchi yetu mwaka 2021 ilikadiriwa kuwa na pato la dola za Marekani bilioni 67.78 na siyo bilioni 62. Ukifanya hesabu kwa idadi ya watu wa sasa hiyo inatupa GDP per capita income ya dola za Kimarekani 1,135.5. Kwa hivyo, utaona kwamba tumepanda kidogo kuliko mwaka 2020. Kwa hiyo, ni hoja kwamba tumeshuka haiwezi kuwa kweli na ni muhimu tukalinda mafanikio yetu kwa wivu mkubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ningeomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha utakapohitimisha hili jambo alitolee kauli nzito ya kueleweka ili nchi isibabaike. Tumeshuka au tuko pale?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo matatu ambayo ningependa kuyaangalia ambayo siyaoni kwenye mpango vizuri. La kwanza ni suala la umuhimu wa kuendelea kupambana na umaskini. Ukichukua mpango wetu wa maendeleo ukurasa wa kwanza kabisa kuna ujumbe mahususi wa Mheshimiwa Rais pale. Na katika ujumbe mahususi huo Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alieleza kwa uzito changamoto ya umaskini, na alitumia maneno haya naomba ninukuu; “Tunapoanza utekelezaji wa mpango wa tatu sote tunatambua changamoto nzito mbele yetu, umaskini bado unaendelea kuwepo nchini licha ya jitihada kubwa, zinazowekwa katika kuimarisha maendeleo ya watu. Aidha utofauti wa kiwango cha kipato na matumizi unaendelea kuwepo katika jamii zetu, ikiwa ni moja ya kati ya viashiria vikubwa katika kufikia malengo kusudiwa ya Dira ya Taifa ya Maendeleo. Moja ya sababu za msingi za maendeleo hafifu wa upunguaji wa umaskini licha ya ukuaji imara wa uchumi ni kutokufanikiwa kikamilifu kwa Tanzania katika kuongeza tija na uzalishaji katika sekta za msingi”.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ndio maneno ya Mheshimiwa Rais kwenye utangulizi wa Mpango wa Maendeleo. Anatambua kwamba, bila kuwekeza katika sera za msingi za kuongeza tija hatuwezi kutoka. Kwa hiyo hilo ni jambo kubwa lakini ikifika Mpango wetu wa Maendeleo wa Miaka Mitano, lengo namba 12 linazungumzia umaskini tu; na linasema, kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi jumuishi na shirikishi kupitia mikakati ya kupunguza umaskini. Hili ni jambo la msingi sana katika mpango wetu wa maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti utafiti wa Benki ya Dunia unaonesha waziwazi kwamba kutokana na janga la Covid watu 140,000 katika nchi hii walipoteza kazi katika sekta rasmi. Watu milioni 2.2 walipoteza kipato. Utafiti unaonesha vilevile kwamba bila kuchukua hatua mahususi watu 600,000 watatupwa kwenye dimbwi la umaskini. Kwa hiyo ni muhimu mpango wa maendeleo uoneshe jitihada za kushughulikia umaskini bayana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma mpango katika kurasa 161 nilikuwa na-set pale, katika mpango mzima neno umaskini limejitokeza mara moja tu, na limetajwa kwenye suala la kushughulikia kunusuru kaya maskini. Hii haitoshi, tuwaombe wataalam wetu warudi katika mapendekezo ya mpango watuletee mikakati ya kupunguza umaskini katika nchi hii, hili ni jambo la msingi sana. Katika mpango tutakaokuja kuupitisha mwezi wa pili tuone bayana mikakati inayoshughulikia umaskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili ambalo sijaliona ni suala la idadi ya watu. Nchi yetu sasa tunafahamu hatubahatishi tena, tupo milioni 61.7 na tumekua kwa kiwango cha asilimia 3.2, ongezeko kubwa kuliko miaka yote ya sensa. 1989 mpaka mwaka 2002 ilikuwa asilimia 2.9, 2012 ilikuwa asilimia 2.7 sasa hivi ni asilimia 3.2 ndiyo kubwa kuliko tangu tuanze kuchukua sensa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ongezeko kubwa la idadi ya watu lina sura mbili. Sura ya kwanza ni fursa, kwamba mpo wengi kwa hivyo nyie ni soko. Sura ya pili ni kwamba mna uhakika wa wafanyakazi wenye nguvu za kufanya kazi kwa sababu mko wengi. Pia uzuri ni kwamba kwa structure ya population yetu asilimia 70 wapo chini ya miaka 35. Kwa hiyo kwa kweli watu wetu wengi tulionao katika nchi hii ni watoto na vijana. Na ndiyo maana hata mimi mwenyewe mwenye miaka 50+ siku hizi vijana wananiita mzee. Mzee kwa sababu gani? nimekuja kugundua hata kama watu wengi ni watoto na vijana wewe miaka 50+ wewe ni mzee bwana, kwa hili ni sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ili uipate hiyo unahitaji nini? population dividends wanaita wataalam. Kwanza lazima uwekeze katika elimu sana. Lazima uwekeze katika mpango kupunguza umaskini, lazima uwe na chakula cha kutosha. Bahati mbaya sisi kwa sasa takriban kila kitu hakitoshi. Katika shule kama ni madarasa, kama ni waalimu, everything you talk about haitoshi, maana yake nini? lazima turudi katika miaka ya 1970, 1980, tuanze kuzungumzia suala la uzazi wa mpango, hili jambo haliwezi kukwepeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii ilikuwa champion wa family planning 1970’s, 1980’s na ndiyo maana tukaweza kupunguza ongezeko la kasi kiasi hicho. Hapa tulipofika lazima hilo lifanyike, na mimi napendekeza kabisa kwamba tufanyie mabadiliko Tanzania Commission for Aids tuiongezee jukumu la family planning. Haya ni pendekezo langu ambalo nimeona kwamba ni muhimu kwamba ni muhimu yaingie kwenye mpango wetu wa maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la mwisho, tumesema kwenye lengo namba 11 kuimarisha jukumu la Mamlaka ya Serikali za Mitaa katika kuleta maendeleo na kuongeza kipato katika ngazi ya jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwenye mpango huu, huoni chochote kuhusu kuimarisha Local Government Authorities. Nimeshasema na ninarudia tena. Itakuwa ni vigumu sana kwa nchi hii kudhani kwamba tunaweza kupinga kasi ya maendeleo from the center. Nchi hii ni kubwa, ina watu wengi lazima tuimarishe Serikali za Mitaa. Na katika kuimarisha Serikali za Mitaa tunazungumzia income, vyanzo vya mapato katika Local Government Authorities havipo. Tungetaka kuona mpango wa maendeleo deliberately kabisa unaanzisha vyanzo vipya vya mapato…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mkumbo kengele ya pili ahsante…

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nakushukuru sana. (Makofi)