Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nichangie mchango wangu kwa kuanza kuipongeza Serikali ya Chama Cha Mapinduzi inayoongozwa na Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kazi nzuri wanayoifanya. Pamoja na mambo mbalimbali ya msukosuko wa uchumi duniani, lakini inafanya kazi yake vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli takwimu hapa zinaonesha kwenye ukuaji wa uchumi wa mwaka 2020/2021, nchi yetu ilikua kwa asilimia 4.9, lakini mpaka Juni, 2022, takwimu zinaonesha kwamba, unakua kwa asilimia 5.2, lakini ugumu wa uchumi huu ukuaji wake ukiangalia uchumi wa dunia utauona unasinyaa. Uchumi wa dunia una-deteriorate na wote tunajua sababu kubwa ya msingi hapa ni Covid-19, lakini pia kabla hatuja-recover, dunia haija-recover kutoka kwenye hii pandemic effects hizi, tukaja tukaingia hii vita ya Ukraine. Kwa hiyo, sasa imekuja imechanganya economic destruction hii vita ya Ukraine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii imejionesha pia huko duniani ambako kuna high inflation rate ambayo imefikia mpaka double digit, lakini sisi tumeweza ku-control bado tuna single digit mpaka sasa hivi. Mpaka sasa hivi tuko kwenye four point something, lakini wenzetu duniani huko labda tuchukulie mfano European Union, kwa nini nasema tunafanya vizuri?

Mheshimiwa Mwenyekiti, European Union, inflation rate yake kuna nchi pale zimefikia mpaka asilimia 25.5 na nchi ya chini kabisa ambayo inafanya vizuri, Ufaransa, iko 6.2 inflation yake. Data zilizokuwa revealed na Eurostat zinasema kwamba, kwa wale giants kwa mfano, Netherlands wana 13.7 ya inflation, Greece wana 11.2, Belgium 10.5, Spain 10.5, Denmark 9.0, Cyprus 9.0, Sweden 9.5. Kwa hiyo, hawa wote hawa ndio ambao wanatuchangia na sisi pia katika miradi mbalimbali, lakini wana high inflation rate, sisi tumeweza ku-control, bado tuko kwenye chini ya tano. Sasa ni lazima tujipongeze katika hili, tusikate tamaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawapongeza sana Mheshimiwa Rais na wasaidizi wake katika eneo hili, lakini sisi sio kisiwa, duniani projections zinaonesha kwamba, ukuaji wa uchumi utashuka kutoka kwenye 6.1 mpaka 3.2. Kwa hiyo, sisi sio kisiwa, ni part ya dunia. Kama ilivyojionesha huko kwa wenzetu ulaya, European Union, inflation ilivyokuwa juu sasa bado sisi tuendelee kuhakikisha kwamba, Mpango wetu huu tujiwekeze sana katika kuhimili hali ya mtetereko wa uchumi duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirudie; Mpango huu tujielekeze sana kwenye uhimili wa hali ya mtetereko wa uchumi duniani kwa sababu, tunapoelekea tumeambiwa pia, takwimu zinatwambia kwamba, tutakapofika half ya pili ya bajeti hii hali ya uchumi itashuka, ukuaji wa uchumi hapa kwetu nchini. Sasa tuwe na mpango wa kuhakikisha sekta za uzalishaji, kilimo, mifugo, uvuvi, nishati, biashara zinakuwa na tunaziwezesha na kusimamia utekelezaji wake na masoko yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia lazima tumalizie miradi yetu ya kimkakati, reli SGR tuimalizie, umeme vijijini tumalizie ili wananchi wetu waweze ku-add value mazao yao, lakini LNG, mradi ya gesi lazima tuhakikishe unajengwa na unakamilika, lakini miradi ya gesi ambayo ile ya kuzalisha umeme tuhakikishe kama ilivyopangwa katika bajeti hii nayo pia inakamilika, lakini Bwawa la Mwalimu Nyerere tulisimamie kwa karibu sana ili liweze kukamilika. Hii itasaidia uchumi wa jumla kukua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu hawa nimeonesha mfano wa data hapa, wa Eurostat data, inaonesha European Union nchi ambayo uchumi wake, high inflation rate yake iko chini Ufaransa, wao waliwekeza sana kwenye energy. Waliwekeza kwenye energy kupitia hii nuclear, sasa hivi wao wameshindwa kubabaika, hawajababaika kabisa na hili tatizo lililokuwepo la Russia kukata au kupunguza umeme na gesi katika Nchi za Ulaya ambalo limesababisha high inflation rate. Hii ni kwa sababu, wao walikazana na wakawekeza kule. Sasa sisi tukazane tukamilishe hii miradi mikubwa ya kimkakati ili uchumi wetu usibabaike. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, pia hali ya uchumi ya dunia inavyokwenda itatuathiri na sisi uchumi wetu katika nusu ya pili, naomba sana ili isituathiri sana tuwekeze kwenye kilimo. Leo kwenye kilimo Serikali iliwekeza bilioni 150 za ruzuku, lakini katika utekelezaji wake huu unasuasua practically kwa maana kwamba, Serikali imetuambia mpaka leo hii, leo asubuhi imetuambia itatufikishia mpaka kwenye makao makuu ya wilaya au tarafa, hautasambazwa vijijini. Kilichonishangaza ni kusikia kwamba, halmashauri ndio zisambaze Serikali itazipa mafuta. Halmashauri hizi zinatoa wapi magari?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii mkulima kwangu tarafa ya mwisho iko kilometa 220, kata ya mwisho iko kilometa 254. Mkulima kuifuata mbolea huko iliko kilometa 254 inabidi asafiri kwa gharama ya 40,000/= kwenda na kurudi, alale hapo, anunue mbolea, asafirishe na mbolea aipeleke kule, gharama inazidi. Kwa hiyo, ushauri wangu, lazima Serikali watafakari upya au watuachie kule wilayani, Mwenyekiti wa Kamati ya Pembejeo Mkuu wa Wilaya asimamie, basi wawaachie wafanyabiashara wa maeneo yale wasafirishe kwa gharama ambayo atailipia mkulima isizidi hata 5,000/=. Nawaomba sana wafanyabiashara tuwaachie kuliko sisi leo tuwaambie halmashauri tutawapa mafuta, magari watatoa wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwaachie wafanyabiashara waifanye kazi hii. Mkulima yuko tayari kuongeza hata shilingi 5,000 kwa ajili ya usafiri ili mbolea imfikie pale. Serikali tunafanya kazi nzuri sana, tumempunguzia nusu, mwaka jana tulikuwa tunanunua mbolea shilingi 130,000, leo tunanunua shilingi 60,000 mkulima sidhani kama atashindwa kulipia shilingi 5,000kwa ajili ya usafiri. Naomba Serikali walitafakari sana na msimu ndio huu hapa, wakati umeshafika wa maandalizi ya kilimo, watu wanababaika wanasafiri, wanapambana, wanalala siku tatu, siku nne, kutafuta mbolea, mnyonge wa kawaida anayeishi Magazini au anayeishi Lingusanguse, anayeishi Msisima kuja kufuata mbolea Namtumbo, kilometa 284, hawezi, kwa hiyo, ni lazima tusaidie hili. (Makofi)

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

T A A R I F A

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpa Taarifa Mheshimiwa Vita Kawawa. Jambo la Nkansi na arrangement ya Nkansi ni maamuzi na ushauri uliotoka kwenye Halmashauri ya Nkansi. Haina maana kwamba, modality tunayoifanya Nkansi ni uniform kwa nchi nzima, hilo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nimesema kwamba, Waheshimiwa Wabunge na Viongozi wa Wilaya, maeneo ambayo wanashauri kufunguliwe vituo sisi kama Wizara tuko tayari ku-facilitate kwa sababu, tunatumia taasisi zetu mbili maeneo ambayo wafanyabiashara hawaoni faida ya kwenda. Sisi kama Serikali tunatumia TFC na Bodi ya Mazao Mchanganyiko kwa ajili ya kufikisha mbolea katika maeneo hayo, ili wakulima waweze kununua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, modal ya tatu ambayo tunaifanya kama Wilaya ya Rorya, Halmashauri inakusanya mahitaji yote ya vijiji vyake halafu tunachagua kampuni inayopeleka katika eneo lile kutokana na orodha ya wakulima. Kwa hiyo, kila eneo lina jiografia yake, lina tabia yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho. Hatuzuwii wakulima kuchangia gharama ya kusafirisha pale ambapo wao wenyewe wanaamua. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Kawawa na muda wako umekwisha. (Makofi)

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kawawa, muda wako umekwisha.

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)