Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia jioni hii katika Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka 2023/2024. Niseme tu, kabla sijaendelea nilitamani nitumie nafasi hii kuweza kumpongeza Mheshimiwa Rais, Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuweka ruzuku katika mbolea. Ambako tunaona wakulima wengi sasa hivi wana amani. Pia, niweze kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Waziri Kindamba kwa namna ambavyo amekuwa akiendelea kupambana na wahujumu mbolea ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeweza kuona kwenye mitandao kwamba kule Mkoani Songwe kulikuwa na wahujumu uchumi kupitia mbolea, waliokuwa wanatoa mbolea Tanzania kwenda Malawi. Kwa hiyo sasa hivi imebadilika, kwamba mbolea badala ya kutoka Malawi kuja Tanzania sasa hivi inatoka Tanzania Kwenda Malawi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nilitaka nijielekeza kwenye kuchangia katika mapendekezo haya ya huu mpango. Kimsingi nitajikita katika maeneo matatu ambayo ni vipaumbele vya mpango huu. Eneo la kwanza, nitaanzia kwenye kuchochea uchumi shindani na shirikishi, ambapo hapa kuna masuala ya usafirishaji, umeme na TEHAMA. Tunafahamu kwamba barabara ya TANZAM imekuwa ni barabara muhimu sana, na barabara hii ndiyo inayosafirisha mizigo mingi kuelekea Nchi za Ukanda wa SADC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuwa nikiongea hapa mara nyingi, lakini kwa awamu hii ninatamani kuomba Wizara ya Fedha iweze kuweka kipaumbele ujenzi wa barabara hususan kwenye eneo la Mlowo-Tunduma. Kama vile walivyotia kipaumbele kwa eneo la Mbeya waweke kwa Tunduma kwa sababu barabara ile inapata jam kubwa sana. Mawaziri ni mashahidi, wamepita kule na wameona, kwamba hali ya pale si nzuri, mizigo mingi inashindwa kufika kwa wakati katika destiny pale mpakani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia, nilishaongelea kwamba barabara ile kutoka Mlo kwenda Tunduma hakuna barabara ya mchepuko ambayo kama barabara hii ikapata tatizo lolote kutakuwa na njia mbadala ya kuweza kufika mpakani. Kwa hiyo, niombe kupitia bajeti hii, waweze kuitazama barabara hii kama ilivyo muhimu. Kama wanavyowekeza kwa upande wa Dar es Salaam wangewekeza Tunduma nadhani tungepunguza changamoto nyingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningependa kuongelea na kuipongeza Kamati ambao wameweza kuona umuhimu wa kuendelea na mchakato wa hii Sheria ya TAZARA. Nilikuwa natamani kusisitiza pia wafanye haraka iwezekanavyo ili kuboresha hii sheria ili uwekezaji katika TAZARA uendelee na hivyo uweze kuleta tija katika usafirishaji wa mizigo inayoenda huu Ukanda wa SADC. Kwa hiyo, kwa hili niombe pia kwenye bajeti ijayo waipe kipaumbele TAZARA ili iweze kufanya kazi yake kama ambavyo ilikuwa imetarajiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kitu ambacho kimekuwepo, na sijajua ni kwa namna gani huu Mpaka wa Tunduma haujapewa kipaumbele. Kama uwekezaji unavyofanyika Dar es Salaam wangeweza kufanya uwekezaji huu Tunduma mimi nina uhakika nchi hii ingeongeza mapato kwa kiwango kikubwa sana. Tunafahamu mizigo mingi inayotoka Dar es Salaam kwa asilimia 70 inapita kuelekea Ukanda wa SADC. Kama tungepajenga Tunduma tukaweka masoko ya Kimataifa pale, tukajenga dry port pale tunaamini kabisa mapato ya nchi hii yangeongezeka; na hata kwenye nchi hizo za Ukanda wa SADC wale wenye mitaji midogo wangeweza kulifikia Soko la Tanzania na kwa namna hiyo tungeweza kupata mapato kutoka kwenye hizo nchi za upande wa SADC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe Wizara kupitia bajeti hii tunayoielekea, huu mpango wa kuelekea bajeti hii inayokuja, wafanye, ikiwezekana, utafiti kwa Mji wa Tunduma, waangalie ni fursa gani zipo ambazo wanaweza wakazifanya kuhakikisha tunatengeneza fursa za kimapato kwa nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tunafahamu pia huu Mpaka wa Tunduma ndio Mpaka wenye changamoto za magendo mengi sana. Magendo mengi yanaenda, bidhaa zinakuwa kama zinaenda Zambia, kama zinaenda Kongo lakini zinapiga u-turn, zikifika Tunduma zikaenda Zambia zinarudi tena Tanzania. Na huu udhibiti wa magendo katika ule mpaka ni kitu ambacho Wizara inatakiwa ikichukulie kwa namna ya kipekee sana. Pale pia kuna deficit ya watumishi, lakini pia mikakati madhubiti ya kuhakikisha kwamba mazingira ya udhibiti wa magendo yanawekwa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi si mtaalam wa mambo ya kodi na wala si mtaalamu wa mambo ya udhibiti wa magendo; lakini magendo nayaona yakitoka Zambia yakirudi Tanzania. Kwa hiyo tunafahamu kabisa nchi zile tunazopakana nazo wao wana mazingira ambayo yanawashawishi wafanyabiashara wa Tanzania wakawekeze na kusajiri kampuni kule ili wanapokuwa wanapeleka mizigo kule, inapiga u-turn ionekana kama ilikuwa imeenda Zambia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hilo, niombe sana watumishi pale mpakani waongezwe. Nadhani hii kwenye upande wa mapato ya nchi tutakuwa tunaisaidia nchi kuweza kupata fedha nyingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ambacho nilitamani kuongelea kwa upande wa Tunduma; ni kwamba tumekuwa tunaona kabisa kuna masoko mbali mbali ambayo yanaendelea kujengwa. Kuna Soko la Kakozi ambalo unaona kabisa ni soko la Kimatifa na ni soko zuri. Hata hivyo bado halijakamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi niseme tu, Wizara ije na mkakati kabambe au maalum kwa ajili ya ile zone ya Tunduma na Momba kwa ujumla. Nadhani kuna kitu ambacho tutafanya additional katika mapato ya nchi hii. Nitakuwa sijajitendea haki kama sintoongelea hiki kipengele cha kuchochea maendeleo ya watu, kumarisha afya, maji, elimu, upimaji wa ardhi na kuimarisha huduma za maendeleo ya jamii na makundi maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuongelea hiki kipengele kwa sababu ni kipengele ambacho huwa kinanigusa sana, hususan ukiangalia na changamoto ambazo zimekuwa zikiendelea. Kama vile ongezeko la magonjwa ya afya ya akili, vifo vya watu kujiua au kuua. Nilitamani kwamba kwenye hiki kipaumbele ambacho kimeandikwa kuchochea maendeleo ya watu kuimarisha afya, maji nakadhalika, hapa kwenye maendeleo ya jamii na makundi maalum, hii makundi maalum ingetamka ustawi wa jamii. Kwa sababu tunafahamu hii Wizara ina kada mbili tu, ina maendeleo ya jamii ina ustawi wa jamii. Ustawi wa jamii ndicho kitu kinachobeba makundi yote haya maalum mengine. Kama kweli nchi inataka kupiga hatua kwenye maendeleo ya watu tuanatakiwa ku-invest kwenye eneo la ustawi wa jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ni nyingi, kada hii ina wataalamu wengi wazuri. Nitumie forum hii pia kumshukuru Rais ameajiri Maafisa Ustawi wa Jamii 139. Tunafahamu mahitaji halisi kwa mwaka uliopita kwenye bajeti iliyopita tulikuwa tunaona ni asilimia 97 ya upungufu wa Maafisa Ustawi wa Jamii kwenye maeneo yetu. Hawa ndio watu ambao wanaweza waka-stabilize hali halisi ya kisaikolojia ya wananchi wetu ili waweze kufanya vizuri kwenye uchumi, katika mambo mengine ya kielimu na masuala mengine ya kijamii. Hata kupambana na hivyo vikundi vya mikopo na nini, huwezi ukapambana na kuchukua fedha huku akili yako kisaikolojia haiku vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninaomba Wizara hapa, wanaposema maendeleo ya jamii na makundi maalum, ile makundi maalum iondoke na badala yake waweke ustawi wa jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kitu kingine pia nilitamani kuomba kwenye mpango wa bajeti unaokuja suala la maji, kama walivyotuahidi kwa mji wa Tunduma, tunajua changamoto ya mji wa Tunduma. Ninaitaja sana Tunduma kwa sababu ni mji ambao ni mpakani na ndiyo wageni wengi wa nchi zingine wanapokuja wanafikia Tunduma kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna maji pale na kuna mradi ambao tumeahidiwa wa almost bilioni 17 basi watusaidie uweze kuisha haraka ili hata watu wanapokuja kuwekeza Tunduma wawe na uhakika wa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nashukuru sana. (Makofi)