Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kutofuata Maelekezo ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kutofuata Maelekezo ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwa mtazamo wangu tunapokutana na changamoto, kwanza nianze na kukushukuru. Kuna kauli umeitoa hapo kabla, binafsi nimeona ni kauli ya kiuongozi. Jambo hili tusipolisema hapa ndani ya Bunge tunaweza tukajenga taswira kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita imeingia madarakani, kuna matatizo makubwa, wanafunzi hawapati mikopo, Serikali haitoi fedha, ndiyo notion ambayo imejengeka huko nje. Sasa nataka tuweke mambo vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais Samia toka ameingia madarakani, ameongeza fedha za mikopo ya Elimu ya Juu kutoka Shilingi bilioni 464 mpaka Shilingi bilioni 570, ambalo ni ongezeko la Shilingi bilioni 100 na kitu kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Hilo nataka tuliweke sawasawa. Kwa sababu ilivyozungumzwa itaonekana kwamba, sasa yaani bodi pamekuwa panayumba, kuna myumbo. Namna hii tukifanya tutakuwa hatumtendei haki Mheshimiwa Rais aliyeko madarakani, tutakuwa hatutendei haki Serikali kwa juhudi wanazozifanya kuhakikisha watoto wetu wanapewa mikopo. Hilo lazima tuliweke vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, kiti chako kimetoa maelekezo kwamba tunavyozungumza it is like kwamba hakuna kitu kinafanyika kwenye bodi, jambo ambalo nimeshukuru sana umetoa hayo maelekezo na huo ndiyo msimamo wangu. Kwa sababu takwimu zinaonesha, Mama Samia toka ameingia madarakani, Rais wetu amefanya deliberate decision ya kuongeza fedha kuwasaidia watoto wa Kitanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama kuna changamoto zimejitokeza za kiutendaji, hatuwezi kufumbiana macho hapa. Mimi sifungwi mdomo na mtu, kama kuna changamoto naiona for the interest ya nchi nitasimama hapa kusema ukweli bila kufungwa mdomo na mtu; na ndiyo kazi ya Mbunge na ndiyo jukumu la Kibunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumesikia ripoti hapa, naomba niseme kwa unyenyekevu mkubwa sana. Hii ripoti iliyosomwa hapa na Mwenyekiti wa Kamati, siyo ripoti ya Kamati, hii ni ripoti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa sababu Kamati imepewa majukumu kama wanafanya kwa niaba ya Bunge.

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Yahaya Massare.

T A A R I F A

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, naomba nimpe taarifa mdogo wangu Mheshimiwa Elibariki Kingu. Tunachokizungumza hapa ni kwa maslahi mapana ya wananchi wetu, na mjadala huu unalenga amri yako ambayo uliitoa kwa Serikali. Uliiambia Serikali kuwa watoto wote waende vyuoni wakati tunaandaa taratibu namna gani watapatiwa mikopo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tujadili namna ya kuwasaidia watoto wa masikini, wa wakulima na wafanyakazi wa nchi hii. Mheshimiwa Rais alishatoa fedha. Sasa kama changamoto ni utekelezaji, ndiyo tulizungumze hilo. Nani kakosea; nani kafanya nini; lakini dhamira yetu ituweke wapi? Tuna nia ya kuwasaidia, Mheshimiwa Rais upande wake kashamaliza, sisi kama Bunge tulishatoa na wewe kama Mkuu wa Mhimili huu ulishatoa maelekezo kwamba wanafunzi hawa waende vyuoni.

Mheshimiwa Spika, ili kumaliza changamoto hii, watoto walioko vyuoni hawajalipwa tuition fees, zinatoka wapi? Matarajio yao ni hii Bodi ya Mikopo na Wizara ya Elimu. Ndiyo tujadili hao watu ili namna gani waende kama timu moja. Watoke huku na kule; nani ni nani; na nani ni nani; na afanye nini; kwa kipindi hiki? Tuisaidie nchi hii, tusaidie watu wetu na tusaidie watoto wa wananchi masikini ambao wazazi wao nao wenyewe walipiga kura kwa ajili yetu na tumo ndani ya nyumba hii.

Mheshimiwa Spika, naomba nimpe taarifa mdogo wangu. (Makofi/Kicheko)

SPIKA: Mheshimiwa Elibariki Kingu, malizia mchango wako.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, wewe ni kiongozi mstahimilivu na mvumilivu sana. Ahsante. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilichokuwa nakisema, taarifa hii iliyoletwa katika Bunge lako ni Taarifa ya Bunge kwa sababu Kamati imekasimiwa madaraka na Bunge lako. Hoja yangu ya msingi, hivi kweli Bunge hili lije kuanza kufanya kazi ya kumfundisha Waziri namna ya kufanya communication na watu wake wa Wizarani? it is impossible. Unajua tusichukulie mambo haya kimzaha mzaha, at the end of day tunaharibu hali ya hewa ya siasa nje, tunaona kwamba ni mambo ya kawaida. Bunge hili lianze kumfundisha Waziri namna ya kuwasiliana na watu wa Bodi ya Mikopo? Bunge lianze kumfundisha Waziri umeipa kazi Tume uliyoiunda wewe…

T A A R I F A

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, terms of reference zinatengezwa na mtu mwingine, aliyempa kazi bodi nani ametengeneza terms of reference? Tunaambiwa hapa kwenye ripoti, kama tumeamua kufunika kombe mwanaharamu apite tulifunike, lakini ukweli utabaki Waziri na timu yake wapange mawasiliano vizuri na Wizara, hatutaki kuharibiwa hali ya hewa ya siasa nje. Ahsante. (Makofi)