Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nichangie kwenye hoja hii ambayo ipo mezani. Mimi ni mjumbe wa Kamati ya PIC. Kwa hiyo nitajikita zaidi kwenye Kamati hiyo.

Mheshimiwa Spika, nianze kwanza kwa kukupongeza wewe kwa kazi nzuri ambayo unafanya, unaongeza Bunge hili kwa umahiri mkubwa, hadi IPU imekuona; hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nisiishie hapo, nimshukuru Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuandika historia kwenye Jimbo langu. Ametuletea fedha nyingi za maendeleo. Hapa si mahali pa kuzizungumzia sana, lakini itoshe kusema nashukuru mno, ameandika historia kwenye Jimbo langu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia, nichukue nafasi hii, kupongeza Wenyeviti wa Kamati hzi tatu PAC, PIC na LAAC, pamoja na wajumbe na wote kwa kazi nzuri ambayo wamefanya na hatimaye hizi taarifa zikaja mezani kwako.

Mheshimiwa Spika, Serikali kama baba ambavyo anahangaika kutafuta resources huku na kule, mikopo ya bei nafuu, misaada, yote hii ni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba anatuletea maendelo wananchi wake. Fedha hizi Serikali imeamua kwamba, pamoja na mambo mengine tutumie resources zote kuziweka kama mitaji kwenye kampuni na taasisi zake.

Mheshimiwa Spika, Kamati yetu ilipewa jukumu la kuchambua na kubaini ufanisi wa uwekezaji huu ambao Serikali inafanya, ambao ni uwekezaji mkubwa sana. Hadi kufikia tarehe 30 Mwezi wa Sita mwaka 2021 Kamati ilibaini kwamba Serikali ilikuwa imewekeza kwenye taasisi na kampuni zake shilingi trilioni 67.95. Hizi ni fedha nyingi sana. Pia, katika uchambuzi, tumebaini kwamba, TR alieka maotea; ali-project kufanya makusanyo ya returns za uwekezaji wa takribani bilioni 930.3, lakini halisi iliyokusanywa ni bilioni 637.66.

Mheshimiwa Spika, tukiendelea kuchambua yale makusanyo ambayo yanatakiwa yakusanywe, kwa maana ya gawio percent 15 ya mapato ghafi ya Serikali na kampuni hizi, urejeshaji wa mikopo, urejeshaji wa TTMS na makusanyo mengine; tumeona kwamba kulikuwa na mapungufu. Kwa mfano, gawio, maoteo ya TR yalikuwa ni bilioni 408 lakini halisi ilikuwa ni bilioni 308.

Mheshimiwa Spika, Kwa hiyo ufanisi hapa ilikuwa ni percent 75.61. Percent 15 ya makusanyo ya kisheria, maoteo ilikuwa bilioni 365.4 makusanyo halisi ilikuwa bilioni
202.2. Kwa hiyo ufanisi hapa wa mtaji ulikuwa percent 51.

Mheshimiwa Spika, tuliendelea kuchambua na kuangalia kwamba ni sababu gani zimepelekea haya mashirika na taasisi za Serikali zikashindwa kufikia malengo. Tukachambua changamoto, tukatazama mashirika yale ambayo yalikuwa yamelengwa, tukaona kulikuwa na matatizo kidogo. Moja, kulikuwa na shida kubwa, taasisi zile zinakuwa hazina Bodi za Wakurugenzi kwa muda mrefu, lakini pia, taasisi zile zilikuwa hazina vibali vya kuajiri wataalum, kwa hiyo vibali vinachelewa sana, matunda yake ufanisi unakwenda ndivyo sivyo.

Mheshimiwa Spika, pia, tuligundua kwamba kuna mwingiliano wa majukumu kati ya taasisi na taasisi. Kwa mfano TANROADS na TIA; ukijaribu kuangalia majukumu yake utakuta yanafanana; lakini TIA wamepewa umiliki, hawaangaliii ujenzi, wao wamepewa jukumu la kuangalia matengenezo ya kazi ambayo imefanywa na mtu mwingine; kwa hiyo, quality ya kazi hawaijui. Lakini pia kulikuwa na tatizo la kuajiri wataalamu. Tumekuta bodi nyingi sana hazina Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi, au watumishi wana kaimu. Hilo ni tataizo kubwa sana kwa sababu hatimaye maamuzi hayafanyiki on time (kwa wakati).

Mheshimiwa Spika, lakini pia, kulikuwepo na tatizo la mitaji. Utakuta Serikali inanzisha taasisi na kuahidi itatoa mtaji kamili, mfano mzuri ni Benki ya TADB ambayo ilikuwa inahitaji mtaji wa Shilingi bilioni 760. Hadi mwaka jana ilikuwa imepata bilioni 208, zikaongezeka bilioni 60. Kwa kweli tunaona kwamba uchelewaji wa mitaji au kutokuwa na mitaji kuna athiri performance za hizi taasisi za Serikali ambazo zimeanzishwa kwa lengo zuri tu la kuhakikisha kwamba fedha zinazungushwa na faida ipatikane, iweze kwenda kuhudumia wananchi.

Mheshimiwa Spika, pia, kuna taasisi ambazo zilianzishwa lakini zina madeni chechefu; kwa mfano TIB na TCB. Hizo ni benki ambazo vitabu vyake vinaonyesha kwamba kuna madeni makubwa ambayo hatimaye hatuamini kama yatalipika. Wazo letu kama Kamati ni kuwa utaratibu ufanyike ili hao madeni yaangaliwe namna ya kufutwa bila kuathiri ukusanywaji wa yale madeni ambayo yanalipika.

Mheshimiwa Spika, kwa maelezo hayo mafupi, Kamati ilikaa ikatoa maoni yake, ikatoa mapendekezo yake na maazimio. Kwa kulinda wakati, niseme kwamba, mimi kama Mwanakamati wa hii Kamati ya PIC, naungana na Mwenyekiti na Wajumbe wote kuunga mkono mapendekezo, maoni na maazimio ambayo yapo kwenye taarifa.

Mheshimiwa Spika, nisiishie hapo, pia nimesoma hizi taarifa za Kamati zingine; zinaeleweka, nako niseme kwamba pia naunga mkono yale maoni, mapendekezo na maazimio ambayo yamewekwa kwenye zile taarifa

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache, niseme nashukuru sana kwa nafasi hii naunga mkono hoja. (Makofi)