Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

Hon. Ravia Idarus Faina

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021

MHE. RAVIA IDARUS FAINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kuwa mzima na kusimama mbele ya Bunge lako na kutoa mchango wangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi limeanzisha Mfuko wa Tuzo na Tozo kwa Jeshi la Polisi, Mfuko huo kwa ajili ya ustawi wa askari, lakini cha kushangaza mpaka sasa hivi hakuna kanuni za kusimamia uendeshaji wa Mfuko huo, hivyo inapelekea kuwa na wasiwasi wa matumizi ya Mfuko huo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi limeweka vizuri sheria na miongozo yake kwenye PGO. Kwa nini hawataki kufuata taratibu hizo walizojipangia hasa kwa askari wadogo. Kwa mfano, posho za maaskari wadogo haziendani na vyeo vyao, kama vile posho za mavazi, udereva, kibaka chekundu na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile, posho za safari, wanapofuata watuhumiwa kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine hawalipwi. Sasa, naishauri Serikali kwa vile katika ripoti ya CAG imebainisha kuwa fedha zinazokusanywa kwenye Mfuko wa Polisi ambazo ni tuzo na tozo, hazipangiwi sheria na kanuni za matumizi yake. Sheria na matumizi yake yaratibiwe kwa mujibu wa Sheria ya Fedha iliyokuwepo nchini ili ziweze kuondoa hizo changamoto za maaskari wadogo na stahiki zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile nashauri fedha hizo aidha zitumike kwa ujenzi wa vituo vya polisi pamoja na nyumba za askari ambazo zimechakaa sana. Mashirika na taasisi za umma ziache mara moja kujiingiza kwenye shughuli zinazoweza kufanywa na vijana wetu na akinamama ambao wanataabika na ukosefu wa ajira kama vile usafishaji wa barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naunga mkono hoja. (Makofi)