Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia katika hoja mbalimbali za Kamati ambazo zimewasilishwa ndani ya Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuwapongeza Wenyeviti wetu wa Kamati ambao wamewasilisha Taarifa nzuri, pia Kamati zimefanya kazi nzuri ya kuhakikisha kwamba tunaendelea kutoa maoni na kuishauri Serikali katika maeneo ambayo tumeona kuna changamoto mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, pia niendelee kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, wetu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuhangaika kule na kule kutafuta fedha kwa ajili ya Uwekezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Nchi yetu. Pia nimpongeze Mheshimiwa Rais, wetu kwa kuridhia fedha za export levy asilimia Hamsini kurudi katika Mfuko wa Maendeleo ya Korosho. Fedha hizi tulikuwa tumezikosa kwa kipindi cha muda karibia wa miaka Minne, mitano pia tulipata changamoto mbalimbli katika kuhakikisha kwamba zao la korosho linaendelezwa kama ambavyo tumelikusudia. Kwa hiyo, niishukuru sana Serikiali kwa kutoa uamuzi huu wa kuhakikisha kwamba asilimia 50 inarudi katika Mfuko wa Maendeleo ya Korosho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile ninaomba sana Bodi ya Korosho kuhakikisha kwamba fedha hizi zinasimamiwa ipasavyo katika matumizi ya Mfuko wa Maendeleo ya Korosho. Tunajua kwamba Wakulima wetu walipata changamoto mbalimbali lakini hata Bodi ilipata changamoto katika kuhakikisha kwamba wanafanya kazi zao za kuhakikisha kwamba zao hili la korosho linaendelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie suala la Shirika letu la Maendeleo Tanzania (NDC). Tumekuwa na mradi huu wa Mchuchuma na Liganga wa muda mrefu lakini tunashindwa kutekeleza kutokana na changanoto mbalimbali ziliyopo, ninaiomba sana Serikali kuhakikisha kwamba inamaliza mazungumzo na Mwekezaji huyu GNT kuhakikisha kwamba NDC sasa wapewe fursa ya kuendeleza mradi huu wa Mchuchuma na Liganga. Ni mradi mkubwa, mradi ambao utatuletea fedha nyingi na utatuingizia mapato ya kutosha pia tutakuwa na ajira nyingi za kutosha katika maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nizungumzie suala la Shirika la TPA kwa maana ya Mamlaka ya Bandari Tanzania. Nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu amewekeza fedha nyingi katika kuhakikisha kwamba Babdari ya Dar- es-Salaam inapanuliwa, Bandari ya Tanga, Bandari ya Mtwara katika kuhakikisha kwamba tunaendelea kutoa huduma mbalimbali lakini kuongeza Mapato ya nchi yetu na kuhakikisha kwamba uchumi wetu unaendelea kukua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile Mheshimiwa Rais amewekeza katika mradi mkubwa wa SGR. Sasa ninaomba ndugu zangu wa bandari wachangamkie fursa hii, kuhakikisha kwamba wanajipanga vizuri kuona namna ya kutumia usafirisahaji wa mizigo kutoka bandarini kwa kutumia njia hii ya reli kupitia mradi wetu wa SGR ili kusafirisaha mizigo mbalimbali ambayo inatoka bandarini.

Mheshimiwa Spika, SGR inauwezo wa kusafirisha tani 10 kwa safari moja, kwa hiyo tutakuwa tumenusuru na tumesafirisha mzigo mkubwa kwa haraka, pia tutakuwa tumeongeza mapato na ajira na wadau mbalimbali wataendelea kufurahia huduma ya bandari yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini Mheshimiwa Rais pia, amewekeza katika mradi mkubwa wa SGR. Sasa ninaomba ndugu zangu wa bandari wachangamkie fursa hii, kuhakikisha kwamba wanajipanga vizuri kuona namna ya kutumia usafirishaji wa mizigo kutoka bandarini kwa kutumia njia hii ya reli kupitia mradi wetu wa SGR ili kusafirisha mizigo mbalimbali ambayo inatoka bandarini. SGR ina uwezo wa kusafirisha tani 10 kwa safari moja. Kwa hiyo tutakuwa tumenusuru na tumesafirisha mzigo mkubwa kwa haraka, lakini pia tutakuwa tumeongeza mapato na ajira na wadau mbalimbali wataendelea kufurahia huduma ya bandari yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia ningeomba ndugu zetu wa TICTS wanaosafirisha ma-container kutoka bandarini; uwezo wa bandari yetu ni mkubwa sana. Kamati yetu imetembelea katika Bandari yetu ya Dar-es-Salaam na tumeona huduma ambazo zinatolewa katika bandari ile. Hata hivyo, tuna changamoto kubwa kwa ndugu zetu wa TICTS hawa katika terminal gate number 8, 9, 10 na 11, na juzi madereva wamefanya mgomo kwa sababu ya huduma mbovu inayotolewa na ndugu zetu hawa wa TICTS, wanasababisha wanaotumia Bandari yetu ya Dar- es-Salaam kuona kwamba kuna changamoto na hatimaye tunaweza tukapoteza sifa ya Bandari yetu ya Dar-es-Salaam; na Bandari yetu ndio roho ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niombe ndugu zetu wa Bandari kuhakikisha kwamba wanaendelea kufanya mazungumzo ya kimkataba na ndugu zetu hawa wa TICTS ili waendelee kutoa huduma nzuri na bandari yetu iwe na sifa ya kuendelea kutumika katika nchi yetu. Niwaombe pia ndugu zetu wa Bandari kuhakikisha ujenzi wa magati mapya ya namba 12, 13, 14 na 15; kuhakikisha kwamba upanuzi huu unaendelea kufanyika na bandari yetu iendelee kuwa na sifa ya wadau na wawekezaji mbalimbali waweze kutumia.

Mheshimiwa Spika, lakini pia, sasahivi Serikali inabidi tujipange kuhakikisha kwamba tunapanua bandari kwa kujenga Bandari ya Bagamoyo. Kwa sababu sasahivi ukiangalia Bandari ya Dar-es-Salaam imeshasheheni. Na ukiangalia baada ya miaka 10 Bandari ile itakuwa imeelemewa. Kwa hiyo ni wakati muafaka sasa wa kuhakikisha kwamba, Serikali inajipanga vema kuhakikisha kwamba tunajenga Bandari yetu ya Bagamoyo.

Mheshimiwa Spika, lakini kuna jambo ambalo tulishaondokananalo, lakini sasahivi linaanza kunyemelea katika Bandari yetu ya Dar-es-Salaam. Wanaopokea mizigo yao kuna kasoro ndogondogo za wizi wa vitu vidogovidogo. Kwa hiyo, niiombe sana Serikali, niwaombe ndugu zetu wa Bandari kuhakikisha kwamba wanaendelea kuimarisha ulinzi ili kuhakikisha kwamba wanaosafirisha na kupokea mizigo yao basi iwe salama.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hayo ni mambo muhimu sana katika mashirika yetu kuhakikisha kwamba wanaendelea kusimamia huduma zetu vizuri na wananchi mbalimbali waendelee kutumia Bandari yetu ya Dar-es-Salaam.

Mheshimiwa Spika, lakini ninajua ya kwamba, Serikali imewekeza fedha nyingi ili kupanua Bandari ya Tanga, pamoja na upanuzi wa Bandari ya Mtwara. Tuhakikishe kwamba tunaendelea kusimamia huduma zile muhimu ambazo zinahitajika katika maeneo ya bandari hizi ambazo nimezitaja ili ziendelee kufanya kazi vizuri. Tunaona kwamba Serikali imefanya kazi kubwa na imesogeza huduma karibu kwa wananchi, lakini pia imepunguza msongamano mkubwa ambao ulikuwa unajitokeza pale Dar-es-Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie suala la TARURA. Tunayo changamoto katika eneo hili la TARURA. Tunaona kwamba Serikali imewekeza sana fedha nyingi, lakini tunaona uwezo wa TARURA kuna upungufu mkubwa wa ma-engineers katika maeneo ya Halmashauri zetu, tumeona pia kuna changamoto ya uwepo wa Ofisi za TARURA pamoja na changamoto kubwa ya uwepo wa magari. Kwa hiyo ndugu zetu hawa wanashindwa kusimamia kwa sababu ya ukosefu wa vifaa hivi. Ninaiomba sana Serikali kuhakikisha kwamba tunakamilisha kuwa na ofisi za TARURA, lakini kuwa na vitendea kazi vya kuwarahisishia kufuatilia ujenzi mbalimbali ambao unaendelea katika maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kukushukuru sana lakini pia niunge mkono ushauri uliotolewa na Kamati ya PIC pamoja na hoja ambazo ziko mbele yetu.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru na wewe nakutakia kila la heri, Mwenyezi Mungu aendelee kukubariki. Ahsante sana. (Makofi)