Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuweza kuchangia kwenye rasimu ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka Mmoja. Nitajikita zaidi kwenye suala la kilimo, lakini muda ukiniruhusu nitajikita kwenye jinsi gani tunaenda kusimamia mapato ya ndani ya halmashauri zetu ili yatumike kwenye ile miradi ya maendeleo, ile asilimia 40.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wachangiaji wengi wameelekeza hapa, taarifa ambazo Dkt. Mwigulu ame- present hapa, zinaonyesha kwamba kilimo kinachangia takribani asilimia 3.9 kwenye pato la Taifa lakini sekta ndogo ya sanaa imechangia karibia asilimia 19 kwenye pato la Taifa, madini yanachangia asilimia 9.6 na biashara inachangia asilimia 3.5. We are not serious. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo kinachukua zaidi ya asilimia 65 ya Watanzania wameji-engage kwenye kilimo. Sasa hivi watu tulionao ni takribani milioni 61, asilimia 65 ya milioni 61 ni takribani watu milioni 40, wapo kwenye shughuli za kilimo. Sasa kama kilimo kinachangia only 3.9 percent kwenye pato la Taifa maana yake kwa mwaka ni watu milioni mbili tu ndio wanaji-engage kwenye kilimo. Ndio maana nilisema kwamba we are still not serious, tunahitaji kuipa kipaumbele Sekta ya Kilimo..

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ni siasa, siasa zetu hizi zipo kwenye kilimo, lakini kilimo ni amani, kilimo ni furaha, tukikosea kwenye kilimo, tumekosea uchumi. Kwa hiyo, tunahitaji kuwekeza sana kwenye kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Bashe alikuja na Mpango wa Pili wa Maendeleeo ya Kilimo (Agricultural Sector Development Plan II). Baada ya ule wa kwanza ulioisha 2014, tukatengeneza mwingine ambao tunao, lakini bado tunaangalia contribution ya kilimo kwenye uchumi, it is only 3.9 percent.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine watu wengi wapo kwenye kilimo na Mheshimiwa Mwigulu anaposema anataka kukuza uchumi, hawezi kukuza uchumi kama anaacha hawa wakulima ambao ni more than 65 percent, hapo tutakuwa tunadanganyana, daktari wangu wa uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tu-invest kwa hawa 65 percent, tuta-invest vipi, niliwahi kuwasilisha hapa Bungeni, sekta ya umwagiliaji ndiyo sekta ambayo tunaweza tukawakomboa wananchi wetu. Tanzania ukiangalia, kuna matatizo makubwa sana, climate change, semi-arid and arid areas, haya yote hayawezi ku-predict kama tuna uwezo wa kuvuna au hautuwezi kuvuna. Mheshimiwa Mwigulu lazima awekeze kwenye sekta ya umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo makubwa matatu ambayo yanafanya sekta ya kilimo isiweze kuchangia vizuri kwenye pato la Taifa. Kwanza, tume-ignore sana sekta ya umwagiliaji. Nitaonyesha, Bajeti yetu 2019/2020, Serikali ilitenga only 32 billion (bilioni 32) kwa ajili ya shughuli za umwagiliaji; mwaka 2020/2021 Serikali ilitenga only 12 billion (bilioni 12) kwa ajili ya shughuli za umwagiliaji. Mwaka 2021/2022, mama yetu akaongeza ikafika 46.5 billion kwenye sekta ndogo ya umwagiliaji. Mwaka huu, mama yetu akatupa bilioni 361.5 kwenye Sekta ndogo ya Umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza sana na kumshukuru sana Rais. Tumetoka 46 billion mpaka 361 billion kwenye Sekta ya Umwagiliaji. Mama yetu ana maono kwenye Sekta ya Kilimo kama nilivyotangulia kusema. Kama tuta-ignore Sekta ya Kilimo, tusitegemee uchumi wetu utakua kwa kiwango ambacho tunakitegemea, kwa hiyo lazima tuwekeze kwenye kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo manne ambayo yanatusumbua. Jambo la kwanza financing hata hii 361 billion ambayo tumeiweka mwaka huu, ukiongea na wataalam wa irrigation wanakwambia kama tunataka kilimo chetu kweli kijikite kwenye umwagiliaji we need a minimum of 600 billion (bilioni 600) kwa mwaka. Lazima tuchukue maamuzi magumu, tuwekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji. Tunahitaji a minimum 600 billion ili angalau tujikite kwenye umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna tatizo moja katika umwagiliaji, tuna miradi mingi ya umwagiliaji, lakini traditional irrigation, inasubiri mvua, mvua isipokuja zile scheme zote zinakufa. We need to shift, lazima tuhame kutoka huko. Tunahitaji kujenga mabwawa, najua mwaka huu Mheshimiwa Bashe amekuja na plan ya kujenga mabwawa, we need to transform our agriculture, lazima tubadilike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, tuna Tume ya Umwagiliaji, ukiangalia ile Tume, ipo Dodoma tu. Vile vile scope yake ni ndogo lazima tui-transform hii Tume. Nashauri upande wa Tume kwa nini tusi-transform iwe mamlaka. Nimepitia nchi nyingi, kwa mfano Kenya, Kenya wana National Irrigation Authority, Ghana wana National Development Irrigation Authority. Sasa sisi tuna katume kapo confined Dodoma, ukienda wilayani hukakuti, mkoani sijui ndiyo wana mtu mmoja na kadhalika, no, we need to shift. Kwa hiyo, nashauri hebu tuibadilishe hii tume yetu iwe na mamlaka kamili wawe na manpower. Tunahitaji kuona hii mitambo ipo located kule kwenye halmashauri zetu. Hiyo mitambo ya kujenga mabwawa, mitambo ya ku-repair hizo schemes zetu iwe kule, kuliko mtu anatoka Bukoba anakuja Dodoma kufuatilia mtambo uende ukafanye maintenance ya scheme iliyoko Bukoba. Kwa hiyo, niliona hilo ni eneo muhimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kama tunataka kubadilika kwenda kwenye kilimo cha umwagiliaji Serikali ni lazima iwekeze kwenye man power. Tunahitaji vijana ambao ni trained kwenye masuala ya irrigation system. Tunahitaji watu wa cheti na diploma, hawa ndiyo watakaofanya kazi na wakulima kule vijijini, hatuhitaji masters na degree kule vijijini, tunahitaji watu wenye certificate pia wale wenye diploma ambao wataweza kusaidia huku, hilo ni eneo jingine ambalo niliona nilishauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo niliona nishauri ni kwamba, ukiangalia scheme zetu nyingi zimechoka sana na nyingi zinategemea mvua kama nilivyosema, tunahitaji kujenga mabwawa. Hatuwezi kujenga mabwawa kwa bajeti ambayo tunaweka, hata hivyo tunamshukuru Mheshimiwa Rais ameliona hili mwaka huu ndiyo maana ame-shift bajeti from 46 Bilioni to 361 billion haijawahi kutokea, nine times. Kwa hiyo hilo ni eneo ambalo ninaomba bajeti ya mwaka huu Mheshimiwa Mwigulu, tunahitaji kuona bajeti angalau ni ya Bilioni 600. Tunataka watu wajikite kwenye kilimo cha umwagiliaji ili tuweze ku-transform kilimo chetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho, pale Manyoni nina mradi wangu mmoja unaojulikana kama mradi kwa ajili ya ukaguzi wa magari wa pamoja. Mheshimiwa Mwigulu anaufahamu, ule mradi upo chini ya Wizara ya Fedha ulisimama tangu mwaka 2016. Sasa ninakuomba Mheshimiwa Mwigulu, hii ni miradi ya kimkakati ambayo inakuja kuchochea masuala ya uchumi. Hebu nalo liangalie ule mradi wa Muhalala ambao ulisimama pale tangu 2016, mradi wa zaidi ya Bilioni 35 na wenyewe tuufufue ili uweze ku-stimulate kwenye masuala ya uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana. (Makofi)