Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru kwa kunipa nafasi. Vile vile niwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa ushauri na maoni yaliyotolewa kwa ujumla na niishukuru Kamati ya PAC na Kamati ya PIC zote kwenye eneo linalohusu Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Spika, la kwanza nataka kuchangia maoni ya Kamati ya PAC hasa kuhusu issue ya vihenge. Ni kweli kwamba Serikali imekuwa na mkataba na kampuni mbili; Kampuni ya FERRUM na Kampuni ya UNEA, mkataba wenye jumla ya thamani ya Dola milioni 55. Kampuni ya UNEA ilipewa site tatu ambazo zimeshakamilika kwa asilimia 100 na tumeanza kuzitumia. Changamoto iko kwenye mradi unaofanywa na kampuni ya FERRUM, lakini nataka nilihakikishie Bunge lako Tukufu kwamba Serikali imechukua hatua, kwamba Kampuni ya FERRUM ilileta intention ya kutaka kuongezewa fedha zaidi ya Dola milioni 18 over and above the contractual agreement. Serikali ilikataa kutekeleza maombi hayo na mpaka sasa Serikali imeshikilia retention ya Dola milioni tatu.

Mheshimiwa Spika, tunafanya nao mazungumzo, kama hawataweza kutekeleza kutokana na scope iliyopo, tutavunja nao mkataba na tutatafuta mkandarasi mwingine kwa ajili ya kuweza kuendelea na mradi huo. Kwa hiyo, tunalichukulia in a serious note na ninaamini kwamba pamoja na maazimio yatakayofikiwa, tukija next time tutakuta jambo hili limeshaondoka kwenye meza yetu.

Mheshimiwa Spika, la pili lilikuwa ni suala la pamba, ni kweli mwaka 2019 Serikali ilitoa maelekezo kwamba pamba inunuliwe kwa bei ya Shilingi 1,200/= na kulikuwa na clear instruction na mechanism. Serikali ilishalipa hasara ya Shiligi bilioni 14, na mimi mwenyewe Kamati ya Bunge iliniita tukiwa na Waziri wa Fedha, tukakutana na kuongea na Kamati ya PIC na kuwaeleza hatua ambazo tunachukua. Kama Serikali hatua ambayo tutachukua kuliondoa hili jambo la mwaka 2019 ni kwamba tutahakikisha tutakapokwenda kwenye mwaka ujao wa fedha hili eneo tunali-resolve once and for good.

Mheshimiwa Spika, nataka niliombe Bunge lako Tukufu, ni vizuri Waheshimiwa Wabunge, suala la mauzo na manunuzi ya bidhaa sokoni, tukaheshimu soko. Mwaka 2018, 2019 tulichukua hatua ambazo zilitupeleka kwenye hasara kubwa na kutuumiza kama nchi, na leo Kamati ya Bunge na CAG wameweza kuleta mapendekezo haya yaliyotokana na influence iliyotoka ndani ya Bunge.

Mheshimiwa Spika, nashauri huko tunakokwenda turuhusu kuchukua hatua ambazo not more political kwenye masuala ya kibiashara.

(Hpa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa Waziri sekunde thelathini.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, sawa. La mwisho, Waheshimiwa Wabunge wame-comment sana kuhusu suala la kupeleka mbolea za ruzuku. Ni kweli Mheshimiwa Rais amezindua, na mimi nilishukuru Bunge lako Tukufu kwa kuweka effort kwenye eneo la kilimo na kuongeza bajeti na Serikali imeanza kutoa ruzuku. Tumetengeneza mfumo ambao una muda wa siku 60 tu.

Mheshimiwa Spika, zipo changamoto, lakini nawaomba Waheshimiwa Wabunge tuendelee kushirikiana pamoja ili kuhakikisha kwamba tunapeleka huduma hii, wakati huo huo tukimlinda mkulima, na wakati huo huo tusiruhusu kwenda kupeleka ili mfumo huu uende kuwafaidisha watu wachache badala ya wakulima.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.