Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii ya kuchangia ripoti ya CAG pamoja na ripoti ya Kamati Tatu ambazo zimeletwa mbele yetu. Nitajielekeza kwenye maeneo manne, nianze na PIC kwenye taarifa yao ya uchambuzi wa taarifa hii ya CAG, katika ukurasa wao wa 24 kipengele cha Mbili, Nne na cha Tano kuhusiana na mikopo chechefu.

Mheshimiwa Spika, hili ni tatizo na pamoja na kwamba tunaangalia benki hizi za Serikali hasa TADB na TCD ni vizuri tulifungamanishe na suala la interest rate ambalo tunalipigia kelele kila siku, ukiongea na Commercial Banks kwa nini interest rate haiwezi kushuka wanasema ni kwa sababu ni risk kubwa kwa mikopo ya kwetu, ambayo inaonekana hata kwenye benki zetu kwamba mikopo, kwa mfano ukiangalia kwenye ile taarifa mpaka asilimia 58 ya mikopo inaonekana ni mikopo chechefu.

Mheshimiwa Spika, nadhani kuna mahali tunakwama hasa kwenye eneo la uhasibu, mimi nadhani kwa ukiangalia SME biashara hizi za kati na biashara ndogo nyingi zinapopeleka mahesabu hata kwenye commercial Bank kunakuwa na mahesabu ya benki ambayo yanaonyesha yanafanya biashara kubwa na anapata faida kubwa, lakini kuna mahesabu ya pili yanakuwa ni ya TRA ya kuonesha kwamba hawatengenezi faida au faida kidogo na haya yote yanakuwa certified na hawa watu wanaitwa CPA ninajua na huku wapo. nadhani ni suala la kuweka mfumo ambao utafungamanisha ili tuweze kwanza tutoe mikopo ambayo itawasaidia wafanyabiashara na taasisi zinazofanya biashara, lakini tutoe mikopo ambayo italeta tija pia kwenye Serikali.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, nadhani tunaweza kufanya jambo moja tukapitisha Sheria ambayo inaifungamanisha NBAA taasisi za fedha pamoja na wafanyabiashara waliopo. Maana yake ni nini, taasisi inataka kutoa mkopo kwa mfanyabiashara fulani au kwa kampuni fulani ni rahisi tu, inatakiwa kuwe na sehemu ambapo financial institution ikienda inaona mahesabu yake ambayo yana uhalisia na yana-reflect kodi yanayolipa. Kwa sababu kama yanapata faida kwa nini asilipe kodi, kama halipi ina maana atakuwa na sababu gani asilipe.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo sasa tunaenda unakuta mtu anapeleka mahesabu makubwa kwenye taasisi za fedha, inaonekana faida ni kubwa, anapewa fedha ambayo pengine hana hata uwezo nayo ndiyo tunaingia kwenye mikopo hii ambayo ni mikopo isiyolipika au ni mikopo chechefu.

Mheshimiwa Spika, nafikiri tuangalie sheria ya namna ya kufungamanisha, kama kulivyotengenezwa credit bureau kuwe kuna sehemu ambapo financial institution ikienda ikichukua mahesabu ya biashara fulani inayotaka kukopeshwa anaweza akaona pia output ya kodi ambayo inaendana na mahesabu aliyoletewa na ikawa haina mawaa. Hilo ni wazo la kwanza kwa PIC. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sehemu ya pili kwenye taarifa ya PIC ni kwenye uwekezaji wa fedha hizi za umma, mitaji kwenye hasa shughuli hizi za kibiashara. Katika ukurasa wa saba waripoti yao wameeleza vizuri namna kile kipengele cha 22.1 na 22.2 wameeleza ni namna gani fedha za umma zinawekezwa na zinakusanywa vipi na zinategemea zilete faida gani? Ninaomba niende sehemu moja tu ya mfano, Serikali inawekeza fedha nyingi sana pale Moshi Mjini kwenye Kiwanda cha Karanga Leather, nia yake ni nzuri na tunategemea kupata ajira labda 3,000 au zaidi, ukiangalia kwenye mnyororo wa faida, faida ni kubwa zaidi, lakini ukiangalia ule uwekezaji na namna ambavyo tunazi-manage ni dhahiri kabisa kwamba matokeo yake mwisho mtakuja kuiona Karanga Leather kwenye vitabu vya CAG tena! Kwa nini?

Mheshimiwa Spika, uwekezaji ni mkubwa mpaka sasa hivi ni zaidi ya Bilioni 156 lakini namna unavyokuwa managed ni jinsi mnavyoona sasa kwamba, tunasubiri matamasha tulete pair tatu za viatu hapa, tunasubiri warsha tulete viatu na mabegi, wakati investment hii inatakiwa itoe production kubwa ambayo inaweza ikatuelekeza kwenye export. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi sioni shida kwa sababu ukiangalia structure ya Dubai Port ambayo ni mali ya UAE wako wataalam kutoka nje wabobezi kwenye mambo ya bandari ambao wanafanyakazi na faida inakuja pale, kwa hiyo nafikiri kiwanda kikubwa kama hiki sasa hivi kimeajiri watu 253 tu na kiko miaka tayari imeshafika minne hakijamaliziwa, ninafikiri kuna haja ya kuwatafuta wabobezi wa biashara wa ndani na nje, na wabobezi wa masoko watusaidie kuendesha tuwalipe tupate faida, lakini tukiendelea kuviendesha kwa utaratibu wa teuzi na hizi Bodi ambazo PIC nao wameelezea matatizo yake, ni dhahiri kwamba matokeo ya kiwanda kama hiki hayataonekana na baadae itakuwa hasara na tutarudi kwenye vitabu kuonesha kwamba hela hii imepotea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, eneo lingine naomba niende kwenye taarifa ya LAAC na hapa nianze na ile mikopo ya vikundi, ni dhahiri kabisa tunaipenda ile mikopo inawaidia watu wetu, lakini ukiangalia hii taarifa ya CAG, ukiangalia uwezo wa kurejesha wa hiyo mokopo ni dhahiri hizi hela tumezitoa kama ruzuku. Hii iitwe TASAF part two kwa sababu hizi hela kuna maeneo mimi nilifanya ziara Jimboni, kuna maeneo vikundi vimekopeshwa 45 kinarudisha kikundi kimoja tu, maana yake ni nini? Kwamba ni hela tumetoa za kwenda ku-boost uchumi siyo za kuzunguka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa nini nasema hivi? Ukiangalia structure ya ule Mfuko hasa baada ya kupitisha Sheria kwamba uwe wa mzunguko, ni kwamba fedha hizi za kila mwaka, kwa kila Halmashauri maana yake zikiwa zinarejeshwa na bado tunatenga ule mfuko utakuwa mkubwa, utaweza hata kuwafikia mtu mmoja mmoja. Lakini kwa sababu hazirejeshwi ule Mfuko haukui.

Mheshimiwa Spika, kwenye ule ukurasa wa 11 wamesema mwaka huu kwa mapato ya Halmashauri zote asilimia 10 inaweza ikafika Bilioni 75, hizi ni hela nyingi sana, lakini tunaenda kuitoa halafu haitarejeshwa, mwaka unaofuata tutatenga tena na tena, maana yake ni nini? Badala ya kuwasaidia watu wajikomboe kwenye umaskini au kuwasaidia wananchi kiuchumi, tunaenda kuwasababishia umaskini kwa sababu tunajua ni hela ya kwenda kufanyia shughuli ambayo siyo serious, hela hizi hazina riba na huweki collateral.

Mheshimiwa Spika, ninaungana na Mbunge aliyesema ni vizuri tuzi-contract kwa benki. Mimi nilishawahi kufanya field Benki ya Akiba Manzese, kuna hela ya kuwasaidia akina mama walio na uwezo wa chini sana kutoka ILO walikuwa contracted Akiba Commercial Bank ndiyo wakawapelekea wale watu, mabenki wana uwezo wa kufuatilia kutathmini biashara ya mtu, kuishauri na wakaweza kutoa ule mkopo na kufuatilia kwa njia ambayo itakuwa haina matatizo kwetu, nasi tutakachofanya ni kuiongezea ile benki mtaji kwenye hizi hela, tunakubaliana kwamba wao watabaki na percent kiasi Fulani, siyo kwamba waongeze gharama ili waweze kuwachaji wale wanufaika, lakini kwa Afisa Maendeleo ya Jamii kwenda kukopesha hela, kutathmini biashara na akasema inatoa faida hii biashara na akafuatilia akusanye hiyo hela, tunajidanganya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni vizuri tutafute mfumo mbadala, sijajua mfumo ambao TAMISEMI wameuanzisha kama utaleta majibu lakini tukikubaliana na benki zetu tukatangaza tenda, Bilioni 75 kwenye mfuko wa benki yoyote ni hela nyingi, tukawaelekeza, utaratibu ule wa kukopesha tukaufanya sisi wao wakaenda kumalizia kwa ku-verify na kutoa ushauri fedha hizi zinaweza zikaleta tija. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye hizi fedha bado kuna matatizo, uwiano ni asilimia Nne kwa vijana, Asilimia Nne akina mama na asilimia Mbili kwa walemavu. Sasa Serikali inataka kulazimisha kwamba hata mahali ambapo walemavu hawataki mkopo tulazimisha hizo hiyo asilimia Mbili wapewe, sasa hawataki au hawapo lakini inakuja ni kweli kwamba kwa nini mmekopesha akina mama zaidi? walemavu hawajakopeshwa? wapo hawataki kufanya biashara, maana yake sasa wanalazimishwa Afisa Maendeleo ya Jamii ili wasipate hiyo kero wanawalazimishia watu mkopo, wewe chukua tu! Sitaweza kurudisha, wewe chukua tu utarudisha utaangaliaangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa huu uwiano uwepo lakini maeneo ambayo kwa mfano, maeneo mengi nimejifunza vijana hawawezi kukaa pamoja kwa muda mrefu kwa sababu bado ni watu wanaotafuta wanaenda sana, kwa hiyo ni wachache sana wanakuwa kwenye makundi lakini akina mama ni watu walio-settle wapo kwenye lile eneo, kwa hiyo tusilazimishe kwamba huu uwuiano ufuatwe kama inaonekana wana uwezo zaidi au vijana wana uwezo zaidi hilo eneo wapewe fedha zirudi lakini kubwa zaidi ziweze kusimamiwa vizuri watu wapate. Isitokee kwamba kuna kundi linahitaji likakosa na share yake imetoka lakini kama halipo na mwaka unaisha wa fedha wapewe wale kundi ambalo liko tayari liweze kufanyia kazi hizo fedha (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende eneo la mwisho ni eneo ambalo kwenye taarifa ya LAAC ukurasa ule wa Saba kipengele 2.2.3 udhaifu wa manunuzi na usimamizi wa miradi. Watu wengi wameliongelea, ni kweli kabisa kuna udhaifu mkubwa kwenye manunuzi ambayo nafikiri kila mtu atasema ifumuliwe lakini ikifumuliwa sijui itawekwa kwa namna gani ili manunuzi yaweze kuleta tija, kwa sababu kalamu ya Shilingi 1,000 ambayo wewe unaweza kununua, ikinunua Serikali itanunua 2,000 mpaka 3,000 wataalam watashauri namna ya kurekebisha mfumo wa manunuzi.

Mheshimiwa Spika, niende kwenye force account. Hili ni janga force account by design ilitakiwa iende sehemu ambayo tunao wataalam wanaojitosheleza. Halmashauri iwe na Injinia wa ujenzi anayejua, iwe na Mthamini anayejua, iwe na watu wote wa technical wanaojua ili ile hela waisimamie kama ilivyo kwenye kampuni.

Mheshimiwa Spika hela, zinapelekwa kwenye halmashauri zinaambiwa zifanye kazi kwa force account, hiyo Halmashauri haina hata Injinia tunachotegemea ni nini? Tunakwenda kutengeneza matatizo makubwa, iko miradi ambayo baada ya muda haitafaa. Nitolee mfano kwenye Halmashauri moja juzi wamepelekana TAKUKURU, mradi unavyoonekana ukiangalia kwa sababu hela tunapeleka sehemu moja, tunapeleka hela za kufanana maeneo yote, lakini ukija kuangalia hela sehemu moja imefanya vizuri tena Halmashauri zilizoko karibu, sehemu nyingine hakuna kitu kabisa, lakini kuna maeneo mengine inaenda hela kwa ajili ya force account lakini unakuta hata eneo la labor wamem-contract mtu, kwa hiyo contractor anapewa tena labor kampuni kabisa inapewa kazi ya labor. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa utaratibu huu wa force account ni lazima tukubaliane aidha hiyo sijui kuajiri tunaweza au hatuwezi ziende sehemu ambazo wataalam wapo wa kutosha ndiyo fedha zipelekwe kwa utaratibu wa force account, vinginevyo tuwape Wakandarasi kwa sababu bahati nzuri tunapata mpaka retention kule na baada ya muda kama huo mradi haujakaa sawa tunauwezo wa kuwaambia warudie, lakini kwenye force account ikishakuwa imeharibika inaharibika na ni ya kwako. Ninashauri force account…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)