Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuweza kuchangia mawasilisho ya Kamati tatu zinazosimamia fedha za umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuwapongeza wachangiaji waliotangulia, na nimpongeze Mheshimiwa Spika kwa kuona unyeti wa kujadili fedha za wananchi na fedha za walipa kodi kwa kina ili kuona namna ya kutekeleza ripoti ya CAG, kama jicho letu kama Bunge kikamilifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuipongeza Serikali ya Mama yetu ya Mama Samia ambayo imekuwa ikitafuta vyanzo na ikitafuta fedha usiku na mchana. Serikali imekuwa ikisafiri kutafuta wahisani mbalimbali kuja kuwasaidia Watanzania. Lengo la Serikali si kumaliza matatizo yote ya wananchi lakini angalau kupunguza shida zao kama inavyoonekana kule kwenye majimbo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa leo tunajadili ripoti ya kamati tatu, Kamati inayosimamia halmashauri zetu (LAAC), Kamati ya Mitaji ya Umma na Kamati ambayo inasimamia Mashirika ya Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na michango mingi sana ya Wabunge; nikianza kwanza na Kamati ya kwanza inayosimamia halmashauri zetu nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa na tatizo moja, unakuta Waziri Mkuu anakuja kwenye maeneo yetu kukagua miradi, Waziri Mkuu ndiye anayekuja kugundua kuwa top za milango zina ufa; Waziri Mkuu anakuja kwenye miradi ndiye anayegundua kibanda cha 1,200,000 kimejengwa kwa 20,000,000 ilhali Serikali ipo kuanzia ngazi ya kitongoji, Kijiji kuja kwenye kata, wilaya na mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi napata kigugumizi sana. Kama kweli katiba yetu tulivyoitengeneza tungeisimamia vizuri kazi ingekuwa ndogo sana. Haya mambo yanayokuja kugundulika na viongozi wa kitaifa wakija katika maeneo yetu si kama viongozi waliopo kule hawajayasema. Shida yetu iko moja, hata sisi wanasiasa, tuposema au tunaposhauri watu wanaona wanasema wanasiasa acha waongee na hivyo hakuna utekelezaji wake. Kwa hiyo mimi niiombe Serikali kupitia Bunge hili kwa sababu Bunge limeumbwa na wanasiasa na Mheshimiwa Rais ni mwanasiasa. Kwa wale ambao wanaoona siasa haiwezi kufanya kazi au kushauri basi wakatafute kazi nyingine ya kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wametuleta huku kuja kuwatetea, wametuleta huku kuja kuwasemea. Leo tukienda kule zahanati ya pale kijijini mwananchi mwenyewe anakwambia mifuko ya cement ilikuwa inaondoka hapa halafu watu wanasema wanasiasa wanapiga kelele. Kwa hiyo mimi niombe, sisi wanasiasa ni kweli tuna maneno mengi lakini kwenye ubadhilifu lazima tuwe wakali; na ndiyo maana nimempongeza Mheshimiwa Spika kwa kuongeza muda wa kujadili ili Wabunge wote waseme nini kilichopo katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kwenye Bunge la Bajeti nilisema hapa, kwamba tumekuwa na tatizo moja; fedha za Serikali zinapokuja kwenye miradi vitu vinapanda bei lakini chanzo cha kupandisha bei hatukioni. Juzi mmepeleka bilioni 160 kwaajili ya kujenga madarasa 8,000, cement ilikuwa 20,000 kwenye mikao ya mbali lakini baada ya kufika zile fedha siku mbili kabla cement imefika 24,000 mpaka 25,000 katika baadhi ya maeneo. Tatizo ni nini? pochi ya mama imetema. Sasa kama pochi ya mama anahangaika kutafuta fedha halafu na sisi Serikali tunajua hakuna kitu kilichosababisha kupandisha bei na tumekaa kimya, hakuna hata Waziri wa Viwanda na Biashara kwenda kubainisha na kutoa taarifa kama uhaba wa cement. Mimi niiombe Serikali kwenye haya tuwe serious.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikirudi kwenye Kamati ya PAC; tumejadili sana. Ukija kuiangalia ripoti ya CAG imebainisha sana, na sisi kama Bunge tumeiamini taasisi yetu ya CAG Kwenda kutuangalizia. Inapotuletea hapa inatuonesha kabisa kwamba sehemu fulani kuna mianya. Sisi tusipochukua hatua tunaivunja moyo taasisi ambayo sisi tuliiamini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nishauri jambo moja. Si kama hawa watu hatuwahoji. Tumekaa hapa tangu mwezi wa 10, tumeita mashirika mbalimbali na tumewahoji ni aibu sana. Kwa kweli ni aibu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba, kama kanuni haziruhusu hebu tuone haya mashirika yakiitwa kwenye kamati ambayo ni Bunge dogo ambalo limeundwa na Mheshimiwa Spika kwa niaba ya Bunge zima ameyagawa mabunge madogomadogo ili kusimamia shughuli za Bunge. Hebu sasa kama tunaweza kurusha live humu ndani hebu na kwenye kamati tuwe tunarusha live waone wataalamu tuliowapeleka kule. Unakuta kabisa mwanasheria mbobevu, msomi darasa la saba anamuuliza swali la kitoto anashindwa kujibu. Sasa wakipigwa mara tatu mpaka nne kwa mikataba fake ambayo inatuingizia gharama wananchi. Wanalipa kodi kwa shida halafu fedha zinakwenda kupotea kirahisirahisi halafu mtu anajibu kirahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi naliomba Bunge hili kama kanuni hazipo, kamati zote wanapoitwa, hasa hizi zinazosimamia fedha za umma, CAG akionyesha mianya, basi na vyombo vya habari viwe vinaingia ili virushe moja kwa moja ili wananchi waone kama tulihoji na wao wamejichanganya vipi. Hii itaongeza ufanisi mzuri katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, asubuhi hapa Wabunge wengi wamezungumza kuhusu Kampuni ya KADCO. Ukija kuangalia sinema inayochezwa kule na KADCO ni aibu kubwa. Serikali imenunua hisa halafu bado ikajipangisha yenyewe. Imetengeneza mkataba ambako inamiliki asilimia 100 halafu yenyewe tena inaanza tena kujipangisha. Sasa nashindwa kuelewa kama mimi nina nyumba ninamiliki asilimia 100 halafu tena naanza kujilipa kodi, inaingia akilini kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kamati ililiona hilo, tumewaita KADCO wanachokisema pale yaani kama watu vile wanaona tu hili acha goma liende kwa sababu halina mwenyewe. Sasa mimi niwaambie wenyewe ndio sisi kwa niaba ya wananchi. Kama tusiposema, tusipotetea siku ya mwisho tutakuja kuhukumiwa. Jumba hili limepewa heshima kwa niaba ya wananchi milioni 60; na Tabora tumekuwa wa tatu tunaongezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo milioni 61 wametuamini sisi mia tatu, mia mbili na tisini na kidogo kwenda kuwatetea tunapokuja humu tunaleta maigizo, ngonjera, kuona kama hatuoni kumbe tunaona tutakuja kupata adhabu kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niombe Bunge hili litoe maelekezo. KADCO tumependekeza kwenye kamati kwamba irudi chini ya usimamizi wa viwanja vya ndege. Lirudi kwenye usimamizi wa viwanja vya ndege kwa sababu Serikali ndiyo inamiliki hisa asilimia 100. Kama tunamiliki asilimia 100 na TAA iko chini ya Serikali kwa hiyo huyu akija haina tija tutakuwa tumemwongeza mtoto mwingine hata kama alikuwa wa kambo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija kuangalia KADCO hii tunayoizungumza yaani iliweka mkataba wake ambao unaisha tarehe 16 yaani ilisema hivi, asitokee mtu yoyote hate yenyewe Serikali isijenge uwanja wa ndege wowote zaidi ya kilometa 240 kila upande kutoka KIA. Hii maana yake ni kwamba Arusha wasijenge uwanja wa ndege na watu wa Manyara wasijenge uwanja wa ndege. Mimi niiombe Serikali kupitia hili irudishe KADCO iwe chini ya usimamizi wa TAA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja. Ahsante nakushukuru sana. (Makofi)