Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa kunipa nafasi kwa siku ya leo tena ili niweze kuchangia kwenye hotuba ya Waziri Mkuu. Nimeisoma hotuba ya Waziri Mkuu Mpango wa Bajeti mwaka, 2022/2023 kweli imekaa vizuri sana. Hivyo sasa, nitumie nafasi hii tu kumuombea kwa Mwenyezi Mungu Mheshimiwa Waziri Mkuu, kama alivyokusudia kwenye malengo yake aweze kutufanyia kazi Watanzania.

Nimeangalia katika ukurasa wa 22 amezungumzia Mahakama ambazo zinakwenda kujengwa katika Taifa letu, ikiwemo na Wilaya yangu ya Mbogwe. Kweli nauunga mkono huu Mpango kwa asilimia mia moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kukupongeza wewe kwa kuchaguliwa kuwa Spika wetu wa Bunge Tukufu pamoja na Baraza la Mawaziri wapya pamoja na Manaibu wale waliochaguliwa kwa mwaka huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niombe sasa kutoa mchango wangu kuiomba Serikali, wajaribu kuzingatia hao Mawaziri waliochaguliwa kufuatilia zile kumbukumbu. Wale Mawaziri waliokuwepo kwamba, kuna ahadi ambazo walizitoa kwenye Majimbo yetu kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wetu. Vile vile, niombe kuwasilisha mawazo ya wengi wananchi wangu wa Jimbo la Mbogwe wananipenda sana na wamenituma kuja kuyasema mahali hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kweli yapo mengi yanazungumzwa na hayana budi kuyakwepa kuyazungumza mahali hapa, maana sisi ndio washauri wa Serikali. Ugumu wa maisha unaongoza sasa hivi mitaani na ugumu huu wa maisha kiukweli kama alivyotangulia kusema Mheshimiwa Iddi hapa, unachangiwa na issue ya mafuta.

Mheshimiwa Spika, naomba ku-declare interest tu kwamba mimi ni muuza mafuta japokuwa alitaka kuliweka vibaya sana lakini wewe ukalinyoosha vizuri, kwamba, asitunyime kutoa mawazo yetu japokuwa kwamba sisi ni wadau wa sekta hizo, tuishauri vizuri tu Serikali ili kusudi kila mmoja aweze kufaidika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini, tumekuwa tukishauri hata kwenye Kamati, kwamba, vipo vyombo vya Serikali ambayo vinachangia kumuumiza mwananchi. Ukiangalia EWURA ina masharti mengi sana na tumeshashauri huko kwamba, wabadilishe miongozo ili watu waweze kufungua vituo vya mafuta vijijini. Leo kwenye Jimbo langu kuna baadhi ya sehemu mafuta yanauzwa mpaka Sh.5,000/= kwa lita moja sio Sh.3,000/= peke yake. Sh.3,000/= ni kwa wale walio na vituo vya mafuta, lakini yakiingia kwenye makopo kwa wananchi walio wengi ambako hakuna huduma za petrol station wanauza wanavyotaka wananchi hao. Kwa hiyo, kuna kila sababu tuiombe Serikali iliangalie upya na ilete miongozo hiyo haraka sana, tuifanyie mabadiliko, watu waweze kufungua vituo kwenye hayo maeneo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, kwenye upande wa barabara hapa, wananchi wanatamani sana kuona barabara zinatengenezwa kila mahali. Jimbo langu la Mbogwe ni kubwa lina kata 17 na kila kata ina barabara za msingi, zinaingiza pato la Taifa pamoja na pato la halmashauri. Jimbo langu linahitaji kuongezewa bajeti ya TARURA ili kusudi Meneja wangu wa TARURA, aweze kurekebisha barabara zinazotakiwa kurekebishwa kwenye hiyo Wilaya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu, wananchi wanahitaji kuona umeme unatengenezwa kwenye maeneo yao. Vipo vijiji ambavyo bado havijawekewa umeme na tumekuwa tukiongea kila wakati humu Bungeni kwamba umeme sasa hii awamu iende kukamilika.

Mheshimiwa Spika, jambo la nne, wananchi wanahitaji kuona maji kwenye maeneo yao. Wananchi kiukweli hawana mambo mengi sana pamoja na kwamba, mipango ni mingi sana ya Serikali, lakini naishauri Serikali iangalie vitu vya msingi tu vichache, vitatu ama vitano ili kuweza kuwasaidia wananchi wetu waliotuweka madarakani. Kwa sasa kwa kweli hali ni ngumu sana, uchaguzi ungekuwa ni kesho au keshokutwa, tulikuwa na asilimia chache sana ya kurudi humu Bungeni maana hali ni mbaya. Ukiangalia wananchi kiukweli mtu wa kwanza wanayemlalamikia ni Mbunge na wanatufuatilia sana na wanatuangalia kwamba, Mbunge wetu anaishauri nini Serikali.

Mheshimiwa Spika, jambo la Nne wananchi wanahitaji kuona maji kwenye maeneo yao. Wananchi kiukweli hawana mambo mengi sana pamoja na kwamba mipango ni mingi sana ya Serikali, lakini ninaishauri Serikali iangalie vitu vya msingi tu vichache, vitano ama vitatu ili kuweza kuwasaidia wananchi wetu waliotuweka madarakani.

Mheshimiwa Spika, kwa hali ilivyo sasa kwa kweli hali ni ngumu sana, uchaguzi ungekuwa ni kesho au keshokutwa tulikuwa na asilimia chache sana ya kurudi humu Bungeni maana hali ni mbaya. Ukiangalia wananchi kiukweli wanamlalamikia mtu wa kwanza ni Mbunge na wanatufuatilia sana wanatuangalia kwamba, Mbunge wetu anaishauri nini Serikali.

Mheshimiwa Spika, mimi nitumie nafasi hii kuishauri Serikali ione namna gani mwananchi anaenda kumpunguziwa ugumu wa maisha. Tukiangalia mfano Serikali ya Awamu ya Kwanza, Awamu ya Pili, Awamu ya Tatu na Awamu ya Nne tulikuwa tuna vyanzo vingi, hapakuwa na tozo lakini maisha yalienda. Hapakuwa na tozo kwenye mafuta na kwenye miamala, lakini watu waliishi kwa raha mustarehe, leo hii tuna ndege, tuna meli kwenye maziwa yetu huko pamoja na bahari yanaingiza kwenye Pato la Taifa.

Kwa hiyo, niiombe Serikali sasa ikae ifikirie wananchi hawa kulingana na kilio kwa vile ngoma ikilia sana hupasuka, maana kilio ni kikubwa sana. Kila kijiwe ukikaa unakuta watu wanaliongelea hilo tu kwamba maisha yamepanda sana, maisha yamekuwa magumu sana, nauli imeongezeka kutoka shilingi 1,000 mpaka shilingi 5,000 ukiingia kwenye huko kwenye Wilaya zetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niiombe Serikali ilione hilo kama jambo la msingi sana ili kuwasaidia wananchi hawa waweze kuishi maisha mazuri.

Mheshimiwa Spika, jambo jingine hapa ninaiomba Serikali kwenye Wilaya yangu sina chuo cha VETA. Na ukisoma kwenye ilani ya Chama chetu cha Mapinduzi tuliinadi kwamba, kila Wilaya itakuwa na Chuo cha VETA. Niiombe Serikali sasa ione namna iweze kunisaidia kwenye Jimbo langu kupata chuo cha VETA.

Mheshimiwa Spika, pia jambo linguine ni taa za barabarani. Kwenye kampeni tulikuwa tukinadi kila patakapojengwa lami kutakuwa na taa za barabarani. Kwangu sina taa za barabarani na Mji wangu unakua kwa kasi sana wa Mbogwe na Masumbwe. Kwa hiyo, niiombe Wizara inayohusika na haya mambo waweze kunisaidia wananchi wangu wapate umeme na waondoke gizani ili waweze kunufaika na utawala huu tulionao wa Awamu ya Sita.

Mheshimiwa Spika, jambo jingine, nikuombe wewe uendelee kutulinda tu sisi ni vijana wako ni wageni humu ndani. Twaweza kuwa tunakukosea kweli, maana hatukusoma chuo kuja kuwakilisha watu humu, kila mtu na lafudhi yake. Kwa mfano, mimi lafudhi yangu inaeleweka ninaweza nikawa ninazungumza kama kwa ukali sana, lakini kumbe ndivyo nilivyo tu. Ninaomba kwa unyenyekevu mkubwa niweze kusikilizwa na niweze kusaidiwa vizuri sana pale ninapochangia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie kwenye hotuba hii ya Waziri Mkuu, ukurasa wa 36, amezungumzia issue ya pato la madini. Niiombe Serikali sasa iangalie haya mapato yanayokusanywa kwa wingi kuna sehemu Serikali haiwezeshi. Wachimbaji hawa wadogo hakuna fungu ambalo limetoka Serikali Kuu kama zinavyofanya sekta nyingine.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia kilimo wanatoa matrekta, wanakopesha matrekta, lakini wachimbaji wadogo ambao hatujawasaidia hawa na wanafanya vizuri ni vyema wakatengenezewa miundombinu angalau ya barabara kwenye migodi yao.

Mheshimiwa Spika, ipo migodi inayozalisha kila siku, lakini haina miundombinu ya barabara, hakuna vituo vya afya kwenye maeneo yale. Dada pale amezungumza UKIMWI unaenea kwa kasi kubwa sana Kanda ya Ziwa, ni kweli watu wanaishi kwa shida, lakini ukiangalia tozo ambazo zinakusanywa ni nyingi na suala hili tumeshalishauri kwenye Kamati. Ninakuomba tu Mheshimiwa Waziri Kaka yangu na umekuwa Waziri wa mfano wa kwanza, maana katika makusanyo nimeangalia kabrasha huko Mawaziri waliopita hakuna Waziri ambaye amewahi kukusanya Bilioni 528 kama mwaka jana, sasa hivi imefika Shilingi Bilioni 400.6 ina maana unaonesha jinsi gani ulivyo mwaminifu Kaka yangu, hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikuombe kwa vile wewe unakaa na Rais mwambie kabisa ukweli kuanzia wewe mwenyewe unatokea sehemu za machimbo, una mgodi wa namba moja, namba saba, hakuna miundombinu ya kutosha kwenye maeneo yale, lakini wananchi hawa ni waaminifu wanaingiza pato la hatari kwenye Taifa, aone fungu ili kusudi aweze kutusaidia wachimbaji wetu wapate manufaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mchango wangu leo naomba nikomee hapo ili Serikali sasa iweze kutusaidia tuweze kuishi maisha mazuri na yenye raha. Ahsante sana. (Makofi)