Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Abdallah Saleh Possi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (WATU WENYE ULEMEVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda nitakwenda haraka haraka. Kwanza, moja kwa moja niseme tu kwamba naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri. Ninachokisema hapa ni kuboresha tu kwa sababu nafahamu kazi waliyokuwa nayo na yapo mengine tutaendelea kuwasiliana vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja katika kuboresha huko, yameongelewa hapa kuhusu masuala ya accessibility ya facilities kwa watu wenye ulemavu. Sitayarudia aliyosema Mheshimiwa Mama Macha na wengine ila nitaboresha tu kwamba ni vizuri sasa pia kuangalia ni namna gani tunaboresha teknolojia kwa ajili ya wale watu wenye uhitaji wa viungo bandia. Nasema haya nikifikiria idadi kubwa ya watu ambao walikatwa viungo vyao, watu wenye Ualbino ambao watakuwa wakihitaji kuwa productive na nimeona ugumu au ughali wa masuala haya ya vifaa bandia. Kwa hiyo, in future for purpose ya kuboresha, ni vizuri tuangalie hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine la pili ambalo nataka kuliweka sawa ni suala la NHIF. Ni utaratibu wa bima yoyote ile duniani kuwa na exemptions; haiwezi ika-cover vitu vyote lakini sasa tuangalie zile life saving instruments; vitu kama pace makers na vingine kwa sababu ni very expensive lakini visipokuwa covered hivi, maana yake kuna watu wanaweza wakapoteza maisha na purpose ya bima ni ku-save life.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ambalo pia ni muhimu sana, najua tumefanya mawasiliano lakini nasema hivi kwa kukumbusha zaidi; ni kwamba kuhusiana na mafuta maalum ambayo yanawakinga watu wa Ualbino kuepukana na skin cancer ni very cheap na bahati nzuri yameanza kutengenezwa hapa katika PPP, kwa hiyo, suala ni kuhakikisha kwamba kuna utaratibu maalum wa MSD kuhakikisha inayanunua mafuta haya na Halmashauri zetu kuyasambaza mafuta haya. Hili likifanyika, ina maana rate ya skin cancer itakuwa imepungua sana na kwa maana hiyo, zile gharama za watu kwenda Ocean Road hazitopatikana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lastly, of course nimeshawasiliana na baadhi ya watu, lakini kutokana na muda sitaweza sana, naomba tu tuwe tuna mawasiliano ya mara kwa mara ili kuona ni namna gani early cancer prevention treatment inaweza ikafanyika kwa kutumia gesi ya nitrogen ambayo kwa sasa inatumika hasa kwa upande wa wanyama. Ila technology inaonesha kwamba hii inaweza ikazuia sana skin cancer na wapo watu ambao wanafanya hivi, wanawatumia Madaktari wetu wa Kitanzania, suala ni kuangalia namna gani tuna- sustainable policy, ili wale wafadhili wakiondoka, basi wataalam wetu waendelee kulifanya hili kama ni jambo endelevu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ulikuwa ni mchango wangu, naomba kuunga mkono hoja.