Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi kwanza kabisa nianze kukupongeza wewe kwa namna ambavyo umeliendesha Bunge hili na kuendelea kuwapa Wabunge nguvu zaidi na kuendelea kuliheshima Bunge, kwa dhati ya moyo wangu ninakupongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mchango wangu kwanza kabisa niseme naunga hoja taarifa zote za Kamati ambazo ziko hapa mezani ambazo ni Kamati ya PAC, LAAC pamoja na PIC ambayo Mimi ni Mjumbe huko. Nitachangia katika maeneo mawili, nitachangia kwenye asilimia Kumi za Halmashauri pamoja na Benki ya Kilimo.

Mheshimiwa Spika, nikianza na asilimia Kumi ya mapato ya Halmashauri naona kabisa nia ya dhati kabisa ya Serikali kwanini waliweka kuwepo na asilimia Kumi hii ya Halmashauri. Lengo kubwa ilikuwa ni kuhakikisha wanampa mwananchi huyu nguvu kumuwezesha katika uchumi wake ikiwa ni sambamba ya kuendelea kumpa madaraka ya yeye kuendelea kujisimamia kama ambavyo Serikali yoyote inapaswa kufanya duniani kote.

Mheshimiwa Spika, kabla sijaendelea na mchango wangu nataka kum-quote kidogo ambaye alishakuwa Rais wa Marekani Thomas Jefferson, anasema hivi, ‘‘The purpose of the Government is to enable the people of a Nation to live in safety and happiness. Government exists for the interests of the governed, not for the Governors’’. Akiwa na maana kwamba Serikali yoyote duniani maslahi yake kwanza ni kuwaridhisha wale ambao wanawatawala na siyo wale ambao watawaliwa. Tafsiri yake, viongozi wote wa Serikali na wasimamizi wote ambao wamepata dhamana cha kwanza kabisa jukumu lao ni kuhakikisha wanalinda maslahi ya wananchi ambayo sisi wao tunawatumikia au kwa lugha nyingine kama ni Serikali ambao tuseme wanawatawala.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo nataka nirejee kwenye Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi, nitasoma mambo kadhaa. Kwenye sura ya Sita ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, ukurasa wa 161 ukienda kwenye ukurasa wa 174 unasema hivi, kwa kutambua umuhimu wa kuendelea kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi katika hali iliyoshirikishi, Chama cha Mapinduzi katika kipindi cha miaka ijayo imetarajia kufanya yafuatayo: -

(i) Kuimarisha mifumo ya taasisi na uwezo wa Viongozi na Watendaji wa Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwenda Vijijini kusikiliza na kushughulikia kero na malalamiko ya wananchi kwa wakati na haki na uadilifu. Aidha, kupokea na kusikiliza na kuwahudumia wananchi wanaotembelea ofisi hizo kwa weledi hekima na busara;

(ii) Kufanya mapitio ya Sheria za Tawala za Mikoa na Sheria za Serikali za Mitaa ili kuendana na uboreshaji wa mifumo ya utoaji huduma kwa wananchi;

(iii) Kuimarisha makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuimarisha makusanyo ya mapato katika vyanzo vilivyopo ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi;

(iv) Kuimarisha Serikali za Mitaa ili ziendelee kuwa chombo cha kuwapa wananchi uwezo na sauti ya kuamua kushiriki kwa karibu katika shughuli za maendeleo, mwisho na mengine yanaendelea;

(v) Kusimamia kikamilifu suala la utawala bora ndiyo hapa ambapo watu wamekula hela hapa, narudia, kusimamia kikamilifu suala la utawala bora, uadilifu, uwajibikaji na matumizi sahihi ya rasimali za umma pamoja na miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika mamlaka hizo, itekelezwe kwa kiwango kinachokusudiwa kuhakikisha kuwa ubora wa miradi unalingana na thamani ya fedha iliyotumika.

Mheshimiwa spika, kwenye ripoti ya CAG inaonesha kwamba kwenye asilimia kumi zipo halmashauri kwamba kwenye asilimia kumi zipo asilimia 155 nchini hazikuweza kurudisha yale marejesho, bilioni 47.5. Bilioni 47.5 zote hizi cha kwanza, zimepora mamlaka ya wananchi ambazo ilani ya Chama cha Mapinduzi inasema; ‘kwamba mtawala yeyote anapokuwepo kwenye madaraka lazima ahakikishe anawapa nguvu wale ambao wao wamemuweka madarakani’. Hizi bilioni 47.5 zimepotea ziko kwenye mifuko ya watu, (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa sio najiuliza na ni wazo langu katika maazimio ambayo wenyeviti wa Kamati wanaweza wakachukua. Nikaona tu; kwa mfano TAMISEMI wangeamua kwamba waweke dirisha maalum linaloshughulikia mikop tu, labda tuchukulie kwamba afisa maendeleo wao wamekuwa na shughuli nyingi na hawana huo utaalam wa kusimamia hizi fedha. Hizi fedha ambazo zimepotea bilioni 47.5 ni katika kipindi cha mwaka mmoja tu 2021/2022, bilioni 47.5.

Mheshimiwa Spika, nikachukulia mfano, wako vijana wengi mtaani ambao hawajaariwa ambao ni bankers, accountant, pamoja na wachumi. Tufanye kama TAMISEMI, ingeamua kuajiri kwa kutumia fedha hizi hizi ambazo ni za Serikali, zimeliwa toka kwenye mifuko ya watu au zimepotea kwa uzembe ambao unasababisha na wataalam wetu kutokuvaa, kuzimiliki zile fedha kwamba ni fedha za Serikali.

Mheshimiwa Spika, mimi nikawa najiuliza, kwenye mabenki yetu, CRDB, NMB na benki zingine zilizopo hapa hapa nchini, hao ambao ni wataalam wa kusasanya mikopo wametoka nje wapi? Si wamesoma hapa hapa ni ma-banker wamesoma hapa hapa nchini kwetu mbona wana huo utaalam wa kukusanya mikopo? Kuna mwananchi yeyote amekopa hela benki anaweza akala fedha? Sasa kwanini sisi Serikali isitenge dirisha kuwaajiri wataalam, wahasibu, wachumi, ma-banker wakasaidia kutoa elimu, kukusanya fedha hizi na fedha hizi zirudi?

Mheshimiwa Spika, nikaweka hesabu ya kawaida tu kwa mfano TAMISEMI, waamua kumuajiri graduate ambaye amemaliza degree yake ya uchumi, uhasibu whatever ambaye anaweza kusimamia vizuri mikopo, waanze kwa kumlipa mshahara wa Shilingi laki saba, wakaajiri watu watatu kwenye halmashauri 84, nikapata kwamba wakiwaajiri watoto watatu kwa mwezi watakuwa wanawalipa milioni 2,100,000, ukichukua milioni 2,100,000 katika halmashauri 184 tutapata milioni 386,400,000. Nikaweka kwamba tufanya kwa miaka mitano ya majaribio, hii ambayo tunatekeleza ilani utakuta hawa vijana umewalipa bilioni 1.932; lakini unaona kwa mwaka mmoja hela zimepotea bilioni 47.5. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tafsiri yake tungeweze kuajiri vijana watatu tu, ambao ni uhasibu, banker na mchumi wanakaa yaani wao kitengo chao ni special kusimamia mikopo tu ya asilimia 10, katika kipindi cha miaka hiyo mitano ambayo tumeweka tungeweza kuwalipa bilioni mbili. Tafsiri yake ni kwamba tungeweza kuokoa hela.

Mheshimiwa Spika, lakini bado nikapiga hesabu, ukiwaajiri vijana hao kwenye halmashauri 184 utaajiri vijana wakitanzania wasiopungua 520. Kwa hiyo pia tungekuwa tume-solve changamoto ya ajiri. Hata hivyo, kama wangesimamia kwa ufanisi, zile hela zingekuwa zinazunguka; maana yake kama mwaka huu watu walikopeshwa bilioni moja, mwaka huu halmashauri ikakusanya tena bilioni moja vikundi vitapata, nikatolea tu mfano, mfano nikachukulia halmashauri yangu. Labda halmashauri yangu sisi labda mwaka huu wa fedha tulipata bilioni 1.7, kwa hiyo ni milioni 170; tukivigawia vikundi vitano wangeweze kupata milioni 34 kwenye kila kikundi. Tafsiri yake milioni 34 hii ingekuja na mwaka mwingine siwangekusanya? Milioni 34 ingekuja na vikundi vingine na wakati huo mapato yaongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hayo ni mapendekezo yangu kwa wenyeviti wa kamati, kwamba ipo haja ya kuona hili. Lakini wakati tunaendelea kuona ipo hoja ya kuona hivi hawa waliohusika na jambo washughulikiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni kuhusiana na benki ya kilimo. Benki ya kilimo, pamoja kwamba mwaka wa nyuma kuna kiwango cha pesa ambazo walipewa kama bilioni 208, lakini walikuwa wanaomba waongezewe mtaji angalau bilioni 760. Ni kweli, mimi ninatamani waongezewe hicho kiwango cha fedha ili kuleta tija kwa wananchi wetu ambao ni wakulima; na tukiangalia nchi hii kwa kiwango kikubwa wazalishaji wakubwa ni wakulima.

Mheshimiwa Spika, pia nataka niseme, watu hawa wa Benki ya Kilimo pamoja na kwamba mnataka kuongezewa fedha na Waziri wa Kilimo upo hapa, pamoja hatukushauri tunakusimamia muda huu, tunaomba kuona mnapotaka kuwaongezea fedha hizi tuwape, zikalete tija kweli kwa wananchi, zifike kule kwa wananchi ambao tunawakusudia. Ni kweli tunaona kuna benki ya kilimo, lakini kuna wakati jamani kule vijijini hatuona sana tija hii ya benki ya kilimo mwananchi wa kawaida hakopesheki, mwananchi wa kawaida kule kijijini hapati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nitoe mfano mzuri tu pamoja naongelea Benki ya Kilimo. Miezi miwili iliyopita tulipata ruzuku ya mbolea, tukaambiwa Wabunge tukatoe taarifa kwamba Serikali inatuletea mbolea, ni kweli mbolea imekuja. Cha kushanga sasa hivi tunavyoongea tumebakiwa na wiki mbili tu msimu wa mvua urudi wananchi vijijini waanze kulima mpaka sasa mbolea hazijafika vijijini, mpaka muda huu mbolea bado na sehemu zingine mbolea imeenda ya aina moja tu.

Mheshimiwa Spika, sasa tunajiuliza wakati mwingine mnapotuomba Wabunge tuwasaidie kuwapikishia hiki tuona na tija ili wakati mwingine tunapokuja hapa; kwamba kama tuliwasaidia kuwapitishia hizi fedha au ndio mnaomba tuwapendekezee kama sisi Bunge maazimio yetu, tuone na mambo ambayo yanafanana na mambo hayo. Kama ni Benki ya Kilimo imewezeshwa imfikie kweli mkulima, lisionekane tu lipo kundi la mapapa hawa ambao wao tu ndio wana-grub na kuchukua wao tu lakini mwananchi wa kawaida yule ambaye ndiye mzalishaji halisi, yule ambaye mpaka sasa hivi analima kwa jembe la mkono, yeye ambaye sasa hivi kununua mfuko mmoja tu wa DAP ni changamoto, amekopeshwa, mwananchi huyu ambaye bado hata mbegu yenyewe kununua ni shughuli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi tunategemea Benki ya Kilimo ndiye huyu tumkusudie apate. Wakati mwingine ukiwauliza watu wa Wizara wanasema Benki ya Kilimo kazi yake si kufungua matawi huko vijijini na sehemu zingine zingine kwenye wilaya kwa sababu hawafanyi transaction.

Mheshimiwa Spika, mimi ninajiuliza, kwani Mheshimiwa Rais, Mama Samia anaishi kwenye halmashauri zote 184? Si anaishi Ikulu hapa Chamwino na Dar es Salaam? Lakini mbona miradi yote akitoa inafikia halmashauri zote 184? Kote anapeleka. Kwa hiyo, kaeni na benki Dar es Salaam, whatever, wekeni kwenye kanda lakini tunachotaka huduma zifike. Whether mtatafuta mawakala wakufikisha hizi huduma kwa wananchi or mtaunda vikundi, lakini tunataka mkulima wa kawaida, yaani tunaongelea mkulima wa kawaida.

Mheshimiwa Spika, na katika hili nimuombe Mheshimiwa Waziri Bashe, twende nikakukutanishe na wakulima wa kawaida huko vijijini ili tunapoongea muwasilize wenyewe kwa masikio yao, hawapati mikopo.

Mheshimiwa Spika, naunga hoja zote za kamati ambazo ziko mezani, ahsante sana. (Makofi)