Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nami nimesimama kuunga hoja ya Mheshimiwa Eng. Ezra. Kama Taifa ni lazima tuwekeze kwenye elimu, in a serious way we need to invest in human capital. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama Taifa na sisi ni lazima tuzalishe wataalam wa kuweza kuwauza nje, kama vile tunaona mataifa mengine madaktari wanatoka huko India, sijui China na kwingineko, ma-engineer, kama Taifa lazima tutengeneze wataalam na sisi ambao tunaweza tukawauza nje na ndiyo tunaweza kufikia huo uchumi wa kati ambao tunaufukuzia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi kwa kweli nashangaa sana. Nashangaa kwa nini, tunapata hii crisis, kila mwaka unakuta watoto wanaopata hii mikopo ni wachache wengine wanaachwa na Serikali inakuja inaona kabisa, hai- assume inakuwa imesha-project kwamba, kwa bajeti hii ambayo tunaomba pamoja na makusanyo ambayo tutakuwa tumechukua, kama ilivyosema mwaka jana imekusanya asilimia 78 tunao uhakika kulingana na trend ya ufaulu wa hawa wanafunzi, kwa sababu lazima mnaangalia trend, mwaka jana 2020 form six walimaliza hawa, katika hawa waliomaliza walio-qualify kwa mikopo, let say walikuwa ni 60%. 2021 you have that trend, kwa kufuatana na hiyo trend mnakuwa mnajua kabisa 2022 tutaweza kupata wahusika wambao wanaweza wakaomba in the likeliness kama asimia hizi na bajeti ambayo tumeomba ni hii.

Mheshimiwa Spika, sasa nikataka nijue Serikali inafanya tafiti ya kina kujua uhitaji halisi wa watoto hawa wa Kitanzania ambao unakuta wengi wao wamesomeshwa kwa shida sana. Kuna wengine wanafanya kuchangishiwa wakati wanaenda shule, unamchangishia akiwa sekondari, high school, unachangishiwa na wanakijiji na wengine, wakifika huko wanashindwa kupata mikopo wanabaki mtaani. Mama hawezi ku-afford hata 200,000/= leave alone hizo 5,000,000/= alizosema Mheshimiwa Ezra hapa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nikataka nijue Mheshimiwa mwenye hoja, Mheshimiwa Ezra, katika maazimio yake mojawapo, nimesema kuanzia mwanzo, tuwekeze katika elimu tuweze kuwa na vyanzo mbadala. Tuwe na chanzo mbadala kabisa na hiki chanzo tuki-ring fence kama tatizo ni hela hazitoki, kiwe ring fenced kama inavyokuwa kwenye REA, tunajua kabisa hii ni kwa ajili ya elimu ya juu, mikopo. Iwekwe kama tunajua itapatikana sehemu gani tutakuwa tunapata kiasi fulani kama ilivyo kwenye REA, ili sasa watoto wetu wote wanaofaulu wanakuwa na sifa waweze Kwenda Chuo Kikuu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili huko nyuma, mpaka Mheshimiwa Tendega hapa ananiambia na yeye alinufaika, wazazi wetu walivyokuwa wanafika CHUO Kikuu walikuwa wanasomeshwa bure. Kama tunaona hapa tunaacha Watanzania wengi wa kimaskini nje na itakuwa ni motisha, wanaopata daraja la kwanza Serikali si tunawekeza kwenye elimu na ndio maana imewekwa kwenye kasma ya maendeleo, wanaopata daraja la kwanza tuwasomeshe bure, siyo mkopo, hao wengine sasa ndiyo tuwape huo mkopo. Hii itatoa motisha sana I am telling you, watafaulu kama nyuma waliweza wazazi wetu wamesoma bure, why not now? Tunaweza kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama tunaweza kuwekeza tukatoa fedha tukajenga barabara, tukajenga maji, tuone human capital na yenyewe ni asset. Ni kitu muhimu sana cha kuweza kuwekeza kwenye Taifa, kama tunavyosema tunawezekeza kwenye barabara, kwenye maji, human capital ni kitu muhimu sana kwenye Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa wale wanaopata division one wasomeshwe na Serikali, wanaopata division one unaweza ukasema hata division one ya kufikia point fulani ambayo itachagiza sana. Let say kama mnataka muweke kwenye sayansi, wanaopata division one at this point wanasomeshwa bure, itachagiza sana bila kubagua amesoma private, amesoma public, sijui amesomeshwa nan ani kwa sababu amefikisha hizo sifa basi aweze kupata huo mkopo, na hao wengine ambao wanafuata sasa ndiyo labda waweze kukopeshwa.

Mheshimiwa Spika, simu ni nyingi, malalamiko ni mengi, Watanzania masikini kabisa watoto wao wamefaulu vizuri na wako nyumbani hawawezi Kwenda shule. Ni kitu ambacho ni cha muhimu sana na cha uharaka kuweza kufanyiwa kazi. Baada ya kusema hayo naomba kuwasilisha. (Makofi)