Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia hoja ya Mheshimiwa Ezra Chiwelesa, kuhusu hili suala la malipo wanayolipa wanafunzi wanapokuwa katika vyuo vikuu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Ezra na naomba niichambue kiuchumi na kisiasa. Dira ya Taifa 2025 ina malengo Matano. Mojawapo ya malengo ni kujenga jamii ya watu walioelimika na wenye uchu wa kujifunza. Kwa hiyo, mtu akikuuliza kwamba 2025 tutafika, kwa speed hii tutakwama, lakini kwa sababu tumeona, naona Mheshimiwa Ezra ametusaidia tunakwenda kukwamua ili tuweze kujenga jamii ya watu walioelimika na wenye uchu wa kujifunza.

Mheshimiwa Spika, kiuchumi kwa haraka haraka nimeangalia kipato cha Mtanzania, income per capita, najua kinachomsumbua Mheshimiwa Ezra, mkoa wake ndiyo ambao una pato dogo. Kwa hiyo, wakuu wa vyuo mkoa wa Mheshimiwa Ezra ukumbukwe sana, ndio una pato dogo. Ila per capital income ya Watanzania ni Dola 1,040. Sasa Dola 1,040 angalia mwanafunzi anayekwenda kusoma shule ya milioni tano kwa mwaka, ataweza vipi na mzazi huyo ana watoto nne mpaka watano?

Mheshimiwa Spika, lengo la Taifa ni kuelimisha watu bila kubagua, lakini kuna fani zinazopendelewa. Ninachoshauri, hapa kuna suala la haraka la kuokoa hii hali na suala linalohitaji mchakato wa miezi mitatu, minne, mpaka sita tufanye maamuzi. Suala la haraka kama walivyodokeza wenzangu, kama mjomba Chumi alivyosema, tutafute namna ya haraka, hawa wenye sifa tuwabebe wote kama walivyo waende wasome, waendelee na shule. Wanapoendelea sisi huku tuweze kwenda kutafuta mpango wa muda mrefu, nami mpango wa muda mrefu kwangu ni miezi sita.

Mheshimiwa Spika, kisiasa nimekwazika, kama mfumo huu tukiendelea nao ambao tuliutengeneza kwa nia njema, lakini umekwama; nami sioni tatizo, unatengeneza formation, inakwama unabadilisha, unatengeneza formation nyingine, unatoka na magoli. Mfumo huu kwenye Chama cha Mapinduzi umekwama, tunakwenda kujenga matabaka wana-CCM wenzangu. Huu mfumo unakwenda kutupeleka kwenye matabaka, hawa wapate hawa wasipate.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kanyasu amebahatika mwanaye yuko chuo kikuu wakamwambia, kuna mzazi hana mtoto chuo kikuu, atasemewa na nani? Kwa hiyo, nawasihi, tuweze kutafuta wepesi wa haraka kuwakomboa wote hao wenye sifa waende chuoni, halafu turudi tuje tutengeneze mipango ya muda mrefu. Mojawapo ya sababu za kufanya, naweza nisishiriki kwenye mchakato huo, hizo fani mnazotaka kupeleka watoto za Shilingi milioni tano, hebu fikiria vyuo vya namna hiyo mvipe ruzuku. Yaani course inapewa ruzuku kabla ya mtoto, kwamba ukienda kusoma udaktari wewe, ni shilingi milioni moja au ni laki saba, kusudi watu waende kule. Ukienda kwenye u-pilot ni shilingi laki tatu, kusudi wale watoto wanaomudu waende kule.

Mheshimiwa Spika, langu ni kuunga mkono hoja kwa sababu wanaolia ni wengi, Mheshimiwa Chiwelesa alilolisema ametusemea wote, amewasemea Watanzania wote.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)