Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa hii nafasi ya kuchangia katika Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ukiangalia leo changamoto ya uchumi tuliyonayo pengine tusingekuwa tumefikia kwa kiwango hiki kama tungeweza kuwa tumewekeza vya kutosha katika sekta mbalimbali ambazo ni dhahiri zingeweza kuleta matunda.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaongelea sekta ya mifugo nikiendeleza alikomalizia mwenzangu mama Kaboyoka. Mama Kaboyoka ameongelea takwimu zinaonyesha kwamba idadi ya ng’ombe na mbuzi na kondoo wameongezeka na mimi nitasema kwa mujibu wa takwimu zenu. Mnasema ng’ombe leo tuna takriban milioni 33, tunakuja mbuzi milioni 25 mpaka 28, tunakuja kondoo na vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo inaonyesha kwamba sekta ya mifugo inakua kama takwimu ni za kweli, lakini ukiangalia ukuaji wa sekta ya mifugo unachangiaje kwenye pato la Taifa wamesema mifugo inachangia kwa 7% mpaka 7.4% kwa miaka miwili mfululizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, unaweza ukaona kwamba hicho ni kiwango kidogo ukilinganisha kwamba ni watu wengi wanaweza kushiriki na kujiajiri katika ufugaji. Ufugaji leo tunaouongelea na kwa kiwango kikubwa katika nchi yetu ni ufugaji wa asili, ufugaji wa asili ambao ungeweza kama ukiwekezwa vizuri kama alivyoeleza mama yangu unaweza ukaleta tija katika nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo sisi Tanzania ni wa pili katika mifugo nyuma ya Ethiopia na mmejinasibu kwa takwimu kwamba leo tunaweza kusindika tunapeleka mpaka Uarabuni na maeneo mengine. Hata hivyo, bado hatujafanya vizuri, nguvu kubwa tumeiwekeza kwenye maziwa lakini na bidhaa ya ng’ombe, tumesahau maziwa na nyama. Tumesahau kwamba bado kuna asset kubwa ambayo inatoka kwenye ngozi.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo kila mtu anaenda kununua kitu dukani kama ni bag, kama ni kiatu, kama ni hand bag chochote atatamani kiwe cha ngozi na ataanza kuangalia quality ya ngozi kumbe kuna fursa kubwa sana kwenye ngozi kama tukiwekeza vizuri. Nimepitia takwimu nimeona tunaeleza kwamba tukiwa na mifugo zaidi ya milioni 33 kwa takwimu za mwaka huu zinaonyesha mmeweza kupata piece za ngozi zaidi ya milioni 13. Katika piece zaidi milioni 13 hizo piece zimeweza kuleta zaidi au zikiuzwa zinaweza kuleta zaidi ya bilioni 28. Kwa mwaka uliopita ziko piece milioni 11, lakini katika piece za ngozi milioni 11 inaonekana zilikuwa zimeshauzwa zaidi au chini ya milioni 1.5. Kwa hiyo unaweza ukaona kwamba ngozi ambayo inakusanywa haiuziki na hapo ndiyo nataka nieleze vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sera ya mifugo ya 2006 inaongelea nini kuhusu bidhaa za ngozi? Bidhaa za ngozi duniani na nchi ikishafahamika inatoa ngozi nzuri automatic tutapata bei nzuri. Nchi kama Ethiopia leo nimesoma mnaonyesha kwamba mnauza ngozi Ethiopia lakini kwa nini mnauza ngozi Ethiopia kwa sababu sisi hatuna repetition ya ku-trade ngozi duniani. Repetition ya ngozi yetu ni duni na kwa sababu wanajua ni duni na uduni huo umetokana na kufuga vibaya. Kuna mtu amefanya research anaitwa Mahmood na wenzake, ameeleza kwamba zaidi ya asilimia 60 ya ngozi inaharibikia kwenye machinjio, kwamba ng’ombe anaweza akawa ametunzwa vizuri despite challenges lakini wanavyoingia kwenye machinjio zaidi ya asilimia 60 ya ngozi inakuwa imeharibika. Akaenda mbali zaidi akasema kwa nyama inayokuwa consumed Tanzania ni 10% tu ya nyama ambazo zinachinjwa katika mabucha sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ngozi leo zipo tans and tans na nimesoma taarifa ya wafanyabiashara wanasema wana tani zaidi ya 3,000 tans zipo zimekosa soko kwa sababu hazina ubora na hivyo nitaongelea specific sera ambayo inaendelea leo mtaani kwamba tuweze kuweka alama ng’ombe, Serikali inabandika alama kwenye ng’ombe kwa kutumia hata traditional method ile ngozi inabandikwa na pasi ngozi inaunguzwa kwa hiyo inapoteza value. Kwa hiyo tunarudi kwa Mahmood alivyosema kwamba 60% ya ngozi inaharibikia kwenye mabucha mbali na sababu nyingine yoyote.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikasoma taarifa ya Wizara inasema kwamba, wameweza kupeleka visu 100 nadhani something like 116 kwenye mabucha maalum, hivi visu vya uchinjaji 116 vinasaidiaje katika ng’ombe au mabucha au wazalishaji wa nyama katika nchi hii. Which means hatujawekeza vya kutosha na hatuwezi kupata faida ya ngozi ambayo kwa kiwango kikubwa ngozi ndiyo bidhaa nzuri duniani. Wafugaji wanaendelea, viwanda au wawekezaji wa kwenye industry ya lather nchini wanalalamika, mazingira mabovu ya uwekezaji, wanalalamika kukosa incentive, wanalalamikia pia ubovu wa ngozi ambayo tunazalisha nchini. Hapa anaendelea ku-capitalize kwamba ni lazima sera ieleze bayana ni kwa kiwango gani tunaenda kupunguza ubovu wa ngozi inayopatikana ili tuweze kupata fedha za kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, tutajinasibu kwamba tuna ng’ombe wengi tunajinasibu tunazalisha nyama ya kutosha, lakini hebu tu-focus kwenye ngozi pia. Kama tukifanya vizuri kwenye finished product za ngozi na siyo tu viwanda tulivyonavyo leo by the way tulikuwa na viwanda mpaka 11, leo tuna viwanda kama vitatu au vine, lakini siyo tu kwamba vinazalisha finished goods bali vinakuwa na vyenyewe ni kama vina export raw material, vinachakata kidogo halafu vinaenda kuuza kwenye nchi za wenzetu pamoja na Burundi. Hivi leo Burundi ni wa kununua ngozi Tanzania? Leo Burundi ndiyo wanapaswa kuonekana wanazalisha ngozi nafuu ukilinganisha na Tanzania? I think something is wrong somewhere na hiyo ndiyo nataka Ofisi ya Waziri Mkuu itueleze ni mkakati gani mahsusi uliopo kupunguza ubovu wa ngozi ambayo imekuwa ikizalishwa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hiyo tu, tunataka tuambie hiyo sera leo tuliyonayo ya mifugo ya 2006, ni lini itakuwa reviewed ili iendane na wakati nimejipa homework, nikasoma sea ya mifugo ya Kenya, nikasoma sera ya mifugo ya Ethiopia, nikaone wenzetu so far wanajua wanachokifanya kwenye industry. Nadhani Ofisi ya Waziri Mkuu ni wakati umefika tuweze ku-review tuone tunaweza kufanya vizuri kwa kiwango gani zaidi kwenye soko la ngozi duniani.

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hiyo tu ambayo naweza nikaeleza bidhaa za ngozi ambayo nimekuwa nikizieleza au nimekuwa nikieleza hapa ikikabiliwa na changamoto ya kuwa mbovu bado pia kuna ujanja ujanja hapa katikati, kwamba wanaodili na bidhaa za ngozi wanakuwa na madalali ambao wanalalia hata wao wenyewe wafanyabiashara wanaonunua ngozi, which means tumetengeneza middle men hapa katikati. Wafanyabiashara wa ngozi au wa viwanda vya ngozi wamesema kwamba ngozi yenyewe inayozalishwa ngozi nzima ni chini ya 15% ambayo ni first grade na second grade.

Kwa hiyo, naomba nitoe wito kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inasimamia sera itusaidie kama ambavyo nguvu kubwa inaelekezwa kwenye maziwa na nyama, tuone mabadiliko kwenye ngozi pia, ndiyo tutaweza kupata tulichokuwa tunataraji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kuongelea changamoto leo ambayo tunapitia ya kupanda kwa bei ya mafuta. Kupanda kwa bei ya mafuta ya petrol na mafuta ya kula yatakuwa na impact kwenye uchumi baadaye…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.